data:post.body JINSI UNAVYOWEZA KUPUNGUA UZITO KIRAHISI KIPINDI HIKI CHA CORONA. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

JINSI UNAVYOWEZA KUPUNGUA UZITO KIRAHISI KIPINDI HIKI CHA CORONA.

Kipindi hichi ambacho watu wengi wanakaa nyumbani ni kipindi muhimu sana cha kubadlisha maisha yako ya kimwili na kiakili kama ukiamua kufanya hivyo kutoka moyoni.
kuna sababu nyingi ambazo zimekua zikiwazuia watu kupungua uzito kama kukosa muda wa mazoezi sababu ya kazi, kushindwa kufanya diet sababu ya kula nje ya nyumbani muda mwingi, kukosa nidhamu ya kula sababu ya presha ya marafiki kwenda kunywa pombe na kula vyakula mahotelini na bar siku za mwisho wa wiki ambapo kwa kiasi kikubwa imekua ikirudisha nyuma juhudi zao za kupungua.
Lakini kwa kipindi hiki ambacho muda mwingi unautumia nyumbani basi kuna mabadiliko makubwa ya kimuonekano unaweza kufanya afya yako iwe bora zaidi.
kuna mambo matatu ya msingi unaweza kufanya sasa hivi kama ifuatavyo.
chakula; punguza ulaji wa mazoea na uanze kula kama mtu anayetaka kupungua uzito kweli, kuna diet za aina nyingi sana kikubwa chukua moja ambayo unaiweza na uende nayo taratibu mpaka utakapopata matokeo.
Na kwasababu uko nyumbani sasa hivi basi unaweza kupika diet yeyote unayotaka, kama huna diet chukua hii http://www.sirizaafyabora.info/2018/01/ufahamu-mpangilio-bora-wa-chakula.html usitamani wanachokula wenzako ambao ni wembamba, wewe ndio unajua unataka nini hivo fuata malengo yako.
mazoezi; sasa hivi una muda mwingi sana wa mazoezi kiasi kwamba unaweza ukafanya asubuhi na jioni kwa masaa mengi kwasababu huna pakwenda, hata ukichoka sana kesho utalala mpaka usingizi uishe.
Tafuta kampani ya mazoezi hapo hapo nyumbani ili kupata motisha, unaweza kuruka kamba au kukimbia na yote ni sawa.
kipindi hiki sio salama sana kwenda gym hivyo fanya mazoezi nyumbani.

.weka malengo rasmi ya kupungua uzito; watu wengi wanaotaka kupungua uzito hawana malengo, mara nyingi wanaamka na kiu kubwa ya kupungua kisha kiu hiyo inaisha baada ya wiki moja.
kwa diet ya kawaida kabisa ambayo haina stress sana unaweza kupungua kilo mbili kwa mwezi, kwa maneno rahisi ni kwamba ukikomaa upungue kilo mbili kila mwezi basi utapungua kilo 24 kwa mwaka hivyo hata kama una uzito kiasi gani baada ya muda utaisha tu. kwa mtu wenye kitambi tu ila sio mnene anahitaji miezi mitatu tu kukimaliza.

weka malengo ya siku, wiki,mwezi na mwaka kisha yafuate na mabadiliko utayaona, kumbuka huwezi kubadilisha chochote kwenye maisha yako kwa kuishi kwa mazoea lazima ubadilishe kitu ili upate kitu.

                                                                STAY ALIVE

                                   DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO.(MD)
                                                     0653095635/0769846183

0 maoni:

Chapisha Maoni