data:post.body FAHAMU KUHUSU MAJI YANAYOMWAGIKA KUTOKA KWA MWANAMKE AKIFIKA KILELENI.(squrting) ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

FAHAMU KUHUSU MAJI YANAYOMWAGIKA KUTOKA KWA MWANAMKE AKIFIKA KILELENI.(squrting)

Squrting ni nini?
Hii ni hali ya mwanamke kumwaga maji kutoka sehemu za siri wakati anafika kileleni, hii huambatana na msisimko mkali wa kuishiwa nguvu, kutetemeka hata kukaa chini.
kuna aina mbili za mwanamke kufika kileleni, moja ni hiyo niliyoandika hapo juu na ya pili ni ile mwanamke anatoa kama utando mweupe ambao unaonekana kusambaa  kwenye uume  wakati tendo hili la ndoa likiendelea, lakini maada hii itazungumzia maji yanayoruka wakati mwanamke anafika kileleni.

jee ni hali ya kawaida?
Hii ni hali ya kawaida kabisa japokua watu wengi hua hawapendi kuizungumzia, kwa miaka mingi watafiti walidhani kwamba huenda wanawake wanaomwaga yale maji wanakua na tatizo la fistula na wengine walidhani maji yale yanatoka ukeni.
Lakini utafiti uliofanyika mwaka 2014 uligundua kwamba hali ile ni ya kawaida na maji yale yanatoka kwenye kibofu cha mkojo.
Utafiti ulifanyika kwa kipimo cha utrasound ambapo mwanamke aliambiwa akakojoe ili kuondoa mkojo wote ndani ya kibofu cha mkojo kisha alianza kujichua huku kipimo cha utrasound kikiangalia hali ya kibovu cha mkojo.
utafiti ulionyesha kwamba, wakati mwanamke anaendelea kujichua maji yalianza kujaa tena kwenye kibovu cha mkojo na alipofika kileleni na kumwaga maji kama kawaida, picha ya utrasound ilionyesha kupotea kwa maji yale, hii ilionyesha kweli maji yale yanatoka kwenye kibofu cha mkojo bila mwanamke kuyatoa mwenyewe kwa hiari.

wanawake wangapi wanafika kileleni kwa staili hii?
Tafiti zinaonyesha kwamba asilimia kumi mpaka hamsini wanafika kileleni kwa kumwaga maji, lakini wataalamu wanaamini kwamba wapo ambao wanaishia kwenye hatua ya kujaza maji kwenye kibovu lakini yale maji hayatoki.
utafiti uliofanyika kwa wanawake 233 ulibaini kwamba 14% walifika kileleni kwa kumwaga maji kila wakati wakilala na wanawake huku 54% walisema hali kama hiyo ishawahi kuwakuta mara moja au mbili.
Utafiti pia unaonyesha kwamba hali ya mwanamke kumwaga maji vile hutegemea na hisia alizonazo kwa mtu huyo na uwezo wa mwanaume huyo kumkuna vizuri anapotaka yeye.

je kuna tofauti kati ya mkojo na maji yanayotoka wakati wa kufika kileleni?
Ndio, maji yanayotoka wakati wa kufika kileleni hua hayana rangi kabisa pia kuna maji yale yana kiasi kikubwa cha sukari aina ya fructose ambayo husaidia mbegu za kiume kusafiri haraka pale mwanaume anapomwaga mbegu kwenye uke huo.

mwisho; kuna wanawake wengi sana ambao wanahisi kwamba hali ile ya kumwaga maji sio yao lakini huenda hawajakutana na watu sahihi ambao wana uwezo wa kuwafanya hivyo.
badhi ya wanawake hali hii walikutana nayo baadae sana baada ya kuingia kwenye mahusiano mengine.

Maoni 2 :