Japokua wanaume wengi ndio wanaonekana sana kusaliti ndoa zao au mahusiano yao kuliko wanawake siku hizi wanawake pia wanasaliti ndoa zao au mahusiano yao pia.
Tangu mwaka 1990 tafiti zinaonyesha kwamba idadi ya wanawake wanaosaliti mahusiano yao umeongezeka kwa asilimia arobaini lakini idadi ya wanaume wanaosaliti ndoa zao imebaki ileile, kitu ambacho kinazua maswali mengi.
wanawake wa siku hizi wana mtazamo sawa na wanaume linapokuja swala la ngono, na huweza kuchepuka mara moja au mbili kwa mwezi au mara moja kila mwezi.
kuna aina ya wanawake ambao hawawezi kua na mwanaume mmoja kwani hawawezi kupata kila wanachotaka maishani kwa kua na mwanaume mmoja tu.
lakini pia baadhi ya wanawake kusaliti mahusiano yao ni sehemu ya maisha yao, yaani wakivutiwa sehemu hawawezi kujidhibiti hisia zao hivyo huamua kulala na hao watu tu ili kupata mambo mapya.
lakini kwa ujumla mara nyingi sana wanawake huenda nje ya ndoa kama kuna vitu fulani vimeanza kukosekana ndani ya ndoa au mahusiano tofauti na wanaume ambao kiukweli huwezi kuwazuia hata kama kila kitu kipo. zifuatazo ni sababu kuu...
kukosa mawasiliano; hata kama unaishi na mwanamke nyumba moja, mawasililiano ni muhimu sana baina yenu, ni vizuri kujua nini kinaendelea kwenye maisha yake kwani anaweza kua ana dukuduku na wewe hutaki kusikiliza lakini pia mahusiano ya mbali kwa kiasi kikubwa yakiwa na mawasiliano yanamfanya mwanamke ahisi kama yuko na mwanaume sehemu moja, lakini mawasiliano yakiwa mabovu yaani kupitisha siku bila kuongea kabisa inamvuta mwanamke kutamani mahusiano mengine.
kisasi; wanawake ni watu wa visasi sana hasa wakitendwa vibaya, au ukiwasaliti wakajua. wanaweza kujifanya wamekubaliana na hali baada ya kuombwa msamaha lakini wakaliweka moyoni na siku moja watakulipa tu.
na sio kwamba atalipiza kisasi kwa kua wewe umelala na mwanamke mwingine tu ila anaweza kulipiza sababu hukumjali, hukukumbuka siku yake ya kuzaliwa, hukukumbuka siku ya wapendanao au siku yake yeyote muhimu.
kutoridhika na tendo la ndoa; wanaume wengi hudhani kwamba wanawake hua hawajisikii kufanya tendo la ndoa mara nyingi kitu ambacho sio kweli.
wanawake pia wana hamu sana ya tendo la ndoa kama wanaume lakini tofauti na sisi wanaume, wao hawajali sana umelala naye mara ngapi kwa siku au umepiga mishindo mingapi ulipokua kitandani.
wanawake wanajali ubora wa tendo la ndoa.
mwanamke anaweza akalala na mume wake mara tatu au nne kwa wiki na akaridhika lakini mwnamke anayelala na mwanume wake kila siku na mishindo minne kila siku asiridhike na akaenda nje.
kimsingi kama unaona unashindwa kumridhisha mwanamke wako kabla ya ndoa ni vizuri ukabadilisha mawazo ukatafuta ambaye unamuweza kwani bila hivyo utasaidiwa sana.
mwanaume kua na wivu sana; kuna wanaume wanawaendesha sana wanawake zao, yaani atapiga simu kila mara na kutaka kuongea na rafiki zake ili kuhakikisha mwanamke wake yupo salama.
lakini hii sio njia nzuri, kisaikolojia binadamu ukimbana sana ndio unamtengenezea mazingira ya kutoroka.
mwanamke huyu atakusaliti ili kukuonyesha kwamba pamoja na mitego yako yote wewe humuwezi, hivyo muache mwanamke huru kama sio msaliti wala hawezi kukusaliti.
kutojiamini; wanawake wanapenda kuambiwa kwamba ni wazuri na wamependeza, sasa ikitokea unakaa na mwenza wako miezi kadhaa bila kumsifia afu akaanza kusifiwa na watu wengine basi anaweza kuamua kulala na huyo anayemsifia kwani ndio mtu anayemfanya ajisikie vizuri.
lakini pia umri ukishamtupa mkono mwanamke halafu akawa kwenye mahusiano ambayo anahisi ndoa inachelewa sana anaweza kuanza kwenda nje kubahatisha mtu ambaye anaweza akamuoa.
ugumu wa maisha; wazungu wanasema kwamba 'everyone has a price' yaani kila mtu ana bei yake ambayo anaweza kununulika.
sasa katika kipindi fulani kigumu sana cha maisha mtu anaweza akatokea akamwambia mpenzi wako au mke wako kwamba nataka kulala na wewe kisha ntakupa fedha kiasi fulani.
sasa akiwa amekabwa sana na shida anaweza kuwaza, kwani kulala mara moja na huyu mtu kutabadilisha nini?
na hapo ndipo usaliti unapoanza.
mfano ni wanawake wachache sana wanaweza kukataa milion moja mpaka kumi kwa tendo la saa moja tu.
kutegemea makubwa kwenye mahusiano; mwanamke anaweza kuingia kwenye mahusiano akiwa na mategemeo makubwa sana ya kimapenzi au ya kiuchumi lakini baadae akagundua kwamba hivyo vitu haviwezekani.
lakini pia hakuna mwanaume ambaye anaweza kuonyesha mapenzi yaleyale kwa miaka yote, kuna kipindi mapenzi lazima yapungue kidogo japokua hayataisha kabisa.
hiii inatoa nafasi ya mwanamke kwenda nje ya ndoa kujaribu kuyapata yale aliyoyategemea.
kukosa vitu vidogo vidogo kwenye mahusiano; unaweza ukamfanyia vitu vikubwa sana mwanamke lakini akakusaliti sababu kuna viti vidogo vidogo sana havipati ambavyo anahisi kwamba haumpendi ndio maana hauvifanyi.
unaweza kumnunulia gari ila siku moja akapata pancha akakupigia ukashindwa kwenda kwa wakati sababu ya kazi zimekubana.
akitokea mwanaume mpya akamsaidia kubadilisha tairi ataonekana muhimu sana kuliko wewe uliyenunua gari.,
presha ya marafiki; mara nyingi tabia huwavuta watu pamoja na kua marafiki, ukiona mwanamke wako ana marafiki ambao wana tabia za undangaji au ni watu wa kutafuta mabwana usifikiri wamekutana na mke wako bahati mbaya, kuna uwezekano mkubwa mke wako pia ni mwenzao.
hata kama mke wako hafanyi hivyo basi ipo siku moja atawafuata.
kuchoshwa na mahusiano; tukiacha unafiki, ndoa za zamani zilidumu sababu ya misingi ya uvumilivu na kumuogopa mungu lakini mioyo ya binadamu ilikua radhi kwenda nje.
sasa kwa dunia hii ya sasa ambayo hofu ya mungu haipo wala uvumilivu hakuna ni rahisi sana mtu aliyemchoka mwenza wake kwenda nje kutafuta ladha nyingine.
mwisho; hakuna mtu anayeweza kusiamama na kudai yeye amemdhibiti mwanamke wake, pamoja kwamba unaweza kufanya yote lakini mwisho wa siku maamuzi hubaki mikononi mwake.
wanawake ambao wanamjua mungu sana hawaendi nje sababu ya kuogopa dhambi sio kwamba mioyo yao imeridhika na wewe.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183