Huko nchini south Africa matumaini ya chanjo mpya ya virusi vya ukimwi yamefeli vibaya baada ya chanjo hiyo ambayo ndio ilikua tumaini la watafiti kushindwa kufanya kazi.
Watafiti hao wameonyesha masikitiko makubwa sana lakini wakaongeza kwamba utafiti wa chanjo hiyo lazima uendelee.
utafiti ulifanyika vipi?
Utafiti huo ambao uliwahusisha watu 5000 ulionyesha kwamba watu 252 waliathirika baada ya muda Fulani.
Dr Antony Fauci kutoka kituo hicho cha utafiti anasema kwamba kipindi hichi ambacho dunia inaumia kwa kuwepo kwa wagonjwa wengi sana wa ukimwi huku ukiacha yatima na wajane wengi na kuharibu uchumi, chanjo ya ukimwi ni muhimu sana" aliongea kwa masikitiko.
Kawaida chanjo hii hutolewa kwa watu Fulani kisha wanaachwa waendelee na Maisha yao ya kawaida kisha huenda tena kupimwa baada ya muda Fulani, kitaalamu kama cohort study.
South Africa ikiwa na wagonjwa milioni tano na laki sita mwaka 2016 ndio inaongoza duniani kwa kua na wagonjwa wengi Zaidi.
South Africa ikiwa na wagonjwa milioni tano na laki sita mwaka 2016 ndio inaongoza duniani kwa kua na wagonjwa wengi Zaidi.
kwa sasa ugonjwa huu unaweza kuzuiliwa vipi?
Kwa sasa njia pekee ya kuzuia ugonjwa huu ni kumeza aina Fulani ya dawa ambayo inazuia ukimwi lakini tofauti na chanzo za kawaida, dawa hii inataikiwa kumezwa kila siku ili ifanye kazi.
Nchini Tanzania dawa hii inapewa Zaidi wa watu ambao wana hatari sana ya kupata ugonjwa huu kama wanawake wanaojiuza na watumiaji wa madawa ya kulevya.
Kwa nchi ambazo hazina dawa hizi basi matumizi ya condom na kujizuia kufanya ngono ndio njia pekee ya kuzuia ukimwi kwani kuamini wenza bado kumeambukiza watu wengi virusi hivi.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
0 maoni:
Chapisha Maoni