data:post.body UFAHAMU UGONJWA WA DENGU, CHANZO CHA KIFO NA MATIBABU YAKE. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

UFAHAMU UGONJWA WA DENGU, CHANZO CHA KIFO NA MATIBABU YAKE.

Kuvuja damu kwenye pua na fidhi za mdomoni mpaka kufa ndio chanzo kikuu cha kifo cha ugonjwa huu.
Shirika la afya duniani WHO linakadiria kwamba kila mwaka watu milion mia tatu na tisini huuugua ugonjwa wa dengu kwa kujua na wengine kutokujua.
                                                         
Ugonjwa huu hupatikana sana maeneo yenye joto hasa afrika na asia sababu maeneo yanaweza kutunza mbu wengi tofauti na maeneo yenye baridi kali ambapo mbu hakuna.
Ugonjwa wa dengu unaweza kua hatari mpaka kusababisha kifo hasa kwa watoto wadogo na wazee ambao kinga zo hua ziko chini.
Inakadiriwa kua katika kila wagonjwa 100 wa dengue basi wawili mpaka watatu hufariki wa ugonjwa huu.

chanzo cha ugonjwa ni nini?
Virusi vya dengu ndio chanzo kikuu cha ugonjwa huu, kuna aina nyingi za virusi hawa kama DEN-1, DEN-2,DEN-3 na DEn-4.
Virusi hawa husambazwa na mbu wa kike kwa jina la Aedes aegypti, Mbu hawa pia husambaza magonjwa mengine kama chikungunya, homa ya manjano na ugonjwa wa zika.

dalili za ugonjwa wa dengue.

  • maumivu ya ghafla ya kichwa.
  • homa kali ya ghafla.
  • maumivu ndani ya macho
  • maumivu makali ya jointi na mifupa
  • kuchoka sana
  • kutapika
  • vipele vya ngozi.
  • kutoka damu puani na kwenye fidhi.
vipimo vya maabara
kipimo maalumu kitaalamu kama antibody test hufanyika kugundua ugonjwa huu.


matibabu ya ugonjwa wa dengu.
hakuna matibabu ya ugonjwa huu ila kuna jinsi ya kutuliza makali ya ugonjwa huu.
ikithibitika una ugonjwa wa dengue unatakiwa unywe maji mengi na kutumia dawa ya paracetamol tu.
epuka dawa zote za jamii ya aspirini kama diclofenac, diclopa, meloxicam, peroxicam, ibuprofen na kadhalika kwani zinaongeza uvujajaji wa damu.

jinsi ya kuzuia ugonjwa huu.
Njia bora ya kuzuia ugonjwa huu ni kuepuka kung'atwa na mbu ambao wanasababisha ugonjwa dengu kama ifuatavyo.

  • usiishi sehemu zenye msongamano mkubwa wa watu.
  • tumia dawa za mbu za kupaka kwenye ngozi au kupuliza.
  • vaa ngo ndefu na za kufunika miguu na mikono.
  • funga madirisha na milango jioni kuzuia mbu wasiingie.
  • ukipata dalili za ugonjwa huo nenda hospitali.


                                                   STAY ALIVE 

                       DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                     0769846183/0653095635

0 maoni:

Chapisha Maoni