data:post.body FAHAMU TATIZO LA KIZAZI KUGEUKA NA MATIBABU YAKE.(RETROVERTED UTERUS) ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

FAHAMU TATIZO LA KIZAZI KUGEUKA NA MATIBABU YAKE.(RETROVERTED UTERUS)

Kwa kawaida zaidi ya 80% ya wanawake wana vizazi ambavyo vimelalia upande mbele yaani kwenye ukuta wa tumbo lakini baadhi ya wanawake wachache vizazi vyao vimelalia nyuma yaani kwa upande wa mgongoni.               
                                                       

Kizazi kugeuka au kulalia mgongo hua sio tatizo kubwa sana wala haliwezi kuzuia mtu kupata mimba japokua linaweza kusababisha dalili mbalimbali kama maumivu wakati wa tendo la ndoa.

kitu gani kinafanya kizazi kinageuka?
hali ya kuzaliwa nayo; kuna wanawake ambao wamezaliwa hivyo wala hakuna tatizo lolote ambalo limetokea kuleta hali hiyo.
makovu(adhehesions); wakati mwingine mwanamke huhitaji upasuaji kutibu magonjwa mbalimbali  au kujifungua sasa baadhi ya wanawake hupata makovu baada ya upasuaji ambayo huweza kupelekea kizazi kukosa nafasi ya kukaa vizuri na kugeuka,
uvimbe wa kizazi; baadhi ya vimbe zinazotokea kwenye kizazi huweza kuingilia ukaaji halisi wa kizazi na kufanya kizazi kigeuke.
Vimbe kama hizo zinaweza kua za saratani au ambazo sio za saratani, mfano fibroids.
endometriosis; huu ni ugonjwa unaosababishwa na seli za ndani ya ukuta wa kizazi kuota sehemu zingine ambazo seli hizo hazikutakiwa kuwepo, seli hizo huwezi kubana kizazi kama gundi na  kukigeuza.
uzazi; kwa kawaida kizazi kinashikwa kwenye sehemu yake na kamba maalumu kitaalamu kama ligament, mwanamke akibeba ujauzito ligament zile zinavutika sana na kushindwa kushika kizazi vizuri.
sasa baada ya kujifungua kizazi kinaweza kurudi kwenye hali yake ya zamani au kisirudi tena na kubaki kimegeuka.

dalili za kizazi kugeuka.
mara nyingi mwanamke hapati dalili yeyote hasa kama amezaliwa hivyo lakini maumivu huweza kutokea wakati wa tendo la ndoa hasa mwanamke akikaa kwa juu wakati wa tendo la ndoa lakini pia mwanamke anaweza kupata maumivu ya tumbo na dalili zingine  kutokana na chanzo husika cha ugonjwa kama nilivyotaja hapo juu.

mahusiano ya ugumba na kizazi kugeuka
kwa kawaida kama mwanake amezaliwa na kizazi kilichogeuka basi hawezi kupata shida ya uzazi lakini kama kizazi kiligeuzwa na matatizo mengine ya uzazi basi kizazi kinaweza kuleta shida ya uzazi japo sio kwa watu wote.

jinsi ya kugundua kama kizazi kimegeuka.
mara nyingi madaktari huweza kugundua kizazi kimegeuka wakati wa uchunguzi wa kawaida au wakati wa vipimo vya picha kitaalamu kama utrasound.

matibabu ya kizazi kilichogeuka;
kuna matibabu aina mbaimbali kama mazoezi, vidonge maalumu kwenye kizazi, na kujaribu kutibu chanzo cha ugonjwa lakini yote hua hayatoi suluhisho la moja kwa moja.
suluhisho la moja kwa moja ni upasuaji tu, ambao huweza kurekebisha kizazi na kukiweka sawa.

                                                                    STAY ALIVE

                                             DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                        0769846183/0653095635

0 maoni:

Chapisha Maoni