Huenda umesikia mara kwa mara kwamba kuna mwanaume amefia chumba cha kulala wageni baada au kabla ya kushiriki tendo la ndoa na huenda hujawahi kufuatilia ili kujua chanzo ramsi cha kifo hicho ni nini.
Naomba nikwambie kwamba moja ya sababu ya kufia chumba cha wageni ni matumizi ya dawa hizi za viagra kiholela bila kujua kama afya yako inaruhusu matumizi ya dawa hii.
Leo ntaenda kuzungumzi makundi ya watu ambao hawaruhusiwi kutumia dawa hizi kama ifuatavyo.
wagonjwa wa moyo; wagonjwa wengi wa moyo hawaruhusiwi hata kushiriki tendo la ndoa kutokana na uwezo wao mdogo wa kuhimili mazoezi lakini pia dawa ya viagra inafanya kazi kwa kusukuma damu nyingi kwenda sehemu za siri na kupanua mishipa ya damu kitu ambacho hakiwezi kuvumilika kwa wagonjwa hawa.
Mshtuko wa moyo, kusimama kwa moyo na vifo vya ghafla vimeripotiwa sana sababu ya matumizi ya dawa hii ya viagra kwa wagonjwa wa moyo.
wagonjwa wa presha ya kushuka: dawa ya viagra ilitengenezwa mwanzoni kabisa kwa ajili ya kushusha presha ya kupanda lakini baadae ikaonekana kwamba madhara yake ni kuongeza nguvu za kiume hivyo ikabidi iondolewe kwenye dawa za presha.
Hivyo kama wewe presha yako ina tabia ya kushuka basi dawa hii inaweza kukushusha mpaka presha ya sifuri na huo ndio ukawa mwisho wako.
wanaotumia dawa za presha ya kupanda; hawa wagonjwa hutumia dawa za kushusha presha kila siku, sasa kama nilivyosema hapo juu.
viagra pia inatabia ya kushusha presha hivyo kama ukiamua kuimeza basi dawa zako za presha ni vizuri usizimeze kwani presha itashuka sana na kuhatarisha maisha yako.
wagonjwa wa macho; kama una tatizo lolote la macho ukatumia dawa hii ukaona giza ghafla basi achana nayo kwani hiyo ni kengere ya hatari na unatakiwa uwahi hospitali kuonana na daktari kwani ukiendelea kutumia itakumaliza macho kabisa.
wagonjwa wa siko seli; moja ya matatizo ya siko seli ni kuzuia damu kwenye uume na kushindwa kutoka kitaalamu kama priapism.
Tatizo hili ni kubwa na huweza kusababisha kufanyika kwa upasuaji, sasa mgonjwa wa siko seli akimeza dawa hii anaongeza hatari ya kushikwa na hali hiyo kwa maana nyingine dawa hii sio salama kwake, wagonjwa wa saratani ya damu pia wana hatari hii.
wagonjwa wa chembe ya moyo; huu ugonjwa kwa kitaalamu unaitwa angina pectoris, ni maumivu ya misuli ya moyo pale moyo unapokosa hewa ya kutosha sababu ya mishipa inayopeleka damu kwenye moyo kuzibwa na mafuta au kukakamaa.
sasa wagonjwa hawa mara nyingi hupewa dawa zinaizwa isosorbide mononitrate or dinatrate, dawa hizi hupanua mishipa ya damu na kuwafanya wapate nafuu huku dawa hizo zikishusha presha kama moja ya madhara yake, hivyo zikitumika na viagra ambayo kazi yake ni kushusha presha pia huweza kumuua mgonjwa.
wanawake; kuna watu hufikiri dawa za viagra zinaweza kuwasaidia wanawake kupata hamu ya tendo la ndoa, kitu hicho sio kweli na hakuna utafiti ulionyesha kitu kama hicho.
matumizi ya dawa hii kwa wanawake haina faida yeyote zaidi ya kushusha presha bure.
kuchanganya na baadhi ya dawa; dawa ya viagra ikishafanya kazi mwilini inaondolewa na maini kwa kutumia enzyme moja inayoitwa cytchrome p450, sasa baadhi ya dawa kama erythromycin, ritonavir na cimetidine hufanya kazi kwa kuzuia enzyme hiyo na kinachotokea ni kwamba viagra haitoki mwilini na inazidi kua nyingi kwenye mfumo wa damu,
Hivyo kua makini usitumie dawa hizi na pamoja na viagra.
MWISHO: viagra ni dawa hatari sana na inatakiwa itolewe kwa kibali maalumu cha daktari pale anaothibitisha kweli hakuna mazingira yeyote yanaweza kuhatarisha afya yako wa matumizi ya dawa hizo.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
Naomba nikwambie kwamba moja ya sababu ya kufia chumba cha wageni ni matumizi ya dawa hizi za viagra kiholela bila kujua kama afya yako inaruhusu matumizi ya dawa hii.
Leo ntaenda kuzungumzi makundi ya watu ambao hawaruhusiwi kutumia dawa hizi kama ifuatavyo.
wagonjwa wa moyo; wagonjwa wengi wa moyo hawaruhusiwi hata kushiriki tendo la ndoa kutokana na uwezo wao mdogo wa kuhimili mazoezi lakini pia dawa ya viagra inafanya kazi kwa kusukuma damu nyingi kwenda sehemu za siri na kupanua mishipa ya damu kitu ambacho hakiwezi kuvumilika kwa wagonjwa hawa.
Mshtuko wa moyo, kusimama kwa moyo na vifo vya ghafla vimeripotiwa sana sababu ya matumizi ya dawa hii ya viagra kwa wagonjwa wa moyo.
wagonjwa wa presha ya kushuka: dawa ya viagra ilitengenezwa mwanzoni kabisa kwa ajili ya kushusha presha ya kupanda lakini baadae ikaonekana kwamba madhara yake ni kuongeza nguvu za kiume hivyo ikabidi iondolewe kwenye dawa za presha.
Hivyo kama wewe presha yako ina tabia ya kushuka basi dawa hii inaweza kukushusha mpaka presha ya sifuri na huo ndio ukawa mwisho wako.
wanaotumia dawa za presha ya kupanda; hawa wagonjwa hutumia dawa za kushusha presha kila siku, sasa kama nilivyosema hapo juu.
viagra pia inatabia ya kushusha presha hivyo kama ukiamua kuimeza basi dawa zako za presha ni vizuri usizimeze kwani presha itashuka sana na kuhatarisha maisha yako.
wagonjwa wa macho; kama una tatizo lolote la macho ukatumia dawa hii ukaona giza ghafla basi achana nayo kwani hiyo ni kengere ya hatari na unatakiwa uwahi hospitali kuonana na daktari kwani ukiendelea kutumia itakumaliza macho kabisa.
wagonjwa wa siko seli; moja ya matatizo ya siko seli ni kuzuia damu kwenye uume na kushindwa kutoka kitaalamu kama priapism.
Tatizo hili ni kubwa na huweza kusababisha kufanyika kwa upasuaji, sasa mgonjwa wa siko seli akimeza dawa hii anaongeza hatari ya kushikwa na hali hiyo kwa maana nyingine dawa hii sio salama kwake, wagonjwa wa saratani ya damu pia wana hatari hii.
wagonjwa wa chembe ya moyo; huu ugonjwa kwa kitaalamu unaitwa angina pectoris, ni maumivu ya misuli ya moyo pale moyo unapokosa hewa ya kutosha sababu ya mishipa inayopeleka damu kwenye moyo kuzibwa na mafuta au kukakamaa.
sasa wagonjwa hawa mara nyingi hupewa dawa zinaizwa isosorbide mononitrate or dinatrate, dawa hizi hupanua mishipa ya damu na kuwafanya wapate nafuu huku dawa hizo zikishusha presha kama moja ya madhara yake, hivyo zikitumika na viagra ambayo kazi yake ni kushusha presha pia huweza kumuua mgonjwa.
wanawake; kuna watu hufikiri dawa za viagra zinaweza kuwasaidia wanawake kupata hamu ya tendo la ndoa, kitu hicho sio kweli na hakuna utafiti ulionyesha kitu kama hicho.
matumizi ya dawa hii kwa wanawake haina faida yeyote zaidi ya kushusha presha bure.
kuchanganya na baadhi ya dawa; dawa ya viagra ikishafanya kazi mwilini inaondolewa na maini kwa kutumia enzyme moja inayoitwa cytchrome p450, sasa baadhi ya dawa kama erythromycin, ritonavir na cimetidine hufanya kazi kwa kuzuia enzyme hiyo na kinachotokea ni kwamba viagra haitoki mwilini na inazidi kua nyingi kwenye mfumo wa damu,
Hivyo kua makini usitumie dawa hizi na pamoja na viagra.
MWISHO: viagra ni dawa hatari sana na inatakiwa itolewe kwa kibali maalumu cha daktari pale anaothibitisha kweli hakuna mazingira yeyote yanaweza kuhatarisha afya yako wa matumizi ya dawa hizo.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
0 maoni:
Chapisha Maoni