data:post.body HIZI NDIO NJIA TATU ZA KUZAA NA MUATHIRIKA WA UKIMWI BILA KUPATA MAAMBUKIZI. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIZI NDIO NJIA TATU ZA KUZAA NA MUATHIRIKA WA UKIMWI BILA KUPATA MAAMBUKIZI.

Katika hali ambayo sio ya kawaida, watu wawili wanaweza wakakutana na kupendana huku mmoja wao ni muathirika wa ukimwi na mwingine asiwe muathirika wa ukimwi.
Hali hii inaweza kuleta ugumu kidogo kwenye mitazamo ya watu wa nje kama ndugu, jamaa na marafiki.                                                             
Lakini linapokuja swala la mapenzi hua ni vigumu sana kulizuia, kwani kuna ushahidi wa watu waliofunga ndoa na waathirika bila kujali afya zao sababu ya mapenzi.
sasa kumekua na utata ni jinsi gani unaweza kuzaa na mtu ambaye ni muathirika kwani watu wengi ambao wana wapenzi waathirika wanatakiwa watumie kondom kujilinda na maambukizi.
Leo ntatoa njia tatu muhimu ambazo unaweza kutumia kulala na mwanamke muathirika bila kondom na ukawa salama.
mgonjwa kutumia dawa zake vizuri;  mgonjwa akitumia dawa zake vizuri kiasi kwamba majibu ya damu kitaalamu kama viral load yakafika hatua amabayo virusi havionekani kwenye vipimo vya damu{ sio vile vinavyotumika nyumbani kujipima} au undetectable basi mchumba wake ambaye sio muathirika anaweza kulala na muathirika huyo bila kutumia kondom na kumpa mimba.
tafiti zinaonyesha kwamba kulala na mtu kama huyu ni sawa na kulala mtu kwa kutumia kondom kwani hawezi kukuambukiza kabisa.

kupandikiza mbegu za kiume; hii ni njia ya kisasa ambayo hutumika kuchukua mbegu za mwanaume na kuzipandikiza kwa mwanamke bila kukutana naye kingono, hii inaweza kutumika mwanamke akiwa muathirika au mwanaume akiwa muathirika kama ifuatavyo.
kama mwanamke ni muathirika basi mbegu za mwanaume zinachukuliwa na kupandikizwa na kumbebesha mimba, kama ni mwanaume muathirika mbegu za zake zinachukuliwa na kusafishwa kitaalamu kabla ya kupandikizwa kupata ujauzito.
                                       
kutumia dawa za kujizuia na ukimwi: kuna dawa maarufu ambazo zinatumika sana siku hizi kwa ajili ya kuwapa watu ambao wamelala na waaathirika bahati mbaya ili kuzuia ukimwi, dawa zile ni maarufu kama PEP.
Zinaweza kutumika pia kama chanjo mtu ambaye anataka kuzaa na muathirika, yaani siku mwanaume au mwanamke ambaye sio muathirika anachukua dozi ya mwezi mmoja na kuanza kumeza huku akikutana na mtu wake ambaye ni muathirika bila kutumia kondomu, akishafanikisha kumpa mimba basi anaendelea kutumia kondom na kuacha dawa.
                                                             
mwisho; kama mama ndio muathirika basi jitihada za msingi za kuhakikisha mimba hiyo inakua chini ya uangalizi wa kliniki ya mama na mtoto inatkiwa zifanyike ili kuhakikisha mtoto mtarajiwa anazaliwa bila maambukizi ya virusi vya ukimwi.

  • Kupata makala zetu mara kwa mara ingia playstore kisha pakua au download application ya "siri za afya bora".

0 maoni:

Chapisha Maoni