data:post.body HIZI NDIO SABABU ZINAZOFANYE UKE WA MWANAMKE KULEGEA NA KUA MKUBWA. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIZI NDIO SABABU ZINAZOFANYE UKE WA MWANAMKE KULEGEA NA KUA MKUBWA.

Katika mambo ambayo yamepotoshwa sana kwenye jamii yetu ni kuhusu kulegea na kutanuka kwa uke wa mwanamke.
Jamii yote inaamini kwamba kulegea kwa uke kunasabishwa na mwanamke kufanya tendo la ndoa mara kwa mara, kulala na wanaume wengi au kulala na mwanaume mwenye uume mkubwa, kitu ambacho hakina ushahidi wowote kitaalamu.
                                                             
 
Ni kweli uke una tabia ya kulegea katika hatua fulani ya maisha ya mwanamke lakini kuna sababu zingine ambazo zinahusika kama ifuatavyo.
umri; kadri umri unavyozidi kwenda misuli yote ya mwili inaanza kuishiwa nguvu na ngozi kuanza kutoa makunyazi.
Katika umri wa miaka 40 mara nyingi kiwango cha homoni za uzazi ambazo zinahusika na shughuli za uke huanza kupungua na uke unaanza kulegea na kupungua kiasi cha maji.
Katika umri wa miaka 50 ambapo mara nyingi hedhi husimama, uke hua mkavu kabisa na kua mdogo mno kiasi kwamba hata tendo la ndoa linaanza kua gumu.

kuzaa watoto; kipindi cha kuzaa mtoto, uke wa mwanamke hutanuka sana ili mtoto aweze kupita vizuri, wanawake wengine huzaa watoto wakubwa kuliko wegingine.
Sasa uharibifu unaosababishwa na mtoto kutoka ni mkubwa, japokua uke hurudi kwenye hali yake ya zamani baada ya kuzaa lakini hautaweza kua kama mwanzo kabisa.

maumbile asili; kuna watu ambao wameumbwa hivyo, kwamba maumbile yao ya kike ni makubwa yaani kama jinsi wanaume wanavyokua na maumbile tofauti.
Ukisikia mwanamke anapenda uume mkubwa basi ujue maumbile yake ndio yanaridhishwa na aina hiyo lakini kuna wanawake wengine ambao uume mkubwa kwao ni mateso na maumivu makali.

mwisho; kuna mazoezi ya kubana uke yanafahamika kama kegel, kama umezaa watoto au umri umeenda na unataka kuendelea kua mbichi basi unaweza kuyafanya na misuli yako ya uke ikawa na nguvu kama mwanzo.
mazoezi haya hufanyika kwa kubana msuli ambao unafanya kazi ya kuzuia na kuachia mkojo mara kwa mara.

                                                                     STAY ALIVE

                                          DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                    0653095635/0769846183
                                                             

Maoni 1 :

  1. mkojo wa mwanamke hupitia katika rundu gani?

    JibuFuta