data:post.body UZAZI WA MPANGO WA KUCHOMA SINDANO KWENYE UUME KUANZA KUTUMIKA. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

UZAZI WA MPANGO WA KUCHOMA SINDANO KWENYE UUME KUANZA KUTUMIKA.

Kwa miaka mingi njia za uzazi wa mpango zimekua zikitumika kwa wanawake tu, isipokua njia moja ya upasuaji kitaalamu kama vasectomy ndio ilikua ikutumika kwa wanaume na kwasababu njia hiyo ukiitumia huwezi kuzalisha tena basi wanaume wengi walikua wanaikwepa.
                                                                             
Njia hii mpya ya uzazi wa mpango itahusika kuchoma sindano kwenye uume imefanikiwa kwenye majaribio kwenye shirika la utafiti huko nchini india.
Akiongea na gazeti la Hindustan nchini india, Mwenyekiti wa shirika hilo la utafiti Dr.Sharma amesema kwamba dawa hiyo iko tayari inasubiri kibali cha serikali.
Utafiti huo ambao ulitumia awamu tatu, uliwahusisha watu 303 na matokeo yalionyesha kwamba dawa ilikua na uwezo wa 97.3% na ilikua na uwezo wa kudumu na kufanya kazi mpaka miaka 13.
Kitaalamu dawa hii itachomwa kwemye mirija inayotoka kwenye korodani kwenda kwenye uuume kitaalamu kama vas difference.

Wakati huohuo huko nchi marekani dawa ya uzazi wa mpango kwa wanaume kwa ajili ya kumeza imeshagunduliwa na kufanyiwa majaribio.
Watafiti wanaamini kwamba itakua tayari baada ya miaka kumi.

                                                          STAY ALIVE
                                   DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

                                               0769846183/0653095635

0 maoni:

Chapisha Maoni