Katika hali ya kawaida binadamu akiwa hai anakua ni mwepesi kuliko maji hivyo hawezi kuzama chini ya maji akiwa bado anapumua, naomba hilo lieleweke vizuri.
Misuli ni mizito kidogo kuliko maji, mifupa ni mizito kidogo kuliko maji, mafuta ni mepesi kuliko maji lakini pia mapafu ya binadamu ya hewa ambayo yanamfanya binadamu awe kama boya la kuogelea.
binadamu akifa inakuwaje?
Sasa binadamu akifia kwenye maji, basi maji mengi yataingia kwenye mapafu na kuupoteza ule uwezo wa binadamu kuelea yaani atakua mzito kuliko maji na matakeo yake atazama chini ya maji kwa muda.
baada ya masaa kadhaa binadamu huyo ataanza kuharibika, wakati wakuharibika binadamu hutoa hewa nyingi ambayo hutokana na kazi ya bacteria wanaomshambulia.
Hewa ile itajaa sehemu mbalimbali za mwili wake na kumfanya avimbe, sasa hapo ndio atakua mwepesi tena kama boya, kama alivyokua mwanzo kabla ya kufa hivyo mwili utarudi juu na kuelea.
mwili unachukua masaa mangapi mpaka kuelea?
kutokana na hali ya hewa ya eneo husika, sehemu yenye joto mwili unaharibika haraka hivyo utaelea ndani ya masaa 24, lakini sehemu yenye baridi kali sana ambapo kuoza kunachelewa basi mwili unaweza kukaa chini hata wiki kadhaa bila kuelea.
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
STAY ALIVE.
Hongera ni Elimu nzuri imeeleweka.
JibuFutaNaomba nitoe challenge kidogo.
1. WAKATI BINADAMU AKIWA HAI kunaweza kukawepo EQUILIBRIUM Kati ya sehemu ya mwili yaani kutoka kiunoni kuelekea miguuni, pia kutoka kiunoni kuelekea sehemu ya kichwa hivyo uzito na urefu vinaweza vikawa katika hali ya EQUILIBRIUM kwa hiyo balance point ikapatikana hivyo mwili usizame kihurahisi ukalea.
2. BINADAMU AKIFA KWENYE MAJI HICHO KITENDO KINATANGULIWA NA KUNYWA MAJI.
Hivyo tumbo linajaa maji na kupelekea na kupelekea sehemu ya kuanzia kiunoni kuelekea kichwa inakuwa na uzito mkubwa Zaidi, hivyo kupelekea mwili kupoteza EQUILIBRIUM hivyo hakuna tena balance point ya mwili. Mwili utaanza kuzama kwa kuanzia sehemu ya kichwa moja kwa moja. 3. KWA NINI MWILI UTARUDI TENA WENYEWE KUELEA JUU YA MAJI BAADA YA KUZAMA KWENYE MAJI BAADA YA MUDA FULANI?. Jibu..... Baada ya muda MISULI YA KUWEKA MKAZO kwenye seheme za wazi za mwili kama sehemu ya haja ndogo na kubwa, na kupitia mdomoni ZINALEGEA AU KUSINYAA na kuruhusu maji na baadhi ya uchafu kutoka ndani ya mwili bila KIZUIZI itategemea hali ya joto au baridi kama alivyoelezea mtaalamu. Zile muscle zitalegezwa na bacteria kama alivyosema mtaalamu na kitendo hicho kitafanyika kwa mda mfupi Zaidi sehemu za joto. nyongeza yake ni kwamba baada ya mda seli za mwili za binadamu zitakuwa zimepasuka baada ya kujaa maji. Mwanzoni maji yaliingia kiuhurahisi kwa kuwa deli mwili zina hali ya chumvi kwa wingi kuliko maji, hivyo MAJI YANAFUATA KULE KWENYE CHUMVI NYINGI ila baada ya mda maji yakishaingia kwenye mwili inatokea dilution hali ya chumvi ya mwili na bahari vinakuwa sawa kabisa hivyo cell kupasuka. Maji yatakuwa yameenea sehemu nzima ya cell za mwili Hadi miguuni japo kwa maji ya upande wa kuanzia kiunoni kwenda miguuni utakuwa sio sawa na kuanzia kiunoni kwenda kichwani.Hali ya EQUILIBRIUM itarudi kwa sababu mwili utavimba na kuwa kama Boya....(buoyancy effect) hasa sehemu ya kuanzia tumboni japo kuna uzito mkubwa kidogo kuliko seheme kuanzia kiunoni kuelekea miguuni. Kuvimba kwa gumbo kutapelekea buoyancy effect na kuleta hali balance point Kati ya upande wa kuanzia kiunoni kuelekea kichwani na kulekea miguuni hivvyo mwili utarudi juu kuelea.
Uko vizuri Mkuu..nashukuru sana
Futa