Kumekua na ongezeko kubwa la watu wanene na vitambi ambao wanahitaji sana kupungua uzito, lakini tatizo kubwa liko palepale kwamba watu wanataka kupungua haraka kuliko kawaida.
Yaani unene uliopatikana kwa miaka miwili mpaka kumi mtu anataka kuupunguza kwa siku moja au wiki kitu ambacho sio cha kawaida na huweza kua hatari kiafya.
Kuna dawa maarufu sana ambazo zinauzwa sana mtaani huku zikidai kwamba zinaweza kupunguza uzito kwa muda mfupi tu.
Inasemekana baada ya kunywa dawa hizo mteja huharisha mafuta yote na baadae anakua mwembamba.
Dawa hizo ni hazina ukweli wowote na mtu anayetumia anakua haelewi kabisa jinsi mwili unavyofanya kazi na anahatarisha maisha yake kama ifuatavyo.
mtu hapungui unene ila anakonda na kusinyaa; siku zote ukiharisha unakua unatoa maji mwilini, kihesabu lita moja ya maji ni sawa na kilo moja ya uzito hivyo ukiharisha lita tano ni sawa umepungua kilo tano,na kwasababu sehemu kubwa ya mwili wa binadamu ni maji basi utasinyaa na kua mdogo.
Kwa matokeo ya haraka mtu ataona uzito umepungua lakini ni maji ndio yamepungua mwilini sio Mafuta na baada ya hapo uzito utarudi kwani utaanza kunywa maji na kurudisha yaliyopotea.
unahatarisha maisha; kuharisha sio hali ya kawaida mwilini ndio maana watu wakiugua kipindupindu hua wanakufa, kuharisha kunapoteza kiasi kikubwa cha madini ya potassium ambayo inasaidia sana misuli ya mwili na moyo.
Hali hii humfanya mgonjwa kuishiwa nguvu sana, mapigo ya moyo kutokwenda kawaida na hata kusimama kabisa kwa mapigo ya moyo na kifo.
mafuta yako hayako kwenye utumbo; hata kama kweli ingekua ukiharisha mafuta yanatoka, mafuta ambayo yanakufanya uonekane mnene yasingetoka kwani yapo chini ya ngozi yako na sio ndani ya utumbo.
Huwezi kutoa mafuta ya usoni, mgongoni na kifuani, mapajani, kifuani na tumboni kwa kuharisha tu.
mwisho; njia bora kabisa ya kupungua uzito ni kupunguza ulaji wa chakula hasa wanga na sukari, mazoezi na kupungua taratibu angalau kilo mbili kwa mwezi lakini mwisho wa siku hata ukishapungua lazima mfumo wako wa maisha ubadilike kwani mfumo wako wa maisha ya zamani ndio umekufikihsa hapa ulipo leo.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
O653095635/0769846183
Yaani unene uliopatikana kwa miaka miwili mpaka kumi mtu anataka kuupunguza kwa siku moja au wiki kitu ambacho sio cha kawaida na huweza kua hatari kiafya.
Kuna dawa maarufu sana ambazo zinauzwa sana mtaani huku zikidai kwamba zinaweza kupunguza uzito kwa muda mfupi tu.
Inasemekana baada ya kunywa dawa hizo mteja huharisha mafuta yote na baadae anakua mwembamba.
Dawa hizo ni hazina ukweli wowote na mtu anayetumia anakua haelewi kabisa jinsi mwili unavyofanya kazi na anahatarisha maisha yake kama ifuatavyo.
mtu hapungui unene ila anakonda na kusinyaa; siku zote ukiharisha unakua unatoa maji mwilini, kihesabu lita moja ya maji ni sawa na kilo moja ya uzito hivyo ukiharisha lita tano ni sawa umepungua kilo tano,na kwasababu sehemu kubwa ya mwili wa binadamu ni maji basi utasinyaa na kua mdogo.
Kwa matokeo ya haraka mtu ataona uzito umepungua lakini ni maji ndio yamepungua mwilini sio Mafuta na baada ya hapo uzito utarudi kwani utaanza kunywa maji na kurudisha yaliyopotea.
unahatarisha maisha; kuharisha sio hali ya kawaida mwilini ndio maana watu wakiugua kipindupindu hua wanakufa, kuharisha kunapoteza kiasi kikubwa cha madini ya potassium ambayo inasaidia sana misuli ya mwili na moyo.
Hali hii humfanya mgonjwa kuishiwa nguvu sana, mapigo ya moyo kutokwenda kawaida na hata kusimama kabisa kwa mapigo ya moyo na kifo.
mafuta yako hayako kwenye utumbo; hata kama kweli ingekua ukiharisha mafuta yanatoka, mafuta ambayo yanakufanya uonekane mnene yasingetoka kwani yapo chini ya ngozi yako na sio ndani ya utumbo.
Huwezi kutoa mafuta ya usoni, mgongoni na kifuani, mapajani, kifuani na tumboni kwa kuharisha tu.
mwisho; njia bora kabisa ya kupungua uzito ni kupunguza ulaji wa chakula hasa wanga na sukari, mazoezi na kupungua taratibu angalau kilo mbili kwa mwezi lakini mwisho wa siku hata ukishapungua lazima mfumo wako wa maisha ubadilike kwani mfumo wako wa maisha ya zamani ndio umekufikihsa hapa ulipo leo.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
O653095635/0769846183
0 maoni:
Chapisha Maoni