David
Duncan Kipeta
Dunia
imevamiwa na adui ambaye kwa kiasi kikubwa sisi kama wakazi wa dunia yetu
hatukuwa tumejiandaa kubabiliana naye. Ametumavia na kutupiga na kisha
kutusambaratisha kila mtu na kwake, watu wamejifungia na hawathubutu kutoka nje
huku baadhi ya mataifa watu wanaendelea na shughuli zao za kiuchumi za kila
siku lakini wakiwa na hofu na wenye tahadhari kubwa wakiogopa kukutana na huyu
adui mkubwa na mbaya mwenye kusababisha watu kupata homa kali, mafua makali,
vichwa kuuma na mbaya zaidi wanapata homa kali sana ya mapafu yenye kusababisha
mfumo wa upumuaji kuwa wa shida. Hali inakuwa mbaya sana kwa ndugu zetu wenye
magonjwa ya muda mrefu na yenye kuathiri sana mfumo wa kinga wa mwili. Magonjwa
kama kisukari, kifua kikuu, shinikizo la damu, virusi vya ukimwi/Ukimwi
yanaongeza hatari ya madhara yatokanayo na adui yetu huyu. Huyu adui anaitwa CORONA
VIRUS INFECTION DISEASE OF 2019 (COVID19).
COVID19
ni ugonjwa unaosababishwa na maambukizi ya virusi vya corona ambayo huambukizwa
haswa kwa kushika au kugusa majimaji yanayotoka kwa mtu mwenye maambukizi hayo.
Ugonjwa huu ulianzia na kugunduliwa huko nchini China katika mji wa Wuhan
mwishoni mwa mwaka 2019 na ulianza kushamili kuanzia mwezi wa Disemba mwaka
huo. Ugonjwa huu uligunduliwa na Daktari Lee Chen ambaye alifarika hapo baadaye
kwa maambukizi ya COVID19. Njia zinazosababisha kuenea kwa ugonjwa huu ni
kuvuta hewa yenye viini vya virusi vya corona, kushikana mikono, kugusa nguo za
muathirika wa virusi vya corona, kushika vitu vilivyoshikwa na mtu mwenye
virusi vya corona.
NAMNA
YA KUJIKINGA NA COVID19
Nchi
nyingi zimeweka namna ya kupunguza maambukizi ya ugonjwa huu kwa kuzuia
mikusanyiko ya wananchi, kusisitiza kanuni bora za afya hasa kwa kunawa mikono
na sabuni au vitakasa mikono(hand sanitizer), kuvaa barakoa (face masks) na
zuio la kuchangamana (social distancing). Lakini jambo kubwa na muhimu
linalofanywa kwa watu wanaohisiwa kuwa na maambukizi ni kuzuiwa kuchangamana na
watu wasiohisiwa kuwa kuwa na maambukizi. Njia hii inatambulika kama karantini.
Karantini ni kitendo cha kuzuia au kujizuia
kutokuchagamana na watu wengine ikiwa mtu fulani amehisiwa au anahisi kwamba
amepata maambukizi ya magonjwa ya kuambukiza ikiwa tiba au chanjo ya ugonjwa
huo haijapatikana. Wikipedia kamusi inaeleza kuwa “karantini
inamaanisha kuzuia miendo ya watu ambao wanaweza kuathiriwa na ugonjwa wa
kuambukiza ilhali ugonjwa kwao haukuweza kuthibitishwa bado… karantini hutumiwa
pia kama mgonjwa anazuiliwa kukutana na watu wengine ili kuzuia uenezaji wa
ugonjwa hatari. Karantini inaweza kutumika kwa wanadamu, lakini pia kwa wanyama
wa aina mbalimbali, na wote kama sehemu ya udhibiti wa mpakani na ndani ya nchi”.
Ingawa
karantini hufanana zaidi na kutengwa, maneno haya mawili yanamaana tofauti.
Kutengwa ni kitendo cha kumuweka mtu aliyethibitika kuwa na maambukizi ya
ugonjwa wa kuambukiza mbali na watu wengine ili kuzuia maambukizi yasienee.
Kikawaida karantini huwekwa kwa muda wa siku
arobaini
(40) Japokuwa
inaweza kuwa muda wa siku kadhaa kuanzia saba (7) na kuendelea.
NAMNA
YA KUFAIDIKA NA KARANTINI
Katazo la kutembea na kuchanganyika na watu
lina faida sana kwa nchi ili kuzuia kuenea kwa maambukizi na hivyo kufanya
mamlaka za afya kuwa na mzigo mdogo katika kushughulikia watu wachache wenye
maambukizi na wenye dalili za maambukizi. Karantini husaidia katika kufuatilia
mienendo ya watu na kufuatilia visa vya maambukizi kwa urahisi na umakini
mkubwa. Hii husaidia pia katika kupunguza matumizi ya vifaa tiba ambavyo vingetumika
kwa watu wengi ambao wangeambukizwa.
Pamoja na faida zote hizo kwa nchi au jamii
fulani pia mtu mmoja mmpoja anaweza kufaidika sana kwa uwepo wa karantini.
Faida hizo zaweza kuwa za kiafya, kiuchumi, kimahusiano au kijamii. Katika
makala hii tutangalia namna unavyoweza kufaidika na karantini.
Sura
ya Kwanza
AFYA
Karantini
inaweza kuwa na faida sana kwa mtu binafsi ikiwa ataliangalia jambo hili kama
nafasi ya pekee ya kujenga afya njema ya mwili wake. Kabla ya karantini watu
wengi hawajali afya zao kama inavyotakiwa kwani watu hawalali kwa muda wa
kutosha, kula vizuri na kwa kutulia, kupata muda mwingi wa kujisomea na hata
kufanya mazoezi na kadharika lakini wakati wa karantini unaweza kumsaidia mtu
kujenga afya bora ya mwili wake ikiwa ataliangalia jambo hili katika mtazamo
chanya. Afya bora wakati huu wa karantini inaweza kujengwa kwa kuzingatia mambo
yafuatayo:
Kupata
muda wa kutosha wa kupumzika.
Kitabibu
mtu mzima anatakiwa kupata muda usiopungua masaa nane (8) ili kupumzika. Muda
huu unatakiwa kutumiwa hasa kwa kulala. Watu wengi wanakosa muda wa kutosha ili
mkulala wakati wa usiku. Kulala masaa nane wakati wa usiku ni muhimu sana ili
kujenga afya bora ya akili,mfumo wa uzazi, mfumo wa kinga, mfumo wa utoaji taka
mwili na hata mmeng’enyo bora wa chakula.
Kukosa muda wa kutosha wa kulala husababisha
kutengenezwa kwa kemikali kama cortisol ambayo huharibu sana afya ya akili na
hata viungo vingi vya mwili ikiwemo moyo, maini, figo na hata viungo vya uzazi
kutokana na uwingi wa kemikali hii katika damu. Ubongo huanza kukosa kupumzika
na hivyo huweza pia kumfanya mtu akose usingizi na baada ya muda mrefu mtu
anaweza kupata magonjwa ya akili ikiwemo hasira za karibu zisizo na sababu,
kiharusi, msongo wa mawazo na hata sonona.
Mfumo
wa kinga huathiriwa sana ukosefu wa usingizi kwa sababu ya uwepo mkubwa wa
kemikali ya cortisol ambayo huathiri na hta kuua seli lindaji (white
blood cells) zinatotumika kulinda mwili dhidi ya magonjwa. Hivyo ili kuwa na
mfumo wa kinga ulio boira na imara ni muhimu sasna kupata muda mwingi wa
kulala.
Kukosa
muda wa kulala wa kutosha huathiri sana mfumo wa uzazi. Na hii ni moja kati ya
sababu kubwa sana za upungufu wa nguvu za kiume, kukosa hamu ya tendo la ndoa
kwa wanawake na wanaume na hata kukosa kufurahia tendo la ndoa. Tafiti mbali
mbali zimefanyika na kuonyesha kwamba ukosefu wa usingizi hupunguza uzalishaji
wa homoni ya kiume iitwayo testosterone ambayo ndio hufanya kazi ya
kuongeza msukumo au hamu ya kufanya tendo la ndoa. Homoni hii ipo kwa uwingi
sana kwa wanaume na kwa kiwango kidogo kwa wanawake. Homoni hii pia hujulikana
sana kama sexual driver yaani kiamshi au kisukumo cha kufanya tendo la
ndoa. Hivyo ukitaka kuwa na afya njema ya mfumo wa uzazi na kufanya vizuri na
kufurahia tendo la ndoa, usingizi ni muhimu sana. Kipindi hiki cha karantini ni
kipindi cha wewe kuirudisha na kujenga heshima katika kitanda chako na mwezi
wako lakini tu itafanyika hivyo ukipata muda mwingi wa kupumzika kila siku.
Hizo
pamoja na athari zingine kama mmeng’enyo mbaya wa chakula, kuharibika kwa mfumo
wa utoaji takamwili ambao huathiri sana figo na maini zinasababishwa kukosa
muda wa kutosha wa kulala hivyo katika kipindi hiki cha karantini ni muhimu
sana kupata muda wa kutosha kupumzika kwa kulala usingizi si chini ya masaa nane
(8) kwa mtu mzima na mtoto kuanzia masaa kumi (10). Usingizi ni Afya.
Kula
Vizuri
Chakula ni afya. Ili kuwa
na afya bora ni muhimu kuzifuata kanuni za afya ikiwepo kula chakula bora.
Kabla ya karantini watu wengi hula vyakula visivyo vizuri na visivyo na
virutubisho vya kutosha ili kujenga afya bora. Vyakula maarufum kama fast foods
au junk food mfano wa chips zinazouzwa, vinapoliwa mara kwa mara na kwa muda
mrefu hudhoofisha afya kwa kuzorotesha mifumo mbali ya mwili wa binadamu.
Vyakula vya kujenga mwili, vyakula vya kulinda mwili na vya kuupa mwili nguvu
hutakiwa kutumiwa kwa uwingi kwa kipindi hiki cha karantini.
Vyakula vya kujenga mwili kama maziwa, mayai,
samaki, nyama, maharage na mboga za majani pamoja na vile vya kulinda mwili
kama maini, samaki, mboga za majani, matunda ni muhimu na vinahitajika kwa
kiwango kikubwa sana kwa kipindi hiki cha karantini bila kusahau vyakula vya
kuupa mwili nguvu ili kuendelea na shughuli nyine muhimu za nyumbani.
Kufanya
Mazoezi
Katika
kuhakikisha umuhimu wa mazoezi katika kipindi hiki cha karantini, hivi karibuni
Mheshimiwa Raisi wa Jamhuri ya Uganda, Yoweri Kaguta Mseveni alionekana katika
picha na mitandao ya kijamii akiwa nyumbani kwake akifanya mazoezi mbalimbali
ya viungo ikiwemo push up. Alifanya hivi ili kuhimiza umma kuhusu umuhimu wa
mazoezi ya viungo huku wakiendelea kubakia ndani katika makazi yao na si
kufanyia mazoezi nje kwenye umati wa watu kama gym na hata katika viwanja vya
mazoezi au kukimbia nje. Jambo hili la kufanya mazoezi nje au mbali na makazi
huweza kuongea hatari ya kupata maambukizi ya vizuri vya COVID19. Uwepo wa
katazo la kutoka nje na kuchangamana na watu kwa sababu ya kuogopa kuenea kwa
COVID19 sio sababu na isiwe sababu ya kuacha kufanya mazoezi ya viungo. Unaweza
kufanya mazoezi ya kutosha hata katika chumba chako cha kulala. Hivyo naomba
nikusihi kuendelea kufanya mazoezi ya viungo kila siku na katika makazi yako. Mwanasaikolojia
na mwandishi wa kitabu cha The Barbarians at the PTA anashauri kuwa “Endelea
kufanya mazoezi na rafiki zako. Ikiwa unapata uvivu kufanya mazoezi peke yako,
unaweza kupanga ratiba na rafiki zako ili kufanya mazoezi kama yoga na
mengineyo kwa njia ya video katika muda mmoja”[1]
Kumbuka:
Afya yako ni mtaji wako na mtaji huu hujengwa na mkukuzwa kwa kula chakula bora,
kulala vizuri na kufanya mazoezi.
Nakutakia heri katika kuendelea kujenga mtaji
wako.

UCHUMI
Kipindi
inapotanghazwa karantini ni kipindi ambacho hofu ya kudorora kwa uchumi huwa
kubwa sana. Uchumi hudorora kwa kwa watu binafsi, makampuni na hivyo hata kwa
taifa. Hofu hii huwa kubwa kutokana na ukweli kwamba watu hupunguza kwenda
kazini na wengine huacha kabisa. Kutokana na kutofanyika kwa shughuli za
kiuchumi, watu huweza kuwa na hali mbaya kiuchumi hasa wale wasio na ajira za
kudumu au waliojiajiri wenyewe. Lakini kwa shghuli zisizohamishika au
zinazohitaji uwepo wa mtu husika mahali pa kazi hali yaweza kuwa mbaya zaidi
tofauti na zile zinazoweza kuhamishika.
Pamoja
na ukweli huu wa mabadiliko ya kiuchumi bado tunaweza kuwa na tumaini la
kufanya kazi kama kawaida lakini kwa mfumo mwingine. Natamani uangalie mfano wa
Mwandishi wa habari na mchekeshaji wa kipindi cha televisheni cha The Daily
Show cha nchini Marekani Ndugu Trevor Noah. Yeye ameendelea na shughuli
zake za kutoa habari na kuchekesha huku akisalia katika makazi yake. Muongozaji
na mchekeshaji wa kipindi cha The Hellen Show, Hellen amekua akiendelea
na kazi zake kama kawaida lakini akiwa katika makazi yake. Lakini pia mmiliki
wa kampuni ya Zoom Video Communications inayoongoza kwa utoaji wa huduma
ya mikutano kwa njia ya video (Video teleconferencing) ndugu Eric Yuan amekuwa
akiendelea kufanya kazi na mikutano yake kwa njia ya video. Njia hii ni njia
maarufu ikiwa kuna vizingiti kama hivi ya karantini au kutokana na umbali wa
wahusika. Pia kulingana na aina za kazi hasa za kiofisi, watu hufanya kazi zao
majumbani katika kompyuta na kuzituma katika ofisi zao. Hivyo kufanya shughuli
zao kama kawaida.
Kipindi
hiki cha karantini kikitumiwa vizuri kinaweza kuwa cha faida kubwa kwa mtu
mmoja mmoja. Kuna mambo mengi ambayo mtu anaweza kuyafanya ambayop yakaleta
faida kubwa kwa uchumi binafsi na kwa nchi nzima kwani watu wengi hukaa
nyumbani. Mambo haya ni kama yafuatayo:
Kuongeza
ujuzi wa kiuchumi
Kipindi
hiki cha karantini kinaweza kutumiwa katika kuongeza ujuzi katika fani mbali
mabali za maisha kwani watu wengi wanakuwa huru na hawajabanwa na majukumu
mengi. Ujuzi huu huweza kuongezwa kwa kusoma vitabu au kutembelea tovuti
mbalimbali zenye kufundisha maudhui ya kazi fulani na hata namna bora ya
kufanya uwekezaji.
Biashara
za mitandaoni na uwekezaji (Online marketing and investments).
Hizi
ni aiana za biashara ambazo hufanyika kwa njia ya mtandao na mara zote
haihitaji wahusika kukutana kwani mnunuzi huagiza mahitaji yake na kuyalipia
kwa njia ya mtandao na kisha mahitaji yake hayo hutumwa kwa njia ya posta au
kuletewa hadi katika makazi yake na mtu mwingine ambaye hufanya kazi ya kubeba
mizigo.
Uwekezaji
wa mitandaoni ni njia nzuri pia kwa kipindi hiki kwani huweza kufanya uchumi
wako baada ya kipindi cha karantini ya COVID19 kuwa mzuri. Uwekezaji huu huweza
kutumia mitandao kama Expert option
Tahadhari:
Ni
muhimu kutambua kwamba katika kipindi hiki ni muhimu kuwa na fedha ya akiba ili
kuweza kuhudumia mahitaji ya familia. Hivyo tahadhari zote za kiuchumi inabidi
zichukuliwe ili kuhakikisha kwamba hupati shida katika kipindi hiki kigumu.
Kutoa
elimu au kozi mbalimbali kwa njia ya video au mitandao ya kijamii
Ikiwa
una ujuzi au utaalamu juu ya kitu fulani basi usikate tamaa, kipindi hiki cha
karantini unaweza kuendelea kutoa elimu kwa kupitia mitandao ya kijamii na hata
baadhi ya mada kuwafikia watu wengi zaidi kuliko kipindi kingine chochcote
kwani watu wako huru na wana muda wa kutosha kusoma na kujifunza zaidi kwa
kupitia mitandao hii ya kijamii.
Kununua
Hisa
Baadhi
ya makampuni ya biashara yanaendelea kufanya vizuri katika masoko yake kutoka
na utengenezaji bora wa bidhaa na huduma zingine zitolewazo. Makampuni haya
yanauza hisa na ikiwa una akiba ya kutosha ni muhimu kuwekeza katika kununua
hisa ili kuendelea kupata faida ambayo itakusaidia kuinuka kiuchumi baada ya
karantini ya COVID19 kuisha.
Kufanya
kazi za muda wa kujitegemea (freelancing)
Hizi
ni kazi ambazo mtu fulani hufanya kwa muda wake aliojipangia na baada ya
kumaliza hupata ujira wake hivyo anaweza kuendelea au akaacha baada ya malipo.
Mtu mmoja huweza kujifanya kazi mbalimbali kwa kujipangia muda wake mwenyewe.
Njia hii huweza kuingiza kipato kikubwa kwa muda mfupi. Baadhi ya programu
tumizi (application) kama Freelancer na zinginezo ni nzuri kwa kazi hizi
kwa kipindi kama hiki.
Sura
ya Tatu
MAHUSIANO
Mahusianona
wengine ni jambo la kwanza kwa kiumbe chochote. Hii ni zawadi kubwa ya Mungu
toka kuumbwa kwetu. Mahusiano baina ya watu ni jambo la msingi ambalo
linatakiwa kuendelezwa katika kipindi hiki kigumu cha karantini.
Katika
kipindi hiki, Mahusiano yanaweza kujengwa na kuwa mahusiano thabiti na imara au
yanaweza kuharibika kwa sababu mbalimbali. Mahusiano yanajengwa na ukaribu wa
watu katika muda fulani. Watu wengi huwa na mahusiano mazuri kwa sababu
wanaonana mara kwa mara na hivyo huwasiliani kwa ukaribu. Lakini katika kipindi
hiki, watu hawaonani na hivyo hupunguza mawasiliano na hata mahusiano yao
hulegea.
Baadhi
ya mahusiona yalijengwa kwa sababu watu wanaonana mara kwa mara na hivyo katika
kipindi hiki mahusiano yao yako katika kipimo ili kujua uimara wake. Katika
kipindi hiki, watu wengi wanakuwa huru na hawajabanwa na majukumu yao ya kila
siku kama katika kipindi kabla ya katazo la mikusanyiko ana kuchangamana hivyo
ni kipindi kizuri zaidi cha kujenga mahusiano na wenzi wao, watoto, familia na
hata ndugu na marafiki wengine kwani hakuna mtu mwenye majukumu mengi sana
yanayowafanya kukosa muda wa kuzungumzia mambo yao ya msingi. Zifuatazo ni
namna za kujenga mahusiano na watu wengine katika kipindi hiki;
a) Matumizi
sahihi ya muda na watu tunaowapenda
Kipindi
hiki cha karantini, watu wengi hawatokina kwenda shemu za mabali na makazi yao
hivyo hupata muda mwingi wa kuzungumza na watu wanaowapenda hasa watu wa
familia yao kama wazazi, kaka na dada, wenzi wetu, watoto wetu, ndugu, jamaa na
marafiki. Kabla ya katazo la kutembea nje au mbali na makazi yetru, watu wengi
walikosa muda wa kuzungumza na watu tunaowapenda hivyo katika kipindi hiki
tunamuda wa kutosha ili kuzungumza na kuyajenga mahusiano yetu.
b) Kuzungumza kwa kupitia vyombo vya mawasiliano
kama simu, Kompyuta (tarakirishi)
Katika
kipindi hiki cha zuio la mikusanyiko na kutotoka nje, tunaweza kuendelea
kujenga, kuimarisha na kuendeleza mawasiliano na watu wetu wa karibu kwa
kutumia simu au tarakirishi kutumiana ujumbe wa maandishi (meseji na barua
pepe) au hata ujumbe wa sauti na hivyo kuendeleza maisha yetu na mahusiano na
watu wengine.
c)
Kuzungumza kwa njia ya
video
Katika
kipindi hiki tunaweza kuendelea na mahusiano yetu na ndugu, jamaa na hata
marafiki kwa kutumia mawasiliano ya video. Mitandao mbalimbali ya kijamii kama Instagram,
Skype, Viber, FaceBook, WhatsApp, WeChat, SnapChat, Telegram,MySpace,
Tumblr, Twitter, Qzone, zoom na
mingine mingi hutoa huduma ya mawasiliano kwa njia ya video maarufu kama Video
Chat au Video Conference.
Njia
hizi na nyingine nyingi zinaweza kutumika katika kuimarisha mahusiano na watu
tunaowapenda na hata kuanzisha mahusiano mapya na watu wengine ili
kubadirishana uzoefu katika shughuli mbalimbali na nyanja mbalimbali za maisha.
Sura
ya Nne
ELIMU
NA MAARIFA
Karantini ni kipindi ambacho watu wanapata
muda ,mwingi kufanya shughuli zaqo nyingi ambazo walikosa kuzifanya kwa usahihi
au hawakuweza kuzifanya kabisa kutokana na kutingwa na majukumu mengine. Hivyo
katika kipindi hiki, matumizi mazuri ya muda yanaweza kuwa na manufaa makubwa
ikiwa tutaishi kwa malengo yakinifu.
Katika kipindi hiki ambacho shule, vyuo na
maktaba mbalimbali zimefungwa ni kipindi ambacho tunaweza kujifunza maarifa
tuliyokuwa tunatamani kuyapat kutokana na kuweli kwamba tuna muda mwingi sana
wa kuyafanya hayo. Hiki ni kipindi ambacho tunatakiwa kusoma baadhi ya vitabu
tunavyovitamani kuvisoma, kurudia vitu ambavyo hatukuvielewa vizuri tukiwa
darasani na tukajifunza zaidi kwa kutulia ili kuvielewa.
Karantini
inakupa nafasi kubwa zaidi ya kujifunza vitu mbalimbali ambavyo huweza kuwa
msaada kwa maisha yako binafsi na hata kwa jamii inayokuzunguka. Kusoma vitabu,
kutazama tamthilia, kujifunza maarifa kama kuchora, kupamba, kuandika,
kutengeneza programu tumizi, kuandika vitabu au
makala, kuandaa na kufundisha kozi fulani kwa njia ya mitandao, Kuchonga
vitu na vingine vingi tunaweza kujifunza namna ya kuvifanya katika kipindi hiki
muhimu. Zifuatazo ni njia za kupata na kutoa elimu aua maaraifa fulani:
a) Kusoma
vitabu, tafiti na makala mbalimbali
Karibu
ya asilimia 99.99% ya kila kitu hapa duniani kimeandikwa katika vitabu na
makala mbalimbali kwa kutumia tafiti au uelewa wa watu fulani juu ya jambo au
kitu fulani. Hivyo ili kujifunza zaidi katika kitu fulani tunachokitamani ni
muhimu kusoma vitabu, makala na tafito mbalimbali ili kupata ujuzi stahiki juu
ya vitu hivyo.
b) Kuwauliza
watu wenye ujuzi wa kitu fulani
Kipindi
hiki cha zuio la makusanyiko na kutembea bila sababu za msingi, kinaweza
kutumiwa kujifunza ikiwa tutawauliza watu fulani wenye ujuzi juu ya mambo
fulanai tunayotaka kuyajua. Tunaweza kuwauliza kwa kutumia barua pepe, mitandao
ya kijamii, vikao vya video, ujumbe mfupi au hata kwa kuwapigia simu na njia ya
ujumbe wa sauti.
c)
Kutazama video katika
mitandao ya kijamii kama Instagram, FaceBook na YouTube.
Watu wengi hutoa elimu na wengine hujifunza
kwa kutazama video mbalimbali na kupata maarifa wayatakayo kwa kutumia njia hii
ya mitandao ya kijamii. Waandaaji wa video hizi hufanya hivyo ili kutoa elimu
kwa jamii na hivyo ukihitaji elimu hii unapaswa kutumia vizuri mitandao ya
kijamii ili ujifunze mambo mengi mbalimbali.
Njia
hizi na nyinginezo nyingi zinawezaa kutumika na hivyo baada ya kipindi cha
karantini uinaweza kuwa mtu mwenye mafanikio zaidi kuliko ulivyo leo.
Ninakutakia
mapumziko mema na hakikisha unachukua hatua stahiki ili kujilinda na COVID19.
Kumbuka; COVID19 inazuilika, jilinde na walinde watu wote wa karibu yako.
Ahsante.
David
Duncan Kipeta
Instagram:davidduncankipeta
FaceBook:
David Kipeta
+255
659711891(WhatsApp)
+255
753 736983
0 maoni:
Chapisha Maoni