Mafuta ya mzaituni ni mafuta ambayo kitaalamu huitwa monosaturated yaani hua kwenye mfumo wa kimiminika kwenye joto la kawaida na huaminika kua na faida za kiafya sana mwilini.
Ukiacha kutumia mafuta ambayo huitwa saturated au ambayo yanakua mgando wakati wa hali ya hewa ya kawaida na kuanza kutumia mafuta ya haya ya mzaituni basi afya yako itapata faida zaidi.
Mafuta ya mzaituni hupunguza sana hatari ya kuugua magonjwa ya moyo kwani yameonyesha kupunguza sana kiasi cha lehemu au cholestrol mwilini ambayo ndio moja ya chanzo kikuu cha ugonjwa wa moyo.
Tafiti zingine zimeonyesha kwamba mafuta haya yana uwezo wa kupunguza kiwango cha sukari mwilini hivyo ni faida sana kwa watu wenye hatari sana ya kupata magonjwa ya kisukari, lakini pamoja na faida zake hizo hutakiwi kutumia mengi kwani yana nguvu au calories nyingi ambazo huweza kukunenepesha.
siku zote chagua mafuta ambayo yako kwenye mfumo wa kimiminika badala ya mafuta ambayo yako kwenye mfumo wa mgando.
lakini pia kumbuka huwezi kuvifanya vyakula ambavyo sio vizuri kwa afya hasa vyakula vya kukaangwa sana eti kwasababu umeongezea au umetumi mafuta haya kuandaa vyakula hivyo.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
0 maoni:
Chapisha Maoni