Kunyonya kitu chochote wakati wa kuzaliwa ni tabia ya kawaida kwa mtoto, na kama mtoto akizaliwa hawezi kunyonya basi ujue kuna tatizo sehemu.
watoto wengine huanza kunyonya vidole wakiwa tumboni mwa mama zao kabla hata ya kuzaliwa na hii ni kawaida kabisa na wakishazaliwa hupenda kunyonya vidole vyao kabla ya kwenda kulala kwani huwafanya wajisikie vizuri.
Ni umri gani mtoto anatakiwa aache kunyonya vidole?
Mtoto anatakiwa aache kujinyonya vidole alifika umri wa miezi 6 mpaka 7 na wakati mwingine mpaka miaka mitatu, lakini akiendelea kujinyonya baada ya miaka mitatu basi kuna hatari ya kuendelea kupata minyoo mara kwa mara ambayo huweza kuleta upungufu wa damu, na kuharibu mpangilio wa meno yake mpaka ukubwani.
mambo gani huweza kusaidia kuacha kunyonya vidole?
mpe zawadi; wazazi wengi hupenda kutumia adhabu kumbadilisha tabia mtoto kitaalamu kama negative reinforcement lakini unaweza kutumia njia tofauti au positive reinforcement kwa kuwapa zawadi pale wanapofanikiwa kuepuka makosa fulani.
mfano unaweza kumpa zawadi ya shilingi 200 akimaliza siku nzima bila kunyonya kidole badala ya kumchapa viboko.
weka tiki kwenye kalenda kwenye siku ambazo hakunyonya vidole na hii itampa nguvu sana.
angalia mambo yanayosababisha anyonye kidole; mara nyingi watoto hunyonya vidole wakiwa na msongo wa mawazo au wakikosa amani kwa muda fulani.
ukiliona hilo basi mkumbatie mtoto wako na kaa naye karibu au jaribu kutatua changamoto yake.
mkumbushe kiutaratibu; muonyeshe tu kwamba hupendezwi na tabia yake kwa sauti ya upole bila kufoka, binadamu ana asili ya kupingana na sheria hasa ukitumia nguvu sana kumzuia, ukimpa uhuru inakua rahisi yeye kuachana na tabia fulani.
vipi kama njia zote zikikwama?: usiwe na wasiwasi, haraka wala usitumie nguvu kubwa, endelea tu na utaratibu huo na mwishowe utafanikiwa tu kumrekebisha.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0769846183/0653095635
watoto wengine huanza kunyonya vidole wakiwa tumboni mwa mama zao kabla hata ya kuzaliwa na hii ni kawaida kabisa na wakishazaliwa hupenda kunyonya vidole vyao kabla ya kwenda kulala kwani huwafanya wajisikie vizuri.
Ni umri gani mtoto anatakiwa aache kunyonya vidole?
Mtoto anatakiwa aache kujinyonya vidole alifika umri wa miezi 6 mpaka 7 na wakati mwingine mpaka miaka mitatu, lakini akiendelea kujinyonya baada ya miaka mitatu basi kuna hatari ya kuendelea kupata minyoo mara kwa mara ambayo huweza kuleta upungufu wa damu, na kuharibu mpangilio wa meno yake mpaka ukubwani.
mambo gani huweza kusaidia kuacha kunyonya vidole?
mpe zawadi; wazazi wengi hupenda kutumia adhabu kumbadilisha tabia mtoto kitaalamu kama negative reinforcement lakini unaweza kutumia njia tofauti au positive reinforcement kwa kuwapa zawadi pale wanapofanikiwa kuepuka makosa fulani.
mfano unaweza kumpa zawadi ya shilingi 200 akimaliza siku nzima bila kunyonya kidole badala ya kumchapa viboko.
weka tiki kwenye kalenda kwenye siku ambazo hakunyonya vidole na hii itampa nguvu sana.
angalia mambo yanayosababisha anyonye kidole; mara nyingi watoto hunyonya vidole wakiwa na msongo wa mawazo au wakikosa amani kwa muda fulani.
ukiliona hilo basi mkumbatie mtoto wako na kaa naye karibu au jaribu kutatua changamoto yake.
mkumbushe kiutaratibu; muonyeshe tu kwamba hupendezwi na tabia yake kwa sauti ya upole bila kufoka, binadamu ana asili ya kupingana na sheria hasa ukitumia nguvu sana kumzuia, ukimpa uhuru inakua rahisi yeye kuachana na tabia fulani.
vipi kama njia zote zikikwama?: usiwe na wasiwasi, haraka wala usitumie nguvu kubwa, endelea tu na utaratibu huo na mwishowe utafanikiwa tu kumrekebisha.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0769846183/0653095635
Thank you for this one 🤛
JibuFuta