data:post.body SABABU 3 KWANINI UGONJWA WA CORONA VIRUS UNAWEZA USIWE NA MADHARA MAKUBWA AFRIKA. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

SABABU 3 KWANINI UGONJWA WA CORONA VIRUS UNAWEZA USIWE NA MADHARA MAKUBWA AFRIKA.

Kama wewe ni mfuatiliaji wa habari za BBC na CNN utagundua kwamba taarifa zinasema kwamba ni 2%  pekee ya wagonjwa wanaopata corona wanafariki dunia na habari zinaongeza kusema watu wengi wanaokufa ni umri wa miaka 81 na kuendelea na wengine ni wale wenye magonjwa sugu ambayo yanashusha kinga kama kisukari, magonjwa ya moyo,saratani na wavutaji sigara wa muda mrefu.
                                                                 
Kitakwimu 42.2% ya vifo ni umri wa miaka  80 mpaka 89, 32.4% umri wa miaka 70 mpaka 79,  8.4% umri wa miaka 60 mpaka 69 na 2.8% miaka 50 mpaka 59. Hizi  ni takwimu za vifo nchini Italy.
sasa kwa akili ya kawaida mambo yafuatayo yanaweza yakasababisha ugonjwa huu uwe wa kawaida Africa.
umri wa waafrika; kama umesoma jiographia kwenye topic ya idadi ya watu duaniani au population utagundua kwamba idadi kubwa ya waafrika ni vijana huku ikiwa na wazee wachache sana lakini pia idadi ya wazee nchi zilizoendelea ni kubwa kuliko vijana au inalingana na vijana kitu ambacho kinafanya waathirike zaidi.
chati hiyo hapo chini kushoto inaonyesha idadi ya waafrika kulingana na umri kwamba watoto na vijana ni wengi Zaidi wakati hiyo ya kulia ya ulaya inaonyesha watoto, vijana na wazee wanataka kulingana huku wakiwa na tofauti ndogo sana. 
kinga imara ya waafrika; Siku zote jamii inayopigwa na magonjwa mengi kwa muda mrefu inatengeneza kinga yenye nguvu sana, Afrika ni sehemu ambayo huwezi kuishi kama wewe ni legelege kiafya kwani utakufa tu, wataalamu wanaita survival of the fittest.
Mtu akifikisha miaka mitano tu afrika anakua amekwepa mikuki mingi ya magonjwa kuliko watu wanaokulia ulaya.
Mfano halisi ni mafua ya influenza ambayo inakadiriwa kwamba yanaua watu laki sita na elfu hamsini kila mwaka duniani na nchi nyingi ulaya zinatoa chanjo za mafua haya kila mwaka kuwalinda watu wake, chakushangaza ni kwamba chanjo hiyo haitolewi afrika kwa watu wazima na hakuna mtu ashawahi kushuhudia mafua yanamuua mwafrika.
hali ilivyo mpaka sasa hivi; kwa ushahidi wa macho yaani evidence based medicine inaonekana hatari ni ndogo sana, wakati Italy wakirekodi mpaka vifo 2000 kwa siku sisi hapa kwetu hakuna kifo wala hakuna nchi ya afrika iliyorekodi vifo vingi hivyo.
Yule mgonjwa wa kwanza Tanzania anaendelea vizuri kitu ambacho kinaleta matuamaini makubwa sana.
Lakini pia wagonjwa ambao wameripotiwa mpaka sasa hivi ni wachache afrika ukilinganisha na nchi za ulaya, japokua shirika la afya duniani WHO limekosoa na kusema kwamba afrika hakuna vipimo vya kutosha kwa hiyo hakuna uhakika wa namba zinapotajwa kwa tafsiri nyingine ni kwamba hata kama wapo hawana dalili na hawajafa na hiyo dalili nzuri.
mwisho; sijasema kwamba watu wasichukue tahadhari bali nimeandika kupunguza hofu na taharuki ambayo imeletwa na watu wengi wanaosambaza habari za uongo kuhusu ugonjwa huu.
Watu wengi wamepaniki sana lakini hakuna sababu ya kupaniki, kikubwa kusikiliza maelekezo ya shirika la afya duniani na wizara ya afya.

DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

0653095635/ 0769846183







0 maoni:

Chapisha Maoni