Mwezi January mwaka 1918, miaka 102 iliyopita wakati vita kuu ya dunia ikielekea ukingoni dunia ilipigishwa magoti na ugonjwa mpya uliovamia ghafla.
Watu walianza kua na dalili za mafua, kichwa kuuma, homa, kikohozi na kuishiwa nguvu.
Wanahistoria wanaamini kwamba ugonjwa huu ulianzia ufaransa ambapo majeshi ya uingereza yalikua yameweka vikosi vyao kwa utitiri wa askari wengi sehemu moja.
Lakini ugonjwa huu ulipewa jina la Spanish flu, sababu uliripotiwa sana nchini Hispania, nchi nyingi ambazo zilikua zinapigana vita zilificha idadi ya wafu wao ili kumficha adui na kuongeza morali ya vita.
Ugonjwa huu ulikua ni ugonjwa hatari zaidi wa mafua kuwahi kutokea duniani na pia ni ugonjwa ulioua watu wengi kwa mpigo karne ya 20, ukisababishwa na virusi vya H1N1.
Ugonjwa huu ulishambulia moja ya tatu ya dunia yaani watu milion 500 waliugua ugonjwa huku ukiua watu Zaidi ya milion 100.
Tofauti na ugonjwa wa COVID 19 ambao unaua sana wazee na watu ambao kinga zao ziko chini kama wagonjwa wa sukari na saratani...ugonjwa huu uliua watoto chini ya miaka mitano, vijana umri wa miaka 20 mpaka 40, na watu wazima Zaidi ya miaka 65.
Kukiwa hakuna chanjo, dawa ya kutibu ugonjwa, wala antibayotiki ya kuzuia bacteria wengine kushambulia… ugonjwa ndani ya miaka miwili ugonjwa ulikua umeshaua watu wengi sana huku ukisambaa kwa kasi sana na kushambulia dunia nzima.
Mwaka 1920 ugonjwa huu ulipotea na baadae tena mwaka 2009 ugonjwa huu ulirudi tena sehemu mbalimbali duniani na kushambulia watu billion moja na laki nne huku ukiacha vifo laki tano.
Shirika la afya duniani wanaamini ugonjwa bado upo ila kwa kiasi kidogo lakini una tabia ya kulipuka kila baada ya muda Fulani.
Bahati nzuri chanjo yake ipo na dawa za kutibu ugonjwa huu kwa sasa zipo japokua wakati mwingine virusi vinakua vikali kuliko dawa na bado mtu anakufa.
Historia ya dunia imeandikwa kwa kalamu yenye damu nyingi sana, watu wengi sana wamepoteza Maisha kwa mgonjwa mbalimbali, vita, ajali na matetemeko makubwa ya dunia huku magonjwa na vita yakiua watu wengi Zaidi.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
Watu walianza kua na dalili za mafua, kichwa kuuma, homa, kikohozi na kuishiwa nguvu.
Wanahistoria wanaamini kwamba ugonjwa huu ulianzia ufaransa ambapo majeshi ya uingereza yalikua yameweka vikosi vyao kwa utitiri wa askari wengi sehemu moja.
Lakini ugonjwa huu ulipewa jina la Spanish flu, sababu uliripotiwa sana nchini Hispania, nchi nyingi ambazo zilikua zinapigana vita zilificha idadi ya wafu wao ili kumficha adui na kuongeza morali ya vita.
Ugonjwa huu ulikua ni ugonjwa hatari zaidi wa mafua kuwahi kutokea duniani na pia ni ugonjwa ulioua watu wengi kwa mpigo karne ya 20, ukisababishwa na virusi vya H1N1.
Ugonjwa huu ulishambulia moja ya tatu ya dunia yaani watu milion 500 waliugua ugonjwa huku ukiua watu Zaidi ya milion 100.
Tofauti na ugonjwa wa COVID 19 ambao unaua sana wazee na watu ambao kinga zao ziko chini kama wagonjwa wa sukari na saratani...ugonjwa huu uliua watoto chini ya miaka mitano, vijana umri wa miaka 20 mpaka 40, na watu wazima Zaidi ya miaka 65.
Kukiwa hakuna chanjo, dawa ya kutibu ugonjwa, wala antibayotiki ya kuzuia bacteria wengine kushambulia… ugonjwa ndani ya miaka miwili ugonjwa ulikua umeshaua watu wengi sana huku ukisambaa kwa kasi sana na kushambulia dunia nzima.
Mwaka 1920 ugonjwa huu ulipotea na baadae tena mwaka 2009 ugonjwa huu ulirudi tena sehemu mbalimbali duniani na kushambulia watu billion moja na laki nne huku ukiacha vifo laki tano.
Shirika la afya duniani wanaamini ugonjwa bado upo ila kwa kiasi kidogo lakini una tabia ya kulipuka kila baada ya muda Fulani.
Bahati nzuri chanjo yake ipo na dawa za kutibu ugonjwa huu kwa sasa zipo japokua wakati mwingine virusi vinakua vikali kuliko dawa na bado mtu anakufa.
Historia ya dunia imeandikwa kwa kalamu yenye damu nyingi sana, watu wengi sana wamepoteza Maisha kwa mgonjwa mbalimbali, vita, ajali na matetemeko makubwa ya dunia huku magonjwa na vita yakiua watu wengi Zaidi.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183