Kwa wagonjwa wa kisukari, tatizo la kushuka sana kwa sukari ni hatari zaidi kuliko tatizo la kupanda kwa sukari.
Kwa hali ya kawaida sukari ikishuka huweza kuua ghafla lakini sukari ya kupanda haiwezi kumuua mtu ghafla, hali hii iko zaidi kwa watoto wadogo na wagonjwa wa kisukari.
Sababu mbalimbali huweza kuchangia kushuka kwa sukari ghafla ikiwemo kuchoma dawa nyingi ya kushusha sukari, kuchelewa kula, kufanya mazoezi sana,kunywa pombe na saratani za kongosho.
Wakati sukari inashuka kuna dalili za mwanzo na dalili za mwishoni, kua makini sana na dalili za mwanzoni kwani kipindi hicho ndio unakua una uwezo wa kujiokoa lakini baada ya hapo unakua huwezi tena kujiokoa bila msaada kutoka kwa watu wengine.
dalili za mwanzo za sukari kushuka.
jinsi ya kuzuia hali hii.
usichelewe kula; baada ya kuchoma dawa ya kushusha sukari au insulin basi hakikisha umekula kwa wakati ili kuzuia kuporomoka sana kwa kiwango cha sukari.
pima kiwango cha sukari; kupima mara kwa mara ni njia pekee ya kujua kiwango chako cha sukari kikoje, sio kwa ajili ya kuogopa sukari inayoshuka tu ila hata ile ya kupanda ni hatari kwa afya yako kama ikiwa imepanda muda wote.
kunywa pombe na chakula; sukari hushuka sana mgonjwa anapokunywa pombe bila chakula hivyo hakikisha umekula kwanza kabla ya kunywa pombe.
mazoezi yako yaendane na dawa unayotumia; ukifanya mazoezi sana hakikisha unapunguza dozi ya dawa unayotumia kwani mazoezi hupunguza sana sukari mwilini.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0789846183
Kwa hali ya kawaida sukari ikishuka huweza kuua ghafla lakini sukari ya kupanda haiwezi kumuua mtu ghafla, hali hii iko zaidi kwa watoto wadogo na wagonjwa wa kisukari.
Sababu mbalimbali huweza kuchangia kushuka kwa sukari ghafla ikiwemo kuchoma dawa nyingi ya kushusha sukari, kuchelewa kula, kufanya mazoezi sana,kunywa pombe na saratani za kongosho.
Wakati sukari inashuka kuna dalili za mwanzo na dalili za mwishoni, kua makini sana na dalili za mwanzoni kwani kipindi hicho ndio unakua una uwezo wa kujiokoa lakini baada ya hapo unakua huwezi tena kujiokoa bila msaada kutoka kwa watu wengine.
dalili za mwanzo za sukari kushuka.
- kizunguzungu
- kutokwa jasho
- njaa kali
- wasiwasi
- kichwa kuuma
- kuloanisha mashuka kwa jasho wakati wa usiku
- kuota ndoto za ajabu
dalili za mwisho baada ya sukari kushuka sana
- degedege
- misuli kuishiwa nguvu
- kushindwa kuongea
- kuchanganyikiwa
- kupoteza fahamu
- kuona ukungu.
vipimo
kwenye kipimo cha sukari au glucometer, pale inapokua chini ya 3.0mmol/l basi ni dalili kwamba sukari imeshuka sana na inaelekea kubaya.
matibabu
mgonjwa katika dalili za mwanzo anaweza kunywa glucose, juice au soda na kupata nafuu kisha kutafuta chakula na kukila, lakini mgonjwa wa dalili za mwisho anatakiwa akimbizwe hospitali kuwekewa sukari kwa njia ya mishipa au dripu.
ni vizuri mgonjwa wa kisukari kuwaambia ndugu zake kuhusu dalili hizi ili waweze kumsaidia ikitokea hajiwezi kabisa.
jinsi ya kuzuia hali hii.
usichelewe kula; baada ya kuchoma dawa ya kushusha sukari au insulin basi hakikisha umekula kwa wakati ili kuzuia kuporomoka sana kwa kiwango cha sukari.
pima kiwango cha sukari; kupima mara kwa mara ni njia pekee ya kujua kiwango chako cha sukari kikoje, sio kwa ajili ya kuogopa sukari inayoshuka tu ila hata ile ya kupanda ni hatari kwa afya yako kama ikiwa imepanda muda wote.
kunywa pombe na chakula; sukari hushuka sana mgonjwa anapokunywa pombe bila chakula hivyo hakikisha umekula kwanza kabla ya kunywa pombe.
mazoezi yako yaendane na dawa unayotumia; ukifanya mazoezi sana hakikisha unapunguza dozi ya dawa unayotumia kwani mazoezi hupunguza sana sukari mwilini.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0789846183
0 maoni:
Chapisha Maoni