data:post.body HIZI NDIO FAIDA 5 ZA KUNYWA SODA AMBAZO HAZINA SUKARI ASILIA.(SUGAR FREE DRINKS) ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIZI NDIO FAIDA 5 ZA KUNYWA SODA AMBAZO HAZINA SUKARI ASILIA.(SUGAR FREE DRINKS)

Soda ambazo hazina sukari asilia ziligunduliwa mwaka 1960 kwa ajili ya kuwapa watu wenye kisukari kwasababu zilikua zimetengenezwa na sukari feki kitaalamu kama artificial sweetener ambayo ukinywa mdomoni inaonekana ni tamu kabisa kama soda lakini, ikifika tumboni ni kama maji tu yaani haiwezi kukupa nguvu wala kuongeza kiasi cha sukari mwilini mwako.


miaka michache baadae soda hizi zilianza kutangazwa zitumike kwa ajili ya watu wote baada ya faida zake kuanza kuonekana ndio maaana siku hizi unazioana nyingi sana mtaani ili kila mtu aweze kutumia kama mbadala wa soda za zenye sukari asilia.
faida zake ni kama ifuatavyo.
husaidia kupunguza uzito; soda za kawaida zina vijiko kumi vya sukari kwa kila moja, kipimo ambacho ni kikubwa sana kwa matumizi ya binadamu na huongeza uzito kwa kiasi kikubwa.
Kawaida mwanaume hatakiwi kutumia zaidi ya vijiko tisa vya sukari kwa siku nzima yaani kwanzia chai na chakula utakachokula mchana huki mwanamke akitakiwa vijiko sita tu.
Hivyo ukinywa soda moja tu ushapita kiwango na hapo hujaongezea biskuti, ndizi mbivu,keki,chocolate, sukari ya chai na vyakula vingine vya jamii ya sukari.
Hivyo wakati soda ya kawaida pekee inakupa calories 150 kwa siku ambayo ni sawa na kilo mbili za unene kila mwezi, soda ambazo hazina sukari asilia hazikuongezi calorie yeyote wala uzito wowote mwilini.
nzuri kwa afya ya meno; sukari za kwenye soda za kawaida hutengeneza tindikali mdomoni ambazo hubandua na kutoboa meno kwa watumiaji, ndio maana wagonjwa wote wa meno hawashauriwi sana kula vyakula vya sukari nyingi.
lakini soda hizi sababu sukari yake sio asilia basi hazina uwezo wa kukuunguza au kukutoboa meno.
nzuri kwa wagonjwa wa kisukari;mgonjwa wa kisukari anaweza kunywa soda hizi bila wasiwasi kama watu wengine na bila kuhofia uwezekano wowote wa sukari yake kupanda, ukilinganisha na soda za zamani ambazo zilikua zina sukari asilia ambazo zilikua zinapandisha sukari kwa kiasi kikubwa sana.
nzuri kwa vyakula vingine pia; siku hizi jamii ya sukari hii inapatikana madukani hivyo ili kupunguza matumizi makubwa sana ya sukari ambayo ni hatari kwa afya yako basi unaweza kuitumia kwenye chai na vyakula vyote ambavyo huhitaji sukari kwenye mapishi kama keki, maandazi na kadhalika.
hupunguza hatari ya saratani mbalimbali; kutokana na kiwango kikubwa sana cha sukari kwenye soda za kawaida, soda hizo zimehusishwa sana na kuugua ugonjwa wa saratani ya kongosho.
Ukilinganishwa na soda hizi mpya ambazo hazina sukari asilia ambazo tafiti zake zomeonyesha kwamba hakuna hatari yeyote ya saratani kwenye soda hizo.

                                                                          STAY ALIVE
                                                 DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

                                                             0653095635/0769846183

0 maoni:

Chapisha Maoni