data:post.body FAHAMU JINSI MAGONJWA YANAVYOTENGENEZWA MAABARA KUUA WATU.(BIOTERRORISM) ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

FAHAMU JINSI MAGONJWA YANAVYOTENGENEZWA MAABARA KUUA WATU.(BIOTERRORISM)

Bioterrorism ni nini?
Hii ni njia ya kuachia virusi, bacteria au fangasi kwenye jamii ya watu, mazao au mifugo ili kuweza kuwaambukiza kwa makusudi ugonjwa fulani na kuua kila kitu chenye uhai kwenye sura ya ardhi.
Hii inawezekana kwa kutumia mabomu maalumu, chakula, maji, dawa za kupuliza na kuchoma sindano.
Silaha hizi ni moja ya silaha hatari zaidi duniani kwani zikitupwa sehemu zinahakikisha hakuna uhai unaobaki, hata samaki na wadudu wa kwenye maji hufariki.
Kumekua na tetesi nyingi sana kwamba huenda ugonjwa wa corona virus umetengenezwa makusudi kuua watu au umewaponyoka maabara lakini hakuna ushahidi wa kutosha japokua hatuwezi kupinga kwani hilo linawezekana kwa asilimia mia moja na historia ya dunia imeonyesha mataifa yalioyofanya hivyo wakati wa vita Fulani Fulani.

magonjwa haya yanatengenezwa vipi?
Gene therapy ni teknolojia ambayo ililetwa mahususi kwa ajili ya kutumika kusaidia kutibu magonjwa kama siko seli, saratani, kisukari, magonjwa ya moyo, magonjwa ya kuvuja damu na hata ukimwi kwa kubadilisha vimelea au gene ambazo zinachochea magonjwa hayo na kuweka gene mpya ambazo zinazuia magonjwa hayo.
Mpaka sasa hivi wagonjwa wengi wamefaidika na teknolojia hiyo lakini ka upande wa pili teknolojia hiyo inatumika vibaya kutengeneza magonjwa hatari na ya kutisha.
Wanasayansi huchukua vimelea au DNA ya  bacteria, virusi au fangasi kisha hutengeneza wadudu wengine wengi wa aina hiyo hiyo  kitaalamu kama cloning kisha huwabadilisha maumbile wadudu hao na kuwafanya wasiweze kutibika na dawa zilizopo.
mfano kama bacteria Fulani alikua na uwezo wa kutibiwa kwa kuharibu gamba lake la nje kitaalamu kama cell wall basi gamba lile huondolewa kwa teknolojia ya gene therapy  na kumfanya bacteria yule kushindwa kutibika.

kwanini corona virusi haitibiki sasa hivi?
Ugonjwa wa corona ulikuepo tangu mwaka 1960, na ulikua sio ugonjwa hatari lakini ghafla ulibadilika mwaka 2019 na kua ugonjwa tishio kitu ambacho kinaleta mashaka kwamba huenda virusi hao wamebadilishwa na kuongezewa nguvu maabara.
Mpaka sasa hivi hakuna mtu aliyekubali kuhusika na ugonjwa huo japokua kuna mashaka kwamba ugonjwa huu umetengenezwa.

Nchi ambazo zilitengeneza magonjwa kwenye historia ya dunia.
Mwaka 1944 wakati ya vita kuu ya pili ya dunia nchi za marekani, uingereza, urusi, china na wenzake walitengeneza maabara kubwa za kutengeneza bacteria wa anthrax, brucellosis, na sumu botulism kwa ajili ya kupambana na wapinzani wake wa japan, ujeruman na italia lakini bahati nzuri vita iliisha kabla ya silaha hizo za kibiologia hazijatumika.

Wakati wa vita ya pili ya dunia japan iliweka bacteria wa kupindupindu kwenye mito 1000 ya maji nchini china na kuua Zaidi ya watu 30000, ugonjwa huo uliendelea kuua watu hata baada ya kuisha kwa vita kuu ya pili ya dunia.

Mwaka 1979 maabara moja nchini urusi iliachia virusi vya anthrax bahati mbaya na kuua watu 66, serikali ya nchi hiyo ilipinga swala hilo lakini baadae ilikubali.

Mwaka 2001 barua ilitumwa nchini marekani ikiwa na bacteria wa anthrax ndani yake na kuua watu watano, haikufahamika barua ile ilitoka wapi.

Wakati wa vita ya mungolia, askari wake walitupa maiti zilizouawa na ugonjwa wa plague kwa wapinzani  ili kusambaza  ugonjwa huo sehemu mpya, hii ni moja ya sababu ya kuchelewa sana kuisha wa ugonjwa huo.

Tutarajie nini miaka ijayo?
kuna uwezekano mkubwa silaha hizi kutumika sana dunia hii ya sasa sababu ya kukua sana kwa teknolojia ya kutengeneza magonjwa haya na mbinu za kupambana kiuchumi kwa mataifa mbalimbali kwani vita ya silaha za kawaida zina athiri sana miundombinu, nyumba za kuishi, viwanda na miji mikubwa iliyojengwa kwa miaka mingi.

                                                                 STAY ALIVE

                                           DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                              0653095635/0769846183

Maoni 1 :

  1. Hali hii inatishia amani dunia nzima kwani hakuna aliyesalama kabisa naiomba jumuiya ya madola kuliingilia kati swala hili kwaajili ya kuinusuru dunia

    JibuFuta