data:post.body TATIZO LA KONDO LA NYUMA KUSHINDWA KUTOKA BAADA YA KUJIFUNGUA(RATAINED PLACENTA) ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

TATIZO LA KONDO LA NYUMA KUSHINDWA KUTOKA BAADA YA KUJIFUNGUA(RATAINED PLACENTA)

Wanawake wengi huamini kwamba safari ya uzazi huisha pale mtoto anapozaliwa, kitu ambacho mara nyingi sio kweli na ukweli ni kwamba safari hii huisha pale kondo la nyuma linapokua limetoka lote kitaalamu kama third stage of labour.

retained placenta ni nini?
Hii ni hali ambayo kondo la nyuma linashindwa kutoka nje ya kizazi nusu saa baada ya kujifungua, ni hali hatari kwa mama kwani anaweza akavuja damu mpaka kifo.

nini chanzo cha kondo la nyuma kukataa kutoka?
kuna sababu mbalimbali za kondo la nyuma kukataa kutoka kama ifuatavyo..
uchungu kidogo; hii hutokea pale baada ya kujifungua mtoto  ambapo uchungu unakua mdogo sana na kondo la nyuma linashindwa kutoka lenyewe.
kukamatwa kwa kondo la nyuma; kondo la nyuma huweza kunaswa na kushindwa kutoka hata kama uchungu upo,mara nyingi husabishwa na kufunga kwa mlango wa uzazi.
kunasa kwenye kizazi; wakati mwingine kondo la nyuma hunasa kabisa kwenye misuli ya kizazi na mara nyingi husabishwa na historia ya kuzaa kwa upasuaji.

watu gani wako kwenye hatari ya kupata tatizo hili?

  • kuzaa baada ya umri wa miaka 30
  • kuzaa kabla ya miezi tisa ya mimba.
  • uchungu kuchukua muda mrefu
  • mtoto kufia tumboni.
  • historia ya kuzaa kwa upasuaji.
dalili za tatizo hili ni zipi kwa mama mjamzito?
  • homa kali
  • maumivu makali
  • harufu sehemu za siri
  • kuvuja damu nyingi
  • kutokwa na vipande vya nyama ukeni.
matibabu
Matibabu makubwa ya hali hii ni kuhakikisha kondo la nyuma linatoka kwa njia yeyote ile, njia zinazotumika hospitalini ni kuchoma sindano ya uchungu, kuingiza mkono kwenye uke na kuondoa kawaida, au kufanyiwa upasuaji mkubwa kama kondo limenasa kwenye kizazi na kuondoa kizazi.(accreta)

                                                       STAY ALIVE

                                     DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                  0653095635/0769846183

0 maoni:

Chapisha Maoni