Kupambana na kiasi cha Sukari kwenye damu kwa wagonjwa wa kisukari ndio msingi mkuu wa matibabu ya ugonjwa wa kisukari kwani huepusha madhara makubwa yatokanayo na ugonjwa huu kama kuharibika kwa figo, ugonjwa wa presha, upofu. matatizo ya mishipa ya fahamu na kadhalika.
Kwa kawaida sukari ya mgonjwa ikiwa zaidi ya 7.1mmol/l baada ya saa 8 bila kula au zaidi ya 10mmol/l saa 2 baada ya kula hutambulika kitaalamu kama hyperglaicemia au sukari ya juu kwa wagonjwa hawa.
nini chanzo cha kupanda sukari kwa wagonjwa hawa?
wagonjwa wengi wa sukari hupata tatizo la sukari zao kupanda sana hata kama wako kwenye dawa na hii husababishwa na sababu zifuatazo.
kutomeza au kutochoma dawa kwa wakati: wagonjwa ambao hawamezi dawa au kuchoma sindano za sukari kama walivyoelekezwa na wataalamu wa afya huishia kupata tatizo la kupanda sukari juu kuliko kawaida.
kula wanga mwingi sana; kimsingi wagonjwa wa sukari wanatakiwa wale vyakula vya wanga kidogo sana na siku zingine ikiwezekana wasile kabisa.
Vyakula vya wanga kama ugali,wali, viazi, tambi, mihogo, chapati, mikate, maandazi, keki na kadhalika huongeza sukari sana ukilinganisha na vyakula vya protini na mafuta kama nyama, samaki, karanga, korosho, maziwa, mayai, na kadhalika.
kuugua; mgonjwa wa sukari akiuugua ugonjwa wowote yaani kama malaria, typhoid, u.t.i au magonjwa yeyote mengine unayojua wewe lazima sukari ipande hivyo kwa kipindi hiki hata kama anapewa dawa za sukari, kama ugonjwa haujafahamika basi sukari haiwezi kushuka.
msongo wa mawazo; msongo wa mawazo huchangia sana homoni zingine mwilini ambazo husababisha kupanda kwa sukari kwenye damu.
kua mvivu; kama wewe ni mtu wa kufanya shughuli mbalimbali kama kutembea, kwenda kazini, kufanya kazi za nyumbani, kwenda mazoezini na kadhalika kisha ikatokea ukaacha hizo shughuli na kushinda nyumbani basi uko kwenye hatari ya kupandisha sukari mwilini.
dalili za sukari kupanda ni zipi?
Kwa kawaida sukari ya mgonjwa ikiwa zaidi ya 7.1mmol/l baada ya saa 8 bila kula au zaidi ya 10mmol/l saa 2 baada ya kula hutambulika kitaalamu kama hyperglaicemia au sukari ya juu kwa wagonjwa hawa.
nini chanzo cha kupanda sukari kwa wagonjwa hawa?
wagonjwa wengi wa sukari hupata tatizo la sukari zao kupanda sana hata kama wako kwenye dawa na hii husababishwa na sababu zifuatazo.
kutomeza au kutochoma dawa kwa wakati: wagonjwa ambao hawamezi dawa au kuchoma sindano za sukari kama walivyoelekezwa na wataalamu wa afya huishia kupata tatizo la kupanda sukari juu kuliko kawaida.
kula wanga mwingi sana; kimsingi wagonjwa wa sukari wanatakiwa wale vyakula vya wanga kidogo sana na siku zingine ikiwezekana wasile kabisa.
Vyakula vya wanga kama ugali,wali, viazi, tambi, mihogo, chapati, mikate, maandazi, keki na kadhalika huongeza sukari sana ukilinganisha na vyakula vya protini na mafuta kama nyama, samaki, karanga, korosho, maziwa, mayai, na kadhalika.
kuugua; mgonjwa wa sukari akiuugua ugonjwa wowote yaani kama malaria, typhoid, u.t.i au magonjwa yeyote mengine unayojua wewe lazima sukari ipande hivyo kwa kipindi hiki hata kama anapewa dawa za sukari, kama ugonjwa haujafahamika basi sukari haiwezi kushuka.
msongo wa mawazo; msongo wa mawazo huchangia sana homoni zingine mwilini ambazo husababisha kupanda kwa sukari kwenye damu.
kua mvivu; kama wewe ni mtu wa kufanya shughuli mbalimbali kama kutembea, kwenda kazini, kufanya kazi za nyumbani, kwenda mazoezini na kadhalika kisha ikatokea ukaacha hizo shughuli na kushinda nyumbani basi uko kwenye hatari ya kupandisha sukari mwilini.
dalili za sukari kupanda ni zipi?
- kusikia kiu sana
- kichwa kuuma
- kushindwa kutuliza akili sehemu moja.
- kuona ukungu
- kukojoa mara kwa mara
- kuishiwa nguvu
- sukari kupanda zaidi ya 10mmo/l kwenye kipimo cha damu.
hali hii ikiendelea kwa muda mrefu husababisha
- magonjwa ya ngozi ya mara kwa mara
- kuchelewa kupona kwa vidonda
- ganzi
- choo ngumu sana au kuharisha.
matibabu ya hali yapi?
matibabu ya sukari kupanda yanategemea sana chanzo cha ugonjwa husika cha kupanda kwa sukari hiyo na huweza kufanyika nyumbani au hospitali kama ifuatavyo.
kunywa maji mengi; maji mengi husaidia sana kupunguza sukari mwilini kwa kuondoa sukari kupitia mkojo lakini pia huzuia kupungua kwa maji mwilini.
fanya mazoezi; mazoezi husaidia sana kupunguza sukari, lakini ikiwa sukari imepanda usifanye mazoezi kwanza bila kuhakikisha kwamba umepima mkojo, ni hatari sana kufanya mazoezi iwapo mkojo wako una vitu vinaitwa ketones.
badili mfumo wa chakula; epuka vyakula vya wanga na sukari na tumia muda mwingi kula vyakula vya ptotini na matunda ambayo hayana sukari.
badilisha dawa; wakati mwingine dawa hazikufai au dozi ni kidogo hivyo onana na daktari wako anaweza kukubadilishia mfumo wa kumeza au akaongeza dozi.
chukua vipimo; wakati mwingine ni ugonjwa mpya unakusumbua hivyo ni vizuri kwenda hospitali kupima magonjwa mbalimbali.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183