chunusi ni nini?
hivi ni vipele vinavyotokea usoni, kifuani na mgongoni sababu ya kubadilika kwa mfumo wa kutengeneza mafuta wa ngozi, hali hii husababishwa na kutengenezwa kwa mafuta mengi chini ya ngozi kuliko kawaida na kuziba kwa vinyweleo vya ngozi.
imekua ni jadi kwa watu wengi kupenda kuzitumbua chunusi pale ambapo zinakua zimekua kubwa na wakati mwingine hata zikiwa ndogo.
lakini kimsingi kuna madhara makubwa sana ya tabia hii kwenye ngozi yako na afya ya mwili wako wote kiujumla kwa ujumla kama ifuatavyo.
kuacha makovu meusi; kwa kawaida chunusi ikipona yenyewe hua haichi alama yeyote lakini ukianza kuikamua na kuisugua basi unatengeneza kidonda kidogo ambacho baadae kitapona kwa kaucha kovu.
makovu ya usoni yanaleta muonekano mbaya sana kwani usoni ni sehemu ambayo inaonekana sana kukiko sehemu zote za mwili.
uwezekano wa kuondoa makovu haya ni mgumu na hata ukiwezekana ni kwa kutumia dawa za gharama kubwa na wengine huamua kujichubua kabisa.
maumivu makali; chunusi huambatana na maumivu makali ikianza kutumbuliwa na chunusi ambazo zinakua mbele kidogo ya masikio husababisha maumivu makali ya kichwa zikitumbuliwa.
hii inaweza kumfanya mtu akawa mgonjwa sana na kushindwa kuendelea na shughuli zake.
homa ya uti wa mgongo; japokua hii hutokea mara chache sana lakini ni hatari na inaweza kumuua mtu, usoni kuna mishipa ya damu ambayo huko ndani huungana na mishipa mingine ya damu na kufika kwenye ubongo.
sasa ukitumbua chunusi bakteria wanaweza kusambaa na kupita kwenye damu mpaka kwenye ubongo.
ugonjwa huu ni hatari na huua watu sana.
kuharibu muonekano hapo hapo; kwa kawaida chunusi ambayo haionekani vizuri huvimba zaidi ukijaribu kuitumbua, hii itakufanya uonekane una chunusi nyingi kuliko kawaida na kukunyima kujiamini mbele za watu.
mwisho: kutumbua chunusi sio njia bora ya kupambana nazo kama tulivyoona hapo juu, hivyo kama unataka kujua matibabu mazuri ya chunusi soma hapa http://www.sirizaafyabora.info/2014/08/ufahamu-ugonjwa-wa-chunusi-na-matibabu.html
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
hivi ni vipele vinavyotokea usoni, kifuani na mgongoni sababu ya kubadilika kwa mfumo wa kutengeneza mafuta wa ngozi, hali hii husababishwa na kutengenezwa kwa mafuta mengi chini ya ngozi kuliko kawaida na kuziba kwa vinyweleo vya ngozi.
imekua ni jadi kwa watu wengi kupenda kuzitumbua chunusi pale ambapo zinakua zimekua kubwa na wakati mwingine hata zikiwa ndogo.
lakini kimsingi kuna madhara makubwa sana ya tabia hii kwenye ngozi yako na afya ya mwili wako wote kiujumla kwa ujumla kama ifuatavyo.
kuacha makovu meusi; kwa kawaida chunusi ikipona yenyewe hua haichi alama yeyote lakini ukianza kuikamua na kuisugua basi unatengeneza kidonda kidogo ambacho baadae kitapona kwa kaucha kovu.
makovu ya usoni yanaleta muonekano mbaya sana kwani usoni ni sehemu ambayo inaonekana sana kukiko sehemu zote za mwili.
uwezekano wa kuondoa makovu haya ni mgumu na hata ukiwezekana ni kwa kutumia dawa za gharama kubwa na wengine huamua kujichubua kabisa.
maumivu makali; chunusi huambatana na maumivu makali ikianza kutumbuliwa na chunusi ambazo zinakua mbele kidogo ya masikio husababisha maumivu makali ya kichwa zikitumbuliwa.
hii inaweza kumfanya mtu akawa mgonjwa sana na kushindwa kuendelea na shughuli zake.
homa ya uti wa mgongo; japokua hii hutokea mara chache sana lakini ni hatari na inaweza kumuua mtu, usoni kuna mishipa ya damu ambayo huko ndani huungana na mishipa mingine ya damu na kufika kwenye ubongo.
sasa ukitumbua chunusi bakteria wanaweza kusambaa na kupita kwenye damu mpaka kwenye ubongo.
ugonjwa huu ni hatari na huua watu sana.
kuharibu muonekano hapo hapo; kwa kawaida chunusi ambayo haionekani vizuri huvimba zaidi ukijaribu kuitumbua, hii itakufanya uonekane una chunusi nyingi kuliko kawaida na kukunyima kujiamini mbele za watu.
mwisho: kutumbua chunusi sio njia bora ya kupambana nazo kama tulivyoona hapo juu, hivyo kama unataka kujua matibabu mazuri ya chunusi soma hapa http://www.sirizaafyabora.info/2014/08/ufahamu-ugonjwa-wa-chunusi-na-matibabu.html
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
0 maoni:
Chapisha Maoni