data:post.body UFAHAMU UGONJWA WA MACHO MEKUNDU NA MATIBABU YAKE.(CONJUCTIVITIS) ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

UFAHAMU UGONJWA WA MACHO MEKUNDU NA MATIBABU YAKE.(CONJUCTIVITIS)

Conjuctivitis ni nini?
huu ni ugonjwa unaohusiana na kushambuliwa kwa sehemu ya mbele ya jicho kitaaalamu kama conjuctiva.
Huu ni moja ya magonjwa ambayo yanaongoza kusababisha macho mekundu kwa wagonjwa wengi.

nini chanzo cha ugonjwa huu?

  • bacteria
  • virusi
  • aleji mbalimbali.
ugonjwa unaweza kuambukizwa?
kama ugonjwa umesababishwa na aleji sio rahisi kuambukizwa lakini kama nia bacteria au virusi basi ugonjwa unaweza kusambaa kwa kasi sana hasa maeneo ya shule.
mara nyingi ugonjwa huanza na jicho moja lakini huambukia jicho lingine pale mtu anapofikicha macho yote na kuhamisha wadudu jicho moja kwenda lingine.
lakini pia unaweza kuambukizwa kwa kuchangia taulo, miwani au nguo ambazo zinafika machoni.

dalili za ugonjwa ni zipi?
wakati mwingine dalili za ugonjwa huweza kutegemea chanzo cha ugonjwa wenyewe kama ni bacteria, virusi au aleji lakini kuna dalili za ujumla kama zifuatazo.
  • usaha kutoka machoni
  • macho kuvimba
  • kutoka majimaji usoni
  • kusikia kama mchanga machoni.
  • macho kuwasha kama ni aleji.

matibabu ni yapi?
  • dawa ya kuweka machoni kwa jina la chlorampenicol itumike kutwa mara tatu kwa muda wa siku tano.
  • kama kuna dalili za aleji basi kuna dawa inaitwa sodium cromoglyacate ambayo mara nyingi hutumika kutwa mara mbili au mara tatu.
jinsi ya kuzuia ugonjwa huu
  • epuka kuchangia taulo au miwani na mgonjwa.
  • nawa uso  na kuosha mikono na sabuni mara kwa mara.
  • kaa mbali na vitu vinavyokupa aleji.
                                                             STAY ALIVE

                                      DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                0769846183/0653095635

0 maoni:

Chapisha Maoni