data:post.body UFAHAMU UGONJWA WA JIPU LA MACHO NA MATIBABU YAKE.(STYE) ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

UFAHAMU UGONJWA WA JIPU LA MACHO NA MATIBABU YAKE.(STYE)

STYE ni nini?
huu ni ugonjwa wa macho ambao huwapata watu wengi sana katika kipindi cha maisha yao yaani angalau mara moja au mara mbili.
huu ni uvimbe wa jipu ambao hutokea kwenye sehemu ya jicho na kuleta maumivu makali.
                                               

chanzo cha ugonjwa huu ni nini?
ugonjwa huu husababishwa na bacteria ambao hushambulia sehemu ya macho inayohusika na kutengeneza majimaji ya kulainisha macho kitaalamu kama gland of zeis.
pamoja na bacteria kusababisha hali hii ukosefu wa maji ya kutumia, kutokula mlo kamili, kusugua macho na mikono, kushuka kwa kinga ya mwili na kukosa usingizi wa kutosha huongeza uwezekano wa kuugua ugonjwa huu.
ugonjwa huu sio hatari lakini una usumbufu mkubwa ambao unaweza kufanya kushindwa kufanya shughuli zako kwa amani.


dalili za ugonjwa huu ni zipi?

  • uvimbe sehemu ya juu au chini ya jicho.
  • maumivu makali sana ya jicho hasa ukiinama,
  • jicho kua jekundu
  • kushindwa kuangalia mwanga wa jua.
  • kutokwa na machozi
  • kuhisi kama mchanga jichoni.
matibabu ya asili;
mara nyingi ugonjwa huu hupona wenyewe bila matibabu yeyote ndani ya siku 7 mpaka 14, lakini kama unataka kupona haraka basi chukua maji ya moto kisha kanda kila siku mara moja sehemu ambayo ina uvimbe na jipu linaweza kupotea bila hata kuiva.
watu wenye ugonjwa huu hawashauriwi kupaka  urembo wowote make up, mafuta ya losheni usoni au kuweka urembo wowote machoni.

matibabu ya kisasa
meza dawa za antibayotiki kama amoxicillin kutwa mara tatu ndani ya siku tano mpaka saba lakini pia unaweza ukatumia dawa za matone.
lakini pia meza panadol au diklopa kutwa mara tatu kupunguza maumivu ya jicho.
kwa matibabu haya ugonjwa unaweza ukaisha wenyewe na kama usipoisha basi inabidi uende hospitali ukapasuliwe ili kuondoa usaha wote.
matibabu ya upasuaji yanapedekezwa kwa jipu lililoiva au kwa mgonjwa ambaye ugonjwa unamrudia mara kwa mara.

jinsi ya kuzuia 
  • usichangie vifaa vya kuoga kama taulo.
  • usichangie vifaa vya kupaka urembo kama make up.
  • nawa mikono na oga kila siku.
  • hakikisha umenawa urembo wote wa macho kabla ya kulala.
  • kula mlo kamili kuweka kinga yako vizuri.

                                                                STAY ALIVE
                                     DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO  
                                                    0769846183/0653095635

0 maoni:

Chapisha Maoni