Ugojwa wa ukimwi ulipogunduliwa mara ya kwanza miaka ya 1980 uliua watu wengi kwa kasi ya kutisha na wengi waliogunduliwa na ugonjwa huu walisubiri kufa tu kwani palikua hakuna tumaini lolote.
Miaka kadhaa baadae baada ya kugundulika dawa za kupunguza makali, tafiti zilionyesha kwamba mgonjwa asingeweza kuzidi miaka 20 baada ya kuambukizwa.
Kama hatakufa kwa matatizo ya ugonjwa wenyewe basi atakufa kwa madhara ya dawa hizi kama kuharibika kwa maini,figo na kadhalika.
Siku za karibuni mambo yamebadilika kidogo ambapo tafiti zinaonyesha kwamba tofauti ya mtu mwenye virusi na asiyekua navyo ni miaka 13 tu kwa maana nyingine ni kwamba kama mtu ambaye hana virusi anaishi miaka 73 basi mwenye virusi anaweza kuishi miaka 60, hesabu hii imeletwa hivi kulingana na kutofautiana kwa urefu wa maisha wa nchi tofauti.
Mtu mmoja kutoka ureno kwa jina la miguel amekua binadamu wa kwanza kufikisha umri mkubwa sana akiwa na virusi vya ukimwi.
Miguel aligunduliwa na virusi hivi miaka 16 iliyopita akiwa na umri wa miaka 84 na kwa wakati huo vipimo vilionyesha kwamba alikua ameugua kwa muda mrefu kabla bila kujua kwani alikua katika hatu ya 3 ya ugonjwa huu.
Wakati anagunduliwa na ugonjwa huu kulitokea mvutano kati ya madaktari kama kweli dawa zingemsaidia kwani umri ulikua umeenda sana lakini baadae madaktari waliamua kumpa dawa aanze.
Miguel anasema ile ilikua kama bahati kwani dawa hazikuwahi kumsumbua na sasa amefikisha miaka 100 akiwa na ugonjwa huu.
Miguel anasema kwamba hajawahi kuacha wala kuruka maumizi ya dawa tangu alipogunduliwa na ugonjwa huu.
Kwasababu ya unyayapaa ambao bado unaendelea dhidi ya wagonjwa wa ukimwi, Miguel hakupenda sura yake iwekwe hadharani lakini pia jina lake halikutajwa lote.
Historia hii inatoa mwanga kwa jamii yetu ya wagonjwa na ambao sio wagonjwa wa ukimwi kwamba kuna matumaini makubwa ya kuishi miaka mingi na kumeza dawa kwa wakati ni njia bora ya kufika huko.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
Miaka kadhaa baadae baada ya kugundulika dawa za kupunguza makali, tafiti zilionyesha kwamba mgonjwa asingeweza kuzidi miaka 20 baada ya kuambukizwa.
Kama hatakufa kwa matatizo ya ugonjwa wenyewe basi atakufa kwa madhara ya dawa hizi kama kuharibika kwa maini,figo na kadhalika.
Siku za karibuni mambo yamebadilika kidogo ambapo tafiti zinaonyesha kwamba tofauti ya mtu mwenye virusi na asiyekua navyo ni miaka 13 tu kwa maana nyingine ni kwamba kama mtu ambaye hana virusi anaishi miaka 73 basi mwenye virusi anaweza kuishi miaka 60, hesabu hii imeletwa hivi kulingana na kutofautiana kwa urefu wa maisha wa nchi tofauti.
Mtu mmoja kutoka ureno kwa jina la miguel amekua binadamu wa kwanza kufikisha umri mkubwa sana akiwa na virusi vya ukimwi.
Miguel aligunduliwa na virusi hivi miaka 16 iliyopita akiwa na umri wa miaka 84 na kwa wakati huo vipimo vilionyesha kwamba alikua ameugua kwa muda mrefu kabla bila kujua kwani alikua katika hatu ya 3 ya ugonjwa huu.
Wakati anagunduliwa na ugonjwa huu kulitokea mvutano kati ya madaktari kama kweli dawa zingemsaidia kwani umri ulikua umeenda sana lakini baadae madaktari waliamua kumpa dawa aanze.
Miguel anasema ile ilikua kama bahati kwani dawa hazikuwahi kumsumbua na sasa amefikisha miaka 100 akiwa na ugonjwa huu.
Miguel anasema kwamba hajawahi kuacha wala kuruka maumizi ya dawa tangu alipogunduliwa na ugonjwa huu.
Kwasababu ya unyayapaa ambao bado unaendelea dhidi ya wagonjwa wa ukimwi, Miguel hakupenda sura yake iwekwe hadharani lakini pia jina lake halikutajwa lote.
Historia hii inatoa mwanga kwa jamii yetu ya wagonjwa na ambao sio wagonjwa wa ukimwi kwamba kuna matumaini makubwa ya kuishi miaka mingi na kumeza dawa kwa wakati ni njia bora ya kufika huko.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
0 maoni:
Chapisha Maoni