Moja ya changamoto kubwa ya kupambana na ugonjwa wa ukimwi ni kushindwa kumeza vidonge vya ARV kila siku na wakati uleule kwa maisha yako yote.
Watu wengi huchoka kumeza kutokana na madhara mbalimbali ya dawa, kumeza kwa kujificha na kushindwa hata kuhifadhi dawa hizo nyumbani sababu ya unyanyapaa mkubwa.
Hali hii hufanya wagonjwa wengi kutoanza dawa au kuacha kabisa dawa na kusubiri kufa tu baada ya kukata tamaa.
Lakini kwa sasa tumaini jipya liko njiani baada ya watafiti kugundua dawa za ARV ambazo zitatolewa kwa mfumo wa sindano badala ya vidonge.
Utafiti huo uliwasilishwa katika mkutano mkuu wa virusi vya ukimwi uliofanyika jijini paris ulionyesha kwamba dawa hizo za kuchomwa zilikua zina uwezo sawa na zile za kumeza.
Utafiti huu ulifanyika kwa watu 1000 katika nchi 16 dunaini ambapo dawa za ARV kwa jina la cabotegravir rilpivirine zilionyesha uwezo wake mzuri wa kufanya kazi.
Sindano hizi zitaweza kutumika kama pre exposure yaani unaweza kuchoma kama hujaathirika na kukaa mwezi mmoja bila kua na hatari ya kuambukizwa au post exposure ambayo unaweza kuchomwa baada ya kulala na muathirika au kujichoma sindano ambayo inahisiwa kua na damua ya muathirika.
Utafiti huu unaamini kupunguza sana maambukiziya ukimwi kwani kuriuka dozi moja tu ya kumeza inahatarisha sana maambukizi kwa mwenza wa mgonjwa lakini pia inawapa uhuru sana kwamba badala ya kua na siku 365 za kumeza dawa kwa mwaka sasa watakua na siku 12 tu kwa mwaka yaani sindano moja kila mwezi.
Mfumo huu wa kumeza vidonge pia ulileta changamoto hat kwa watoto wadogo ambao wengi wanashindwa kueza dawa hizo kutokana na uchungu au ladha mbaya na kushindwa kufuata ratiba zake vizuri.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
Watu wengi huchoka kumeza kutokana na madhara mbalimbali ya dawa, kumeza kwa kujificha na kushindwa hata kuhifadhi dawa hizo nyumbani sababu ya unyanyapaa mkubwa.
Hali hii hufanya wagonjwa wengi kutoanza dawa au kuacha kabisa dawa na kusubiri kufa tu baada ya kukata tamaa.
Lakini kwa sasa tumaini jipya liko njiani baada ya watafiti kugundua dawa za ARV ambazo zitatolewa kwa mfumo wa sindano badala ya vidonge.
Utafiti huo uliwasilishwa katika mkutano mkuu wa virusi vya ukimwi uliofanyika jijini paris ulionyesha kwamba dawa hizo za kuchomwa zilikua zina uwezo sawa na zile za kumeza.
Utafiti huu ulifanyika kwa watu 1000 katika nchi 16 dunaini ambapo dawa za ARV kwa jina la cabotegravir rilpivirine zilionyesha uwezo wake mzuri wa kufanya kazi.
Sindano hizi zitaweza kutumika kama pre exposure yaani unaweza kuchoma kama hujaathirika na kukaa mwezi mmoja bila kua na hatari ya kuambukizwa au post exposure ambayo unaweza kuchomwa baada ya kulala na muathirika au kujichoma sindano ambayo inahisiwa kua na damua ya muathirika.
Utafiti huu unaamini kupunguza sana maambukiziya ukimwi kwani kuriuka dozi moja tu ya kumeza inahatarisha sana maambukizi kwa mwenza wa mgonjwa lakini pia inawapa uhuru sana kwamba badala ya kua na siku 365 za kumeza dawa kwa mwaka sasa watakua na siku 12 tu kwa mwaka yaani sindano moja kila mwezi.
Mfumo huu wa kumeza vidonge pia ulileta changamoto hat kwa watoto wadogo ambao wengi wanashindwa kueza dawa hizo kutokana na uchungu au ladha mbaya na kushindwa kufuata ratiba zake vizuri.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
0 maoni:
Chapisha Maoni