data:post.body 2019 ~ SIRI ZA AFYA BORA...
  • Karibu kwenye blog ya SIRI ZA AFYA BORA ujifunze mbinu bora za afya ili uweze kuwa na afya bora.

Recent Posts

KUOSHA SEHEMU ZA SIRI BAADA YA TENDO LA NDOA HUONGEZA MAAMBUKIZI YA UKIMWI.(TAFITI)

Kwa miaka mingi imekua ikifahamika kwamba kuosha sehemu za siri baada ya tendo la ndoa kuna zuia magonjwa ya zinaa kama kaswende, pangusa na mengine ambayo huambukizwa kwa tendo la ndoa, hii imekua ni kweli kwasababu magonjwa ya aina hiyo huhitaji muda wa kutosha kuweza kuanzisha makoloni yao sehemu za siri ili kuleta ugonjwa.
hivyo maji maji yenye ugonjwa huo yakishaoshwa yanasimamisha mfumo mzima wa kuanzisha ugonjwa husika.


Lakini hii imeonekana ni tofauti linapokuja swala la virusi vya  ukimwi kwani kuosha sehemu za siri hasa kwa wanawake na wanaume ambao hawajatahiriwa kumeonekana kuongeza maambukizi badala ya kupunguza.
Utafiti huu ulifanyika nchini Uganda ulichukua wanaume ambao hawajatahiriwa ambao wanatabia hiyo kisha kuchukua wanaume ambao hawana tabia hiyo na kuwafuatilia kwa muda Fulani( cohort studies) na majibu yakionyesha kuongezeka kwa maambukizi kwa 2.3% kwa wale wenye tabia ya kuosha uume wao muda mfupi tu baada ya tendo la ndoa.
Lakini utafiti mwingine ulifanyika nchini kenya kwa muda wa miaka kumi kwa wanawake 1270 na majibu yalionyesha kuongezeka kwa maambukizi ya ukimwi kwa asilimia 2.6% kwa wale walio osha sehemu zao za siri pale pale ukilinganisha na wale waliochelewa na kuosha baada ya dakika kumi mpaka 20.

je chanzo cha maambukizi haya ni nini?
Hakuna majibu ya uhakika wa swali hili lakini wataalamu wamekuja na ababu ambazo huenda ndio zinachangia kutokea kwa jambo hili kama ifuatavyo.
kuongeza ukali wa virusi; sehemu za siri za mwanamke zina maji maji ambayo yana tindikali ambayo kazi yake ni kuua wadudu ambao wanaingia ndani ya uke, sasa ukimwaga maji pale ile tidikali inaishiwa nguvu na kuwapa virusi wale nguvu.
kuongeza michubuko; baadhi ya watu huosha na sabuni au dawa mbalimbali,yale maumivu kidogo unayosikai baada ya kumwaga maji au kupaka sabuni ni kuongezeka kwa michubuko ambayo inatoa nafasi zaidi kwa virusi vya ukimwi kufanya mashambulizi.
kuvipa virusi uwezo wa kuishi na kusafiri; kwa kawaida virusi huishiwa nguvu au kufa pale maji maji yanayovizunguka yanapokauka, kuosha na maji na kuongeza maji maji na kuvihamisha sehemu zingine za sehemu za siri ambazo huenda zina michubuko Zaidi.
mwisho;Kwa lugha nyingine sio vizuri kuosha sehemu za siri muda mfupi tu baada ya tendo la ndoa, jipe muda wa kutosha kitandani na mtu wako kama dakika 10 au 20 ukiwa umepumzika au unafanya mambo mengine kisha unaweza kwenda kunawa.


                                                                        STAY ALIVE

                                                  DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                                 0653095635/0769846183

UFAHAMU UPASUAJI WA KUKATA UTUMBO KUPUNGUA UZITO.(GASTRIC BYPASS SURGERY)

Msanii mmoja wa maigizo kwa jina la Wema Sepetu inasemekana alifanya upasuaji wa kuondoa utumbo lakini yeye mwenyewe hajakubali wala hakuna ushahidi wa hilo.
Hivyo watu wengi wamekua wakijiuliza maswali mengi kwamba upasuaji huo unafanyika vipi, wapi na gharama za upasuaji huo zikoje.

Gastric by pass surgery ni nini?
Huu ni upasuaji wa ambao unabadilisha jinsi tumbo lako unavyopokea chakula na kukitumia, baada ya upasuaji tumbo lako litakua dogo na ukila chakula kidogo tu limejaa.
Baada ya upasuaji huu tumbo lako litakua linapokea chakula kidogo sana na baadhi ya sehemu za utumbo wako zitakua hazifikiwi na chakula hivyo ni chakula kidogo sana kitakua kinachukuliwa na mwili, hii itamfanya mtu apungue uzito mwingi sana.

upasuaji huu hufanyika kwa watu wa aina gani?
upasuaji huu hufanyika kwa watu ambao ni wanene sana na wameshindwa kujipunguza kwa njia za asili yaani mazoezi na diet.

upasuaji huu unafanyika vipi?
Hatua ya kwanza daktari atagawanya tumbo lako katika sehemu kuu mbili, sehemu ya chini kubwa na sehemu ya juu ndogo kisha atabakiza sehehemu ndogo ya juu. kawaida tumbo la binadamu lina uwezo wa kuchukua lita moja na nusu ya chakula lakini kwa sasa utakua na uwezo wa kuchukua kama theluthi tu ya lita moja.
Hatua ya pili daktari ataukata utumbo mdogo wa juu kitaalamu kama duedonum kisha atachukua utumbo wa katikati kwa jina juejonum na kuunganisha na tumbo lako dogo jipya hivyo utakua ukila chakula kinaingia kwenye tumbo dogo na kupitiliza moja kwa moja kwenye utumbo wa katikati.

upasuaji huu unafanyika wapi?
sina uhakika sana kama upasuaji huu unafanyika hapa nchini lakini nina uhakika madaktari wetu wanaweza kufanya kazi hii, gharama kwa nchi kama marekani ni shilingi milion 30 lakini kwa hapa kwetu inaweza kua chini ya hapo.

mwisho; kama ilivyo kwa aina zingine za upasuaji, uparesheni hii inaweza kua na madhara kama kuvuja damu nyingi, kupata henia, kupata makovu tumboni, kuziba kwa utumbo hata kifo japokua utafiti unaonyesha madhara yake wanapata watu chini ya 1% na vifo vikiwa 0.5%.

                                                                                STAY ALIVE

                                                                     DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                                              0653095635/0769846183

UFAHAMU UPASUAJI WA KUPUNGUZA MAFUTA MWILINI,(liposuction)

Liposuction ni nini?
Hii ni aina ya upasuaji ambayo inatumika kuondoa Mafuta mwilini kwa watu wanene,  mara nyingi hutumika kuondoa Mafuta tumbo, mapaja, shingo, kidevu, mgongo na mikono.
Mafuta huondolewa kwa Bomba Fulani maalumu ambalo huwekwa chini ya ngozi kisha presha kubwa sana hutumika kuvuta Mafuta hayo.
Nchini marekani hii ni moja ya upasuaji ambao unafanyika sana Sababu ya watu wengi huko kua wanene na data zinaonyesha kwamba zaidi ya watu laki tatu kila mwaka hufanyiwa upasuaji huo.
                                                                         
Je upasuaji huu unafaa watu wa aina gani?
Huu upasuaji sio wa kupunguza Uzito kwa watu wanene ila ni kwa ajili ya kuondoa Mafuta ya ziada sehemu mbali mbali za mwili hasa baada ya kushindikana kutoka kwa mazoezi na diet ya kupunguza Uzito.
Lakini pia mtu anaweza kua ni mwembamba lakini ana sehemu ya mwili ambayo ina mafuta mengi na ameshindwa kuyatoa kwa mazoezi na chakula.

Mafuta yanavutwa vipi?
kuna  aina mbali mbali za kufanya upasuaji huu lakini mara nyingi upasuaji maarufu kitaalamu kama tumescent liposuction hufanyika kwa kumpa mgonjwa Dawa ya usingizi au Dawa ya ganzi kisha sehemu ambayo inatakiwa itolewe Mafuta inawekewa Maji maalumu(normal saline) na Dawa ya kukunja Mishipa ya damu(adrenaline) kisha Mafuta huvutwa nje.
Baada ya upasuaji sehemu zilizotolewa Mafuta huota huvimba kwa muda(inflammation) hivyo matokeo ya upasuaji yataonekana baada ya wiki nne uvimbe ukishapungua.
                                       
Nini kifanyike baada ya upasuaji?
Mgonjwa anatakiwa ajaribu kula vizuri baada ya upasuaji ili kuzuia kunenepa tena Kwani upasuaji huu hauzuii mtu kunenepa tena.
Watu wenye ngozi inayovutika hufaidi upasuaji huu kwani ngozi hujivuta kawaida lakini watu ambao hawana ngozi ya kuvutika huishia kua na ngozi kubwa iliyolala ambayo baadae itahitaji upasuaji mwingine.

Nini madhara ya upasuaji huu?
Kama ilivyo kwa upasuaji wa aina yeyoye, upasuaji huu pia una madhara kama kuvimba mwili kwa muda Mrefu, kuganda kwa damu, shepu kutoka vibaya, ganzi, au kifo kutokana na madhara ya dawa za usingizi.
                                                                            STAY ALIVE

                                                       DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                                          0653095635/0769846183
                                                           
                       

UFAHAMU UTAPELI WA DAWA ZA KUHARISHA ILI KUPUNGUA UZITO.

Kumekua na ongezeko kubwa la watu wanene na vitambi ambao wanahitaji sana kupungua uzito, lakini tatizo kubwa liko palepale kwamba watu wanataka kupungua haraka kuliko kawaida.
Yaani unene uliopatikana kwa miaka miwili mpaka kumi mtu anataka kuupunguza kwa siku moja au wiki kitu ambacho sio cha kawaida na huweza kua hatari kiafya.
Kuna dawa maarufu sana ambazo zinauzwa sana mtaani huku zikidai kwamba zinaweza kupunguza uzito kwa muda mfupi tu.
Inasemekana baada ya kunywa dawa hizo mteja huharisha mafuta yote na baadae anakua mwembamba.

Dawa hizo ni hazina ukweli wowote na mtu anayetumia anakua haelewi kabisa jinsi mwili unavyofanya kazi na anahatarisha maisha yake kama ifuatavyo.
mtu hapungui unene ila anakonda na kusinyaa; siku zote ukiharisha unakua unatoa maji mwilini, kihesabu lita moja ya maji ni sawa na kilo moja ya uzito hivyo ukiharisha lita tano ni sawa umepungua kilo tano,na kwasababu sehemu kubwa ya mwili wa binadamu ni maji basi utasinyaa na kua mdogo.
Kwa matokeo ya haraka mtu ataona uzito umepungua lakini ni maji ndio yamepungua mwilini sio Mafuta na baada ya hapo uzito utarudi kwani utaanza kunywa maji na kurudisha yaliyopotea.
unahatarisha maisha; kuharisha sio hali ya kawaida mwilini ndio maana watu wakiugua kipindupindu hua wanakufa, kuharisha kunapoteza kiasi kikubwa cha madini ya potassium ambayo inasaidia sana misuli ya mwili na moyo.
Hali hii humfanya mgonjwa kuishiwa nguvu sana, mapigo ya moyo kutokwenda kawaida na hata kusimama kabisa kwa mapigo ya moyo na kifo.
mafuta yako hayako kwenye utumbo; hata kama kweli ingekua ukiharisha mafuta yanatoka, mafuta ambayo yanakufanya uonekane mnene yasingetoka kwani yapo chini ya ngozi yako na sio ndani ya utumbo.
Huwezi kutoa mafuta ya usoni, mgongoni na kifuani, mapajani, kifuani na tumboni kwa kuharisha tu.
mwisho; njia bora kabisa ya kupungua uzito ni kupunguza ulaji wa chakula hasa wanga na sukari, mazoezi na kupungua taratibu angalau kilo mbili kwa mwezi lakini mwisho wa siku hata ukishapungua lazima mfumo wako wa maisha ubadilike kwani mfumo wako wa maisha ya zamani ndio umekufikihsa hapa ulipo leo.
                                                                         STAY ALIVE

                                                        DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                                    O653095635/0769846183

UZAZI WA MPANGO WA KUCHOMA SINDANO KWENYE UUME KUANZA KUTUMIKA.

Kwa miaka mingi njia za uzazi wa mpango zimekua zikitumika kwa wanawake tu, isipokua njia moja ya upasuaji kitaalamu kama vasectomy ndio ilikua ikutumika kwa wanaume na kwasababu njia hiyo ukiitumia huwezi kuzalisha tena basi wanaume wengi walikua wanaikwepa.
                                                                             
Njia hii mpya ya uzazi wa mpango itahusika kuchoma sindano kwenye uume imefanikiwa kwenye majaribio kwenye shirika la utafiti huko nchini india.
Akiongea na gazeti la Hindustan nchini india, Mwenyekiti wa shirika hilo la utafiti Dr.Sharma amesema kwamba dawa hiyo iko tayari inasubiri kibali cha serikali.
Utafiti huo ambao ulitumia awamu tatu, uliwahusisha watu 303 na matokeo yalionyesha kwamba dawa ilikua na uwezo wa 97.3% na ilikua na uwezo wa kudumu na kufanya kazi mpaka miaka 13.
Kitaalamu dawa hii itachomwa kwemye mirija inayotoka kwenye korodani kwenda kwenye uuume kitaalamu kama vas difference.

Wakati huohuo huko nchi marekani dawa ya uzazi wa mpango kwa wanaume kwa ajili ya kumeza imeshagunduliwa na kufanyiwa majaribio.
Watafiti wanaamini kwamba itakua tayari baada ya miaka kumi.

                                                          STAY ALIVE
                                   DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

                                               0769846183/0653095635

WAGONJWA WA UKIMWI KUANZA KUCHOMWA SINDANO MOJA KILA MWEZI BADALA YA VIDONGE.

Moja ya changamoto kubwa ya kupambana na ugonjwa wa ukimwi ni kushindwa kumeza vidonge  vya ARV kila siku na wakati uleule  kwa maisha yako yote.
Watu wengi huchoka kumeza kutokana na madhara mbalimbali ya dawa, kumeza kwa kujificha na kushindwa hata kuhifadhi dawa hizo nyumbani sababu ya unyanyapaa mkubwa.
Hali hii hufanya wagonjwa wengi kutoanza dawa au kuacha kabisa dawa na kusubiri kufa tu baada ya kukata tamaa.

Lakini kwa sasa tumaini jipya liko njiani baada ya watafiti kugundua dawa za ARV ambazo zitatolewa kwa mfumo wa sindano badala ya vidonge.
Utafiti huo uliwasilishwa katika mkutano mkuu wa virusi vya ukimwi uliofanyika jijini paris ulionyesha kwamba dawa hizo za kuchomwa zilikua zina uwezo sawa na zile za kumeza.
Utafiti huu ulifanyika  kwa watu 1000 katika nchi 16 dunaini ambapo dawa za ARV kwa jina la  cabotegravir rilpivirine zilionyesha uwezo wake mzuri wa kufanya kazi.

Sindano hizi zitaweza kutumika kama pre exposure yaani unaweza kuchoma kama hujaathirika na kukaa mwezi mmoja bila kua na hatari ya kuambukizwa au post exposure ambayo unaweza kuchomwa baada ya kulala na muathirika au kujichoma sindano ambayo inahisiwa kua na damua ya muathirika.
Utafiti huu unaamini kupunguza sana maambukiziya ukimwi kwani kuriuka dozi moja tu ya kumeza inahatarisha sana maambukizi kwa mwenza wa mgonjwa lakini pia inawapa uhuru sana kwamba badala ya kua na siku 365 za kumeza dawa kwa mwaka sasa watakua na siku 12 tu kwa mwaka yaani sindano moja kila mwezi.
Mfumo huu wa kumeza vidonge pia ulileta changamoto hat kwa watoto wadogo ambao wengi wanashindwa kueza dawa hizo kutokana na uchungu au ladha mbaya na kushindwa kufuata ratiba zake vizuri.

                                                           STAY ALIVE
                                      DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                            0653095635/0769846183

VIRUSI VIPYA VYA UKIMWI VYAGUNDULIWA.

Moja ya changamoto kubwa wakati wa kutafuta dawa ya ukimwi ni kubadilika badilika kwa kirusi hicho kwenye mifumo na maumbo mbalimbali.
Wanasayansi nchini marekani wamegundua kirusi kipya cha ukimwi kwa mara ya kwanza baada ya miaka 20.
Kirusi hicho ni sehemu ya familia ya kile kirusi cha zamani ambacho kimeathiri na kuua wengi duniani kote kwa ujumla kitaalamu kwa jina la HIV-1 Group M.
M ikisimama kwa maana ya major kwani imeathiri watu wengi sana duniani kote kwa ujumla.

Sampuli za damu ambazo zimekutwa na virusi hivi vya ukimwi zilichukuliwa nchini congo kati ya mwaka 1980 mpaka 2001.
“Bahati nzuri utafiti huu unaonyesha kwamba dawa zilizopo zina uwezo wa kutumika kutibu kirusi hiki lakini hakuna uhakika kama vipimo vinavyotumika kwa sasa vina uwezo wa kuwatambua wagonjwa wenye virusi hivi’.Anasema Dr.Antony Fauci kiongozi kitengo cha magonjwa ya kuambukiza nchini Marekani.

‘Ugunduzi wa kirusi hiki unatukumbusha kwamba kumaliza ugonjwa wa ukimwi bado tunahitaji teknolojia ya hali ya juu kuvielewa virusi hivi’, anasema Dr Marry Rodgers.
Kitengo cha kupambana na kuzuia na magonjwa maarufu kama CDC nchini marekani kinaamini kwamba kuna zaidi ya wagonjwa milioni 40 walioathirika na ugonjwa huu duniani kote huku zaidi ya wagonjwa milioni moja wakiishi marekani na 14% duniani kote hawajua kama ni waathirika.

                                                                             STAY ALIVE

                                                    DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                                0653095635/0769846183

HUYU NDIO MGONJWA WA UKIMWI MWENYE UMRI MKUBWA ZAIDI DUNIANI.

Ugojwa wa ukimwi ulipogunduliwa mara ya kwanza miaka ya 1980 uliua watu wengi kwa kasi ya kutisha na wengi waliogunduliwa na ugonjwa huu walisubiri kufa tu kwani palikua hakuna tumaini lolote.
Miaka kadhaa baadae baada ya kugundulika dawa za kupunguza makali, tafiti zilionyesha kwamba mgonjwa asingeweza kuzidi miaka 20 baada ya kuambukizwa.
Kama hatakufa kwa matatizo ya ugonjwa wenyewe basi atakufa kwa madhara ya dawa hizi kama kuharibika kwa maini,figo na kadhalika.

Siku za karibuni mambo yamebadilika kidogo ambapo tafiti zinaonyesha kwamba tofauti ya mtu mwenye virusi na asiyekua navyo ni miaka 13 tu kwa maana nyingine ni kwamba kama mtu ambaye hana virusi anaishi miaka 73 basi mwenye virusi anaweza kuishi miaka 60, hesabu hii imeletwa hivi kulingana na kutofautiana kwa urefu wa maisha wa nchi tofauti.

Mtu mmoja kutoka ureno kwa jina la miguel amekua binadamu wa kwanza kufikisha umri mkubwa sana akiwa na virusi vya ukimwi.
Miguel aligunduliwa na virusi hivi miaka 16 iliyopita akiwa na umri wa miaka 84 na kwa wakati huo vipimo vilionyesha kwamba alikua ameugua kwa muda mrefu kabla bila kujua kwani alikua katika hatu ya 3 ya ugonjwa huu.

Wakati anagunduliwa na ugonjwa huu kulitokea mvutano kati ya madaktari kama kweli dawa zingemsaidia kwani umri ulikua umeenda sana lakini baadae madaktari waliamua kumpa dawa aanze.
Miguel anasema ile ilikua kama bahati kwani dawa hazikuwahi kumsumbua na sasa amefikisha miaka 100 akiwa na ugonjwa huu.
Miguel anasema kwamba hajawahi kuacha wala kuruka maumizi ya dawa tangu alipogunduliwa na ugonjwa huu.

Kwasababu ya unyayapaa ambao bado unaendelea dhidi ya wagonjwa wa ukimwi, Miguel hakupenda sura yake iwekwe hadharani lakini pia jina lake halikutajwa lote.
Historia hii inatoa mwanga kwa jamii yetu ya wagonjwa na ambao sio wagonjwa wa ukimwi kwamba kuna matumaini makubwa ya kuishi miaka mingi na kumeza dawa kwa wakati ni njia bora ya kufika huko.

                                                                             STAY ALIVE

                                                      DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                                 0653095635/0769846183

HIVI NDIO UPUNGUFU WA SUKARI MWILINI UNAVYOWEZA KUUA MTU.

Kwa wagonjwa wa kisukari, tatizo la kushuka sana kwa sukari ni hatari zaidi kuliko tatizo la kupanda kwa sukari.
Kwa hali ya kawaida sukari ikishuka huweza kuua ghafla lakini sukari ya kupanda haiwezi kumuua mtu ghafla, hali hii iko zaidi kwa watoto wadogo na wagonjwa wa kisukari.
Sababu mbalimbali huweza kuchangia kushuka kwa sukari ghafla ikiwemo kuchoma dawa nyingi ya kushusha sukari, kuchelewa kula, kufanya mazoezi sana,kunywa pombe na saratani za kongosho.
Wakati sukari inashuka kuna dalili za mwanzo na dalili za mwishoni, kua makini sana na dalili za mwanzoni kwani kipindi hicho ndio unakua una uwezo wa kujiokoa lakini baada ya hapo unakua huwezi tena kujiokoa bila msaada kutoka kwa watu wengine.

dalili za mwanzo za sukari kushuka.

  • kizunguzungu
  • kutokwa jasho
  • njaa kali
  • wasiwasi
  • kichwa kuuma
  • kuloanisha mashuka kwa jasho wakati wa usiku
  • kuota ndoto za ajabu
dalili za mwisho baada ya sukari kushuka sana
  • degedege
  • misuli kuishiwa nguvu
  • kushindwa kuongea
  • kuchanganyikiwa
  • kupoteza fahamu
  • kuona ukungu.
vipimo
kwenye kipimo cha sukari au glucometer, pale inapokua chini ya 3.0mmol/l basi ni dalili kwamba sukari imeshuka sana na inaelekea kubaya.
matibabu
mgonjwa katika dalili za mwanzo anaweza kunywa glucose, juice au soda na kupata nafuu kisha kutafuta chakula na kukila, lakini mgonjwa wa dalili za mwisho anatakiwa akimbizwe hospitali kuwekewa sukari kwa njia ya mishipa au dripu.
ni vizuri mgonjwa wa kisukari kuwaambia ndugu zake kuhusu dalili hizi ili waweze kumsaidia ikitokea hajiwezi kabisa.

jinsi ya kuzuia hali hii.
usichelewe kula; baada ya kuchoma dawa ya kushusha sukari au insulin basi hakikisha umekula kwa wakati ili kuzuia kuporomoka sana kwa kiwango cha sukari.
pima kiwango cha sukari; kupima mara kwa mara ni njia pekee ya kujua kiwango chako cha sukari kikoje, sio kwa ajili ya kuogopa sukari inayoshuka tu ila hata ile ya kupanda ni hatari kwa afya yako kama ikiwa imepanda muda wote.
kunywa pombe na chakula; sukari hushuka sana mgonjwa anapokunywa pombe bila chakula hivyo hakikisha umekula kwanza kabla ya kunywa pombe.
mazoezi yako yaendane na dawa unayotumia; ukifanya mazoezi sana hakikisha unapunguza dozi ya dawa unayotumia kwani mazoezi hupunguza sana sukari mwilini.

                                                                              STAY ALIVE
                                                       DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                                0653095635/0789846183

FAHAMU DALILI ZA KUPANDA KWA SUKARI KWA WAGONJWA WA KISUKARI.

Kupambana na kiasi cha Sukari kwenye damu kwa wagonjwa wa kisukari ndio msingi mkuu wa matibabu ya ugonjwa wa kisukari kwani huepusha madhara makubwa yatokanayo na ugonjwa huu kama kuharibika kwa figo, ugonjwa wa presha, upofu. matatizo ya mishipa ya fahamu na kadhalika.
Kwa kawaida sukari ya mgonjwa ikiwa zaidi ya 7.1mmol/l baada ya saa 8 bila kula au zaidi ya 10mmol/l saa 2 baada ya kula hutambulika kitaalamu kama hyperglaicemia au sukari ya juu kwa wagonjwa hawa.

nini chanzo cha kupanda sukari kwa wagonjwa hawa?
wagonjwa wengi wa sukari hupata tatizo la sukari zao kupanda sana hata kama wako kwenye dawa na hii husababishwa na sababu zifuatazo.
kutomeza au kutochoma dawa kwa wakati: wagonjwa ambao hawamezi dawa au kuchoma sindano za sukari kama walivyoelekezwa na wataalamu wa afya huishia kupata tatizo la kupanda sukari juu kuliko kawaida.
kula wanga mwingi sana; kimsingi wagonjwa wa sukari wanatakiwa wale vyakula vya wanga kidogo sana na siku zingine ikiwezekana wasile kabisa.
Vyakula vya wanga kama ugali,wali, viazi, tambi, mihogo, chapati, mikate, maandazi, keki na kadhalika huongeza sukari sana ukilinganisha na vyakula vya protini na mafuta kama nyama, samaki, karanga, korosho, maziwa, mayai, na kadhalika.
kuugua; mgonjwa wa sukari akiuugua ugonjwa wowote yaani kama malaria, typhoid, u.t.i au magonjwa yeyote mengine unayojua wewe lazima sukari ipande hivyo kwa kipindi hiki hata kama anapewa dawa za sukari, kama ugonjwa haujafahamika basi sukari haiwezi kushuka.
msongo wa mawazo; msongo wa mawazo huchangia sana homoni zingine mwilini ambazo husababisha kupanda kwa sukari kwenye damu.
kua mvivu; kama wewe ni mtu wa kufanya shughuli mbalimbali kama kutembea, kwenda kazini, kufanya kazi za nyumbani, kwenda mazoezini na kadhalika kisha ikatokea ukaacha hizo shughuli na kushinda nyumbani basi uko kwenye hatari ya kupandisha sukari mwilini.

dalili za sukari kupanda ni zipi?
  • kusikia kiu sana
  • kichwa kuuma
  • kushindwa kutuliza akili sehemu moja.
  • kuona ukungu
  • kukojoa mara kwa mara 
  • kuishiwa nguvu
  • sukari kupanda zaidi ya 10mmo/l kwenye kipimo cha damu.
hali hii ikiendelea kwa muda mrefu husababisha
  • magonjwa ya ngozi ya mara kwa mara
  • kuchelewa kupona kwa vidonda
  • ganzi
  • choo ngumu sana au kuharisha.

matibabu ya hali yapi?
matibabu ya sukari kupanda yanategemea sana chanzo cha ugonjwa husika cha kupanda kwa sukari hiyo na huweza kufanyika nyumbani au hospitali kama ifuatavyo.
kunywa maji mengi; maji mengi husaidia sana kupunguza sukari mwilini kwa kuondoa sukari kupitia mkojo lakini pia huzuia kupungua kwa maji mwilini.
fanya mazoezi; mazoezi husaidia sana kupunguza sukari, lakini ikiwa sukari imepanda usifanye mazoezi kwanza bila kuhakikisha kwamba umepima mkojo, ni hatari sana kufanya mazoezi iwapo mkojo wako una vitu vinaitwa ketones.
badili mfumo wa chakula; epuka vyakula vya wanga na sukari na tumia muda mwingi kula vyakula vya ptotini na matunda ambayo hayana sukari.
badilisha dawa; wakati mwingine dawa hazikufai au dozi ni kidogo hivyo onana na daktari wako anaweza kukubadilishia mfumo wa kumeza au akaongeza dozi.
chukua vipimo; wakati mwingine ni ugonjwa mpya unakusumbua hivyo ni vizuri kwenda hospitali kupima magonjwa mbalimbali.

                                                               STAY ALIVE

                                        DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                      0653095635/0769846183

FAHAMU KUHUSU MAJI YANAYOMWAGIKA KUTOKA KWA MWANAMKE AKIFIKA KILELENI.(squrting)

Squrting ni nini?
Hii ni hali ya mwanamke kumwaga maji kutoka sehemu za siri wakati anafika kileleni, hii huambatana na msisimko mkali wa kuishiwa nguvu, kutetemeka hata kukaa chini.
kuna aina mbili za mwanamke kufika kileleni, moja ni hiyo niliyoandika hapo juu na ya pili ni ile mwanamke anatoa kama utando mweupe ambao unaonekana kusambaa  kwenye uume  wakati tendo hili la ndoa likiendelea, lakini maada hii itazungumzia maji yanayoruka wakati mwanamke anafika kileleni.

jee ni hali ya kawaida?
Hii ni hali ya kawaida kabisa japokua watu wengi hua hawapendi kuizungumzia, kwa miaka mingi watafiti walidhani kwamba huenda wanawake wanaomwaga yale maji wanakua na tatizo la fistula na wengine walidhani maji yale yanatoka ukeni.
Lakini utafiti uliofanyika mwaka 2014 uligundua kwamba hali ile ni ya kawaida na maji yale yanatoka kwenye kibofu cha mkojo.
Utafiti ulifanyika kwa kipimo cha utrasound ambapo mwanamke aliambiwa akakojoe ili kuondoa mkojo wote ndani ya kibofu cha mkojo kisha alianza kujichua huku kipimo cha utrasound kikiangalia hali ya kibovu cha mkojo.
utafiti ulionyesha kwamba, wakati mwanamke anaendelea kujichua maji yalianza kujaa tena kwenye kibovu cha mkojo na alipofika kileleni na kumwaga maji kama kawaida, picha ya utrasound ilionyesha kupotea kwa maji yale, hii ilionyesha kweli maji yale yanatoka kwenye kibofu cha mkojo bila mwanamke kuyatoa mwenyewe kwa hiari.

wanawake wangapi wanafika kileleni kwa staili hii?
Tafiti zinaonyesha kwamba asilimia kumi mpaka hamsini wanafika kileleni kwa kumwaga maji, lakini wataalamu wanaamini kwamba wapo ambao wanaishia kwenye hatua ya kujaza maji kwenye kibovu lakini yale maji hayatoki.
utafiti uliofanyika kwa wanawake 233 ulibaini kwamba 14% walifika kileleni kwa kumwaga maji kila wakati wakilala na wanawake huku 54% walisema hali kama hiyo ishawahi kuwakuta mara moja au mbili.
Utafiti pia unaonyesha kwamba hali ya mwanamke kumwaga maji vile hutegemea na hisia alizonazo kwa mtu huyo na uwezo wa mwanaume huyo kumkuna vizuri anapotaka yeye.

je kuna tofauti kati ya mkojo na maji yanayotoka wakati wa kufika kileleni?
Ndio, maji yanayotoka wakati wa kufika kileleni hua hayana rangi kabisa pia kuna maji yale yana kiasi kikubwa cha sukari aina ya fructose ambayo husaidia mbegu za kiume kusafiri haraka pale mwanaume anapomwaga mbegu kwenye uke huo.

mwisho; kuna wanawake wengi sana ambao wanahisi kwamba hali ile ya kumwaga maji sio yao lakini huenda hawajakutana na watu sahihi ambao wana uwezo wa kuwafanya hivyo.
badhi ya wanawake hali hii walikutana nayo baadae sana baada ya kuingia kwenye mahusiano mengine.

HIZI NDIO SABABU ZINAZOFANYE UKE WA MWANAMKE KULEGEA NA KUA MKUBWA.

Katika mambo ambayo yamepotoshwa sana kwenye jamii yetu ni kuhusu kulegea na kutanuka kwa uke wa mwanamke.
Jamii yote inaamini kwamba kulegea kwa uke kunasabishwa na mwanamke kufanya tendo la ndoa mara kwa mara, kulala na wanaume wengi au kulala na mwanaume mwenye uume mkubwa, kitu ambacho hakina ushahidi wowote kitaalamu.
                                                             
 
Ni kweli uke una tabia ya kulegea katika hatua fulani ya maisha ya mwanamke lakini kuna sababu zingine ambazo zinahusika kama ifuatavyo.
umri; kadri umri unavyozidi kwenda misuli yote ya mwili inaanza kuishiwa nguvu na ngozi kuanza kutoa makunyazi.
Katika umri wa miaka 40 mara nyingi kiwango cha homoni za uzazi ambazo zinahusika na shughuli za uke huanza kupungua na uke unaanza kulegea na kupungua kiasi cha maji.
Katika umri wa miaka 50 ambapo mara nyingi hedhi husimama, uke hua mkavu kabisa na kua mdogo mno kiasi kwamba hata tendo la ndoa linaanza kua gumu.

kuzaa watoto; kipindi cha kuzaa mtoto, uke wa mwanamke hutanuka sana ili mtoto aweze kupita vizuri, wanawake wengine huzaa watoto wakubwa kuliko wegingine.
Sasa uharibifu unaosababishwa na mtoto kutoka ni mkubwa, japokua uke hurudi kwenye hali yake ya zamani baada ya kuzaa lakini hautaweza kua kama mwanzo kabisa.

maumbile asili; kuna watu ambao wameumbwa hivyo, kwamba maumbile yao ya kike ni makubwa yaani kama jinsi wanaume wanavyokua na maumbile tofauti.
Ukisikia mwanamke anapenda uume mkubwa basi ujue maumbile yake ndio yanaridhishwa na aina hiyo lakini kuna wanawake wengine ambao uume mkubwa kwao ni mateso na maumivu makali.

mwisho; kuna mazoezi ya kubana uke yanafahamika kama kegel, kama umezaa watoto au umri umeenda na unataka kuendelea kua mbichi basi unaweza kuyafanya na misuli yako ya uke ikawa na nguvu kama mwanzo.
mazoezi haya hufanyika kwa kubana msuli ambao unafanya kazi ya kuzuia na kuachia mkojo mara kwa mara.

                                                                     STAY ALIVE

                                          DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                    0653095635/0769846183
                                                             

YAFAHAMU MATIBABU YA UKOSEFU WA MAZIWA BAADA YA KUJIFUNGUA.

Baada ya kujifungua, baadhi ya akina mama hutoa maziwa kidogo sana kwa ajili ya watoto wao na wengine hukosa kabisa maziwa.
Hali hii huleta changamoto kubwa kwani mtoto huanza kulia sana na wakati mwingine kuishiwa maji mwilini na kuchemka.
Kitaalamu baada ya kujifungua homoni nyingi za uzazi zinapungua kisha homoni zingine kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa kitaalamu kama prolactin hutengenezwa, sasa kuchelewa kwa kwa hatua hii kunaweza kuleta shida hii.
Lakini pia zipo sababu zingine za tatizo hili na unaweza kuzisoma hapa.......http://www.sirizaafyabora.info/2016/09/sababu-kumi-za-kuishiwa-au-kukaukiwa.html

mambo gani unaweza kufanya kutibu tatizo hili?
usiishiwe na maji mwilini: hakikisha unakunywa maji ya kutosha angalau glass nane kwa siku ili kuongeza kiasi cha maji mwilini mwako.
kumbuka maziwa yako kwenye mfumo wa kimiminika hivyo maji mengi yanahitajika kuyatoa.
kula mlo kamili; ungeza ulaji wako wa zamani kwa zaidi kidogo, vyakula vya protini kama mayai, nyama,maziwa nay ng'ombe samaki na mboga za majani husaidia sana sana kuzalisha maziwa ya kutosha ambayo yanaweza kukidhi mahitaji ya mtoto.
tumia virutubisho; taasisi  nyingi za kiafya zinashauri matumizi ya madini ya clacium, vitamin D, Iron, na folic acid kama kiungo muhimu sana katika kumuandaa mama kuzalisha maziwa mengi na yenye virutubisho vya kutosha ndani yake.
nyonyesha mara kwa mara; hata kama maziwa ni kidogo sana jitahidi kumnyonyesha mtoto mara nyingi sana iwezekanavyo yaani mara 10 mpaka 12 ndani ya saa 24 au kila anapohitahi na hii itasaidia sana kutengeneza homoni ya oxytocin ambayo husaidia sana kutengeneza maziwa.
nyonyesha ziwa moja moja; ukimpa mtoto ziwa moja mpaka maziwa yakaaisha kabisa, taarifa hutumwa kwenye ubongo kwamba maziwa yameisha kabisa hivyo ziwa lingine litajazwa maziwa haraka wakati mtoto anamalizia kunyonya ziwa lingine.
matumizi ya dawa; wakati mwingine baadhi ya dawa hutumika hasa pale kiwango cha homoni inayohusika na maziwa inapoenekana iko chini sana na haiwezi kuongeza kiwango cha maziwa.
dawa ya dompiredone huweza kutumika kwa dozi ya 10mg kutwa mara nne na kuongeza mpaka kiwango cha mwisho cha 20mg kutwa mara nne.
Mama anaweza kupunguza dozi na kuacha kabisa kama maziwa yakipatikana, ila ikitokea maziwa yanapungua tena basi ataanza dozi na kuendelea nayo mpaka atakapomuanzishia mtoto vyakula vingine, mara nyingi baada ya miezi sita.
mwisho; wakati mwingine mama anaweza asipate nafuu pamoja nakutumia dawa zote, huenda sababu ya vyanzo vingine ambavyo vinakua nje ya matibabu kama historia ya upasuaji wa matiti na kadhalika hivyo anaweza kutumia maziwa mbadala ya lactogen au maziwa ya ng'ombe ambayo mchanganyiko wake umetajwa hapa.....http://www.sirizaafyabora.info/2015/05/jinsi-ya-kutengeneza-maziwa-ya-mtoto.html

                                                              STAY ALIVE

                                  DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                0769846183/0653095635

JINSI YA KUJIOKOA KUTOKA KWENYE GARI AMBAYO INAZAMA KWENYE MAJI.

Siku chache zilizopita mama mmoja na na mtoto wake nchini kenya walizama kwenye maji na kupoteza maisha, inasemekana gari ile ilidondoka kutoka kwenye kivuko.
Kila mwaka zaidi ya ajali 10000 hutokea duniani kote, wengi hufariki na wachache huweza kujiokoa katika majanga kama hayo.
Wataalamu wanaamini kwamba dakika moja ya kwanza ndio inaamua kwamba wewe utakufa au utabaki hai, ukifanya makosa katika muda huu basi uwezekano wa kutoka hai haupo.
Kwenye makala hii ntaenda kuzungumzia mambo muhimu ya kufanya ili uweze kutoaka hai ndani ya gari linalozama kwenye maji kama ifuatavyo;
tulia kabisa bila kupaniki; sio rahisi kutumbukia kwenye maji bila kupaniki lakini jitahidi unavyoweza kujituliza ili kufanya maamuzi sahihi, ukianza kutumia nguvu nyingi ndio utaishiwa hewa na kufa mapema.
watu wengi wana tabia ya kuanza kuwapigia simu ndugu zao wa karibu na mwisho wa siku ndugu hao hawawezi kufika eneo hilo kwa wakati.
vunja kioo cha dirishani; gari ikizama kwenye maji, presha ya nje inakua kubwa sana kuliko presha ya ndnai kiasi kwamba huwezi kufungua mlango, mlango hufunguka baada ya muda fulani maji yakishajaa ndani ya gari hivyo kama muda huo utakua bado uko hai basi utatoka salama.
sasa kuliko kusubiri mlango ufunguke basi ni bora uvunje kioo kwa kutumia kitu chochote kigumu au kiwiko chako cha mkono.
Kioo ni kigumu kidogo hivyo kinahitaji nguvu ya ziada kukipasua kwa kiwiko cha mkono.
toka haraka dirishani: baada ya kupasua kioo maji huingia kwenye gari kwa kasi na gari haunza kuzama haraka, huu ni muda wa kutoka haraka dirishani na kuogelea kwenda juu ili uweze kupata msaada na kuokolewa.
kama una abiria; kama uko na abiria basi msipoteze muda kubushana nini cha kufanya, wape mpango wako kisha vunja kioo, mkianza kubishana nani anajua kuogelea na nani hajui basi mtakufa wote.
kama kuna mtoto basi mshike mkono utoke naye, kwa ambao hawajui kuogelea ni vizuri wakatoka hivyohivyo kwani maji yatawarudisha juu na pia ni rahisi kupata msaada kuliko kushuka na gari mpaka chini ya ziwa au bahari.
mwisho;majanga haya hutokea mara kwa mara, kama sio vibaya kua na boya la kuogelea kwa watu wasiojua kuogelea kwenye gari na kifaa chochote kigumu kama nyundo iwapo ikitokea shida kama  hii uweze kuokoka.

                                                                    STAY ALIVE

                                           DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                             0653095635/0769846183

JINSI YA KUEPUKA MICHUBUKO WAKATI WA TENDO LA NDOA ILI KUZUIA MAAMBUKIZI YA UKIMWI.

Sio kila anayefanya ngono na mgonjwa wa ukimwi anapata maambukizi, kuna watu wameishi na wagonjwa wa ukimwi miaka na kuzaa watoto lakini bado hawakupata maambukizi haya ya virusi vya ukimwi.
                               
         
Tafiti zinaonyesha kwamba ukilala na muathirika wa ukimwi basi uwezekano wakupata maambukizi ni asilimia 0.002 mpaka asilimia 1, kwa maana nyingine ni kwamba kati ya watu 100 mpaka 500 wanaolala na waathirika wa ukimwi ni mmoja anayepata maambukizi.
Hatari ya maambukizi huongezeka kwa asilimia 1 mpaka 1.4 kwa watu ambao wanafanya ngono kinyume na maumbile.
Kama ingekua kila anayelala na muathirika wa ukimwi na yeye anapata basi watu wangeisha kwani sisi wote tumeunganishwa kwenye mnyororo mmoja wa ngono bila kujuana.
Pamoja kwamba mnaweza kupima kabla ya kuanza mahusiano kitu ambacho kweli ni muhimu, bado Kuna haja ya kuendelea kua makini kwani watu wengi sio waaminifu na waathirika wengi ni wanandoa  na watu ambao wako kwenye mahusiano sababu yakuaminiana sana.
yafuatayo ni mambo unayoweza kufanya kuzuia michubuko na kukuepusha maradhi ya mbalimbali ikiwemo ukimwi.
maandalizi mazuri; Hakikisha mwanamke ameloa vya kutosha muda wote wa tendo la ndoa na hii ni matokeo mazuri ya kumuandaa vizuri kabla ya tendo la ndoa na ukiona ukavu umeanza basi sitisha na muandae tena, kamwe usikubali kuendela na tendo la ndoa wakati unasikia uke ni mkavu kabisa au unasikia maumivu.
tumia vilainishi; watu wengi wanaamini vilainishi ni kwa ajili ya kuingiliwa kinyume na maumbile kitu ambacho sio kweli.
kama mwanamke unaona umeshindwa kuloana kwa sababu ambao ziko nje ya uwezo wako basi unaweza kutumia vilainishi hivi kuepuka michubuko.
kama wewe ni kijana ambaye hua unashiriki tendo la ndoa basi sio vibaya kua nayo nyumbani.
epuka ngono ya kukomoa; kama mwanaume achana na mawazo yakumkomesha mwanaume, huwezi kumkomesha mwanamke kwa sex, ile sehemu mtoto anapita, wewe ni nani? fanya mambo yako kaa pembeni.
Ni rahisi sana kumridhisha mwanamke kwa round moja tu au mbili, ukizidi hapo mara nyingi anakua mkavu na kukauka.
ndio maana maambukizi yako juu kwa vijana kuliko wazee ambao hawana muda wala nguvu za kukomesha.
fanya taratibu; usidanganywe na video za ngono, mwanamke anaweza kuridhika sana kwa tendo la ndoa la taratibu kuliko ile ya fujo ambayo umeaminishwa kuiamini.
kufanya ngono taratibu kunaongeza msisimko, maji mengi ukeni na kupunguza uwezekano wa kuchubuka kwani unatumia nguvu kidogo sana kuingia na kutoka.
kua msikivu; kama kuna staili ambayo unaona ukimuweka mwenza wako anasikia maumivu au analalamika basi achana nayo, mwanamke akianza kusikia maumivu anakosa hamu ya tendo na kukauka haraka huku akisubiri umalize tu avae nguo.
hakikisha anafika kileleni; jaribu kua mtundu na kuhakikisha mwenza wako anafika kileleni siku zote, kumfikisha kileleni siku zote kunamfanya mwanamke aloane sana na kupunguza sana uwezekano wa kuchubuka.
bahati nzuri mwanamke anaweza kuingia kileleni hata mara nne au tano wakati mwanaume akifika kileleni mara moja au mbili.
usioshe uke na maji kama bado unaendelea; mwanamke anaweza kuosha uke wake kabla ya tendo la ndoa, sio kitu kibaya kwani maandalizi hayajaanza.
Lakini kwenda kuosha tena baada ya mshindo wa kwanza unapafanya kule kua kugumu na kukavu kwani maji sio laini, hivyo utaleta ukavu ambao haukuepo mwanzoni.
usilazimishe; kama mwanamke amechoka au ana sababu nyingine yeyote ya kutojisikia kufanya ngono basi usitumie nguvu kwani utajikuta umelala na mtu mkavu, mara nyingi watu ambao wanabakwa au kubaka huambukizwa maambukizi ya ukimwi sababu ya kufanya ngono na watu ambao hawakua tayari.
mwisho; tendo la ndoa sio vita, jipe muda wa kutosha kujiandaa kiakili na kimwili kabla ya kushiriki, hii itakuletea raha na kukuzuia na magonjwa mbalimbali ambayo ni hatari sana kwa mwili wako.

MAMBO 8 YANAYOWEZA KUHARIBU MUONEKANO MZURI WA MWANAWAKE.

Ukiumuona mwanamke baada ya kuvunja ungo basi utagundua kweli mungu aliweka kitu cha ziada au aliweka uzuri wa asili ambao kila mwanamke anao hapa duniani.
Bahati mbaya ni wanawake wachache sana wanaweza kuuendeleza uzuri au muonekano ule hata kwa miaka mitano au kumi tu.
Wengi huingia kwenye mfumo wa maisha ambao unaanza kuharibu kabisa mionekano yao na wakati mwingine kuonekana wana umri mkubwa sana kuliko umri wao halisi.
                                                                       
       
Kimsingi mwanamke akijitunza vizuri ana uwezo wa kuonekana mbichi mpaka miaka 45 au 50 ambapo siku zake za mwezi zinasimama na hapo ndio ana haki ya kuanza kuonekana kwamba ameanza kubadilika sana lakini kabla ya hapo mwanamke anaweza kubaki katika hali hiyo hiyo ya muonekano mzuri kwa miaka mingi tu.
Leo naenda kuzungumzia mambo ambayo yanaweza kumchosha mwanamke na kuonekana mkubwa sana kabla ya umri wake.
kula vibaya; wanawake wengi huharibika kwa kula vyakula ambavyo sio vya kiafya kabisa hasa mikaango na vyakula vya haraka maarufu kama fast food, sukari na wanga mwingi.
vyakula hivi huwanenepesha sana, kuwapa vitambi mpaka wanapoteza kabisa ile shepu asilia ambayo walikua nayo hapo mwanzo.
lakini pia mwanamke anaweza kuchoka kwa kukosa chakula cha kutosha hasa kutokana na ugumu wa maisha.
kutofanya mazoezi; mazoezi yanachangia sana kumfanya mwanamke abaki na misuli iliyokaza na kutokua nyama uzembe kitaalamu kama muscle tone.
unaweza kua unakula vizuri na sio mnene lakini baadhi ya maeneo ya mwili wako yamejikunja kunja kama mzee sababu ya kukosa mazoezi kabisa.

kutumia vipodozi wasivyovifahamu; kuna vipodozi vingi sana sokoni ambavyo huwafanya wanawake wanaonekane warembo ndani ya muda mfupi sana lakini mara nyingi vipodozi vile hua na madhara ya muda mrefu ambayo wakati mwingine hayatoki.
ukikutana na mwanamke ambaye alijichubua miaka kumi iliyopita na baadae akaacha mara nyingi utaona kabisa ngozi yake imeungua na imeshindwa kurudi katika hali yake ya zamani, lakini pia vipodozi vya nywele vingine ni hatari na huunguza ngozi ya nywele.

msongo wa mawazo; katika karne hii ambayo dunia ina mambo mengi sana ambayo yanaleta msongo wa mawazo hasa ukosefu wa ajira na mahusiano mabovu ya kimapenzi basi wanawake wengi hutumia muda mwingi sana kuwaza mwisho wao.
Siku zote mtu akifika kwenye hali hii basi hawezi kula vizuri na kupata mahitaji yake muhimu na matokeo yake huonekana kabisa amechoka na kudhoofu.

kutoshiriki tendo la ndoa; tendo la ndoa kwa wanawake lina faida nyingi za kiurembo kama kufanya ngozi kung'aa sana kwani damu nyingi huenda kwenye ngozi wakati wa tendo la ndoa na kupeleka hewa ya oxgen na virutubisho vingine.
lakini pia wakati wa tendo la ndoa mwanamke anatoa homoni nyingi ikiwemo oxytocin na oestrogen ambazo ndio msingi mkuu unaomfanya mwanamke awe na shepu nzuri na ngozi laini kwanzia kuvunja ungo mpaka mwisho.
mwanamke asiyeshiriki tendo la ndoa hapati faida hizi.
ulevi na uvutaji wa sigara; siku hizi wanawake ni walevi sana kama wanaume, kimsingi pombe hupunguza maji mwilini kitaalamu kama deuresis na kuifanya ngozi kukosa maji na kua mbaya lakini pia sigara huweka kemikali kitaalamu kama nicotine kwenye ngozi.
Kemikali hii hufanya ngozi kua nyeusi na kupoteza muonekano wake wa awali.

magonjwa; ukiachana na magonjwa ya mwili kama saratani, ukimwi,sukari ambayo huchosha mwili kabisa baadhi ya magonjwa kama ugumba na magonjwa ya kizazi huathiri sana saikolojia ya wanawake.
Hali hii huwakondesha, kuwachosha na kuwazeesha kabisa.

kazi ngumu; miili ya wanawake haikuandaliwa kufanya kazi ngumu kama za wanaume, miili ya wanaume iliumbwa kwa ajili ya kazi ngumu hivyo sio kitu cha ajabu ila mwanamke akijikita kwenye kazi ngumu hupoteza kabisa muonekano wake wa awali na anaweza kuanza kuonekana kama mwanaume.                                                              
 Mwisho; wawake wengi hasa wa afrika huamini kwamba swala la muonekano mzuri ni bahati tu, wakisahau kua kwamba wao pia wanachangia kwa asilimia kubwa kua katiaka muonekano huo, mambo mengi ya urembo na muonekano yapo ndani ya uwezo wako ni swala la kuchukua hatua tu.

                                                                        STAY ALIVE

                                             DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                        0653095635/0769846183

TATIZO LA KONDO LA NYUMA KUSHINDWA KUTOKA BAADA YA KUJIFUNGUA(RATAINED PLACENTA)

Wanawake wengi huamini kwamba safari ya uzazi huisha pale mtoto anapozaliwa, kitu ambacho mara nyingi sio kweli na ukweli ni kwamba safari hii huisha pale kondo la nyuma linapokua limetoka lote kitaalamu kama third stage of labour.

retained placenta ni nini?
Hii ni hali ambayo kondo la nyuma linashindwa kutoka nje ya kizazi nusu saa baada ya kujifungua, ni hali hatari kwa mama kwani anaweza akavuja damu mpaka kifo.

nini chanzo cha kondo la nyuma kukataa kutoka?
kuna sababu mbalimbali za kondo la nyuma kukataa kutoka kama ifuatavyo..
uchungu kidogo; hii hutokea pale baada ya kujifungua mtoto  ambapo uchungu unakua mdogo sana na kondo la nyuma linashindwa kutoka lenyewe.
kukamatwa kwa kondo la nyuma; kondo la nyuma huweza kunaswa na kushindwa kutoka hata kama uchungu upo,mara nyingi husabishwa na kufunga kwa mlango wa uzazi.
kunasa kwenye kizazi; wakati mwingine kondo la nyuma hunasa kabisa kwenye misuli ya kizazi na mara nyingi husabishwa na historia ya kuzaa kwa upasuaji.

watu gani wako kwenye hatari ya kupata tatizo hili?

  • kuzaa baada ya umri wa miaka 30
  • kuzaa kabla ya miezi tisa ya mimba.
  • uchungu kuchukua muda mrefu
  • mtoto kufia tumboni.
  • historia ya kuzaa kwa upasuaji.
dalili za tatizo hili ni zipi kwa mama mjamzito?
  • homa kali
  • maumivu makali
  • harufu sehemu za siri
  • kuvuja damu nyingi
  • kutokwa na vipande vya nyama ukeni.
matibabu
Matibabu makubwa ya hali hii ni kuhakikisha kondo la nyuma linatoka kwa njia yeyote ile, njia zinazotumika hospitalini ni kuchoma sindano ya uchungu, kuingiza mkono kwenye uke na kuondoa kawaida, au kufanyiwa upasuaji mkubwa kama kondo limenasa kwenye kizazi na kuondoa kizazi.(accreta)

                                                       STAY ALIVE

                                     DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                  0653095635/0769846183

FAHAMU KWANINI MIHOGO NI SUMU KALI KWA BINADAMU.

Pamoja kwamba mihogo ni zao la tatu duniani kwa ajili ya chakula cha aina ya wanga huku likiwa na virutubisho vingine kama madini, vitamin A,B  na C lakini ni moja ya mazao hatari sana kwa binadamu.
Tarehe 10 mwezi wa tatu mwaka 2005 watoto 27 walifariki nchini ufilipino huku wengine 100 wakinusurika baada ya kula mihogo.
Watoto hao walikula mihogo ya kukaangwa wakati wa chakula cha asubuhi baada ya kununuliwa kwa mtu wa mtaani aliyekua anatembeza.
                                   
Wakati wa vita ya pili ya dunia wajapani wengi walikimbilia brazili kutafuta maisha mazuri, kutokana na ugumu wa maisha huko walipewa ardhi yenye ukame hivyo walipanda mihogo ili kuweza kuishi.
Historia inaonyesha ni watatu tu ndio waliobaki baada ya vita ya pili ya dunia kuisha baada ya kuishi kwa kutumia chakula hicho, wengi walikufa kwa sumu ya mihogo.

Sehemu zingine duniani ambazo watu hula mihogo kama afrika na sehemu zingine hua inatokea ghafla tu na kuua watu kadhaa na mara nyingi hapa Tanzania vifo husababishwa kwa kuliwa kwa majani ya mihogo maaruufu kama kisamvu.
Familia kadhaa nchini Tanzania zimewahi kufa kwa kula kisamvu tu ambacho pia hua na kemikali hiyo hasa kisipoiva vizuri.
Kwasasa baadhi ya serikali duniani kama japan zilishapiga marufuku matumizi ya mihogo na majani yake yote kama chakula.

nini chanzo cha sumu kwenye mihogo?
Mihogo ina kemikali moja kwa jina ya linamarin, mara nyingi muhogo ukiliwa mbichi kemikali hii hubadilishwa kwenye tumbo la binadamu na kua sumu kwa jina la cyanide.
Hizi ni moja ya sumu hatari zaidi duniani ambayo inaua ndani ya sekunde chache sana.
Kitaalamu ni kipande kidogo tu cha muhogo kina dozi ya kutosha kumuondoa mtu.


unaweza kuutambua muhogo wenye sumu?
Sio rahisi kuutambua, japokua tafiti zinaonyesha muhogo mchungu una sumu zaidi kuliko ule mtamu.

Pamoja na mbinu mbali mbali za kuloeka mihogo na kupunguza sumu zake bado wataalamu wana amini mihogo ina sumu zingine ambazo hata kama hazikuui basi zinakuumiza taratibu kwenye mfumo wa ubongo, maini na figo ndio maana baadhi ya nchu duniani ziliamua kupiga marufuku zao hilo kwani kuna vyakula vingi mbadala kama wali, ugali, viazi na ngano.

                                                                     STAY ALIVE

                                                     DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                             0769846183/0653095635

HII NDIO SABABU MAFUTA YA MZAITUNI NI BORA KIFYA.(OLIVE OIL)

Mafuta ya mzaituni ni mafuta ambayo kitaalamu huitwa monosaturated yaani hua kwenye mfumo wa kimiminika kwenye joto la kawaida na huaminika kua na faida za kiafya sana mwilini.
                                                                    

Ukiacha  kutumia mafuta ambayo huitwa saturated au ambayo yanakua mgando wakati wa hali ya hewa ya kawaida na kuanza kutumia mafuta ya haya ya mzaituni basi afya yako itapata faida zaidi.

Mafuta ya mzaituni hupunguza sana hatari ya kuugua magonjwa ya moyo kwani yameonyesha kupunguza sana kiasi cha lehemu au cholestrol mwilini ambayo ndio moja ya chanzo kikuu cha ugonjwa wa moyo.

Tafiti zingine zimeonyesha kwamba mafuta haya yana uwezo wa kupunguza kiwango cha sukari mwilini hivyo ni faida sana kwa watu wenye hatari sana ya kupata magonjwa ya kisukari, lakini pamoja na faida zake hizo hutakiwi kutumia mengi kwani yana nguvu au calories nyingi ambazo huweza kukunenepesha.

siku zote chagua mafuta ambayo yako kwenye mfumo wa kimiminika badala ya mafuta ambayo yako kwenye mfumo wa mgando.
lakini pia kumbuka huwezi kuvifanya vyakula ambavyo sio vizuri kwa afya hasa vyakula vya kukaangwa sana eti kwasababu umeongezea  au umetumi mafuta haya kuandaa vyakula hivyo.

                                                               STAY ALIVE

                                        DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                       0653095635/0769846183

FAHAMU AINA ZA VIRUSI VYA UKIMWI NA TOFAUTI ZA MAKALI YAKE MWILINI.

Unaweza kushangaa mtu anapata ukimwi leo lakini anakufa baada ya mwaka mmoja au miwili pamoja na kufuata masharti yote na kutumia dawa zote kwa uaminifu.
Hii ni kwasababu virusi vya ukimwi havifanani, kuna ambavyo vikikupata vinakushambulia na kusambaa kwa kasi lakini vingine haviwezi.

je kuna aina ngapi ya virusi vya ukimwi?
Kuna aina mbili za virusi vya ukimwi kwa jina la HIV-1 na HIV-2 vyote husababisha maambukizi ya ukimwi lakini hutofautiana.
HIV-1 ndio aina ya virusi ambavyo vinapatikana zaidi, zaidi ya asilimia tisini ya wagonjwa wameathirika na virusi hivi,ni vikali sana, vinaambukizwa kirahisi, huchukua muda mfupi kutoka kwenye HIV kwenda kwenye AIDS na vimeua watu wengi sana duniani, yaani kwa haraka haraka ukisikia mtu ni mgonjwa wa ukimwi basi uwezekano mkubwa yuko na hivi.
Virusi hivi vina makundi manne yaani M,N,O na P lakini pia vikundi hivi vimegawanyika katika vikundi vingine vidogo vidogo zaidi na mara nyingi daktari anaweza kukutibu vizuri kama akijua ni aina gani ya hivyo vikundi vidogo vidogo unavyo kwani baadhi ya vikundi havisikii kabisa dawa fulani na vingine vinasikia, na bahati mbaya ni nchi zilizoendelea tu  ndio zina uwezo wa kutambua iana ya ukimwi ulionao.

HIV-2 ni aina ya virusi ambavyo vinashambulia watu wachache sana, mara nyingi hupatikana maeneo ya ya afrika magharibi.
Virusi hivi sio vikali, ni ngumu kumuambukiza mtu na huchukua muda mrefu sana kumfanya mtu awe hoi kitandani kwani hata kasi yake ya kusambaa ni ndogo.
Virusi hivi pia vinakua na na magroup yake makubwa na madogo madogo.

je unaweza kuathirika na aina zote mbili?
Ndio mgonjwa wa ukimwi anaweza kupata iana zote mbili za ukimwi au aina moja na magroup yake mengine kitaalamu kama HIV superinfection, na mara nyingi hatari ya maambukizi haya iko kwenye miezi michache ya kwanza baada ya kuambukizwa aina fulani ya virusi vya ukimwi.
Mara nyingi wagonjwa wenye virusi vya aina zote mbili huugua na kufa baada ya muda mfupi hata kama wakipewa dawa kwani dawa nyingi hukataa kuwatibu.

Kwanini wagonjwa wa ukimwi hushauriwa kuendelea kutumia condom?
Unaweza ukapata ukimwi kwa mara ya kwanza na kupata aina fulani ya virusi ambavyo vinatibika kirahisi ukitumia dawa.
Lakini ukiendelea kulala na watu bila kinga basi unaweza ukapata virusi vingine na vingine kiasi kwamba hata dawa ulizopewa mwanzoni zikashindwa kukusaidia.

                                                         
                                                          STAY ALIVE
                                           

                                        DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                               0653095635/0769846183

TATIZO LA MTOTO KUNYONYA KIDOLE NA MATIBABU YAKE.

Kunyonya kitu chochote wakati wa kuzaliwa ni tabia ya kawaida kwa mtoto, na kama mtoto akizaliwa hawezi kunyonya basi ujue kuna tatizo sehemu.
watoto wengine huanza kunyonya vidole wakiwa tumboni mwa mama zao kabla hata ya kuzaliwa na hii ni kawaida kabisa na wakishazaliwa hupenda kunyonya vidole vyao kabla ya kwenda kulala kwani huwafanya wajisikie vizuri.

Ni umri gani mtoto anatakiwa aache kunyonya vidole?
Mtoto anatakiwa aache kujinyonya vidole alifika umri wa miezi 6 mpaka 7 na wakati mwingine mpaka miaka mitatu, lakini akiendelea kujinyonya baada ya miaka mitatu basi kuna hatari ya kuendelea kupata minyoo mara kwa mara ambayo huweza kuleta upungufu wa damu, na kuharibu mpangilio wa meno yake mpaka ukubwani.

mambo gani huweza kusaidia kuacha kunyonya vidole?
mpe zawadi; wazazi wengi hupenda kutumia adhabu kumbadilisha tabia mtoto kitaalamu kama negative reinforcement lakini unaweza kutumia njia tofauti au positive reinforcement kwa kuwapa zawadi pale wanapofanikiwa kuepuka makosa fulani.
mfano unaweza kumpa zawadi ya shilingi 200 akimaliza siku nzima bila kunyonya kidole badala ya kumchapa viboko.
weka tiki kwenye kalenda kwenye siku ambazo hakunyonya vidole na hii itampa nguvu sana.
angalia mambo yanayosababisha anyonye kidole; mara nyingi watoto hunyonya vidole wakiwa na msongo wa mawazo au wakikosa amani kwa muda fulani.
ukiliona hilo basi mkumbatie mtoto wako na kaa naye karibu au jaribu kutatua changamoto yake.
mkumbushe kiutaratibu; muonyeshe tu kwamba hupendezwi na tabia yake kwa sauti ya upole bila kufoka, binadamu ana asili ya kupingana na sheria hasa ukitumia nguvu sana kumzuia, ukimpa uhuru inakua rahisi yeye kuachana na tabia fulani.
vipi kama njia zote zikikwama?: usiwe na wasiwasi, haraka wala usitumie nguvu kubwa, endelea tu na utaratibu huo na mwishowe utafanikiwa tu kumrekebisha.

                                                                         STAY ALIVE

                                              DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                             0769846183/0653095635  
                                                          

makundi 8 ya watu wasioruhusiwa kunywa dawa za kuongeza nguvu za kiume.

Huenda umesikia mara kwa mara kwamba kuna mwanaume amefia chumba cha kulala wageni baada au kabla ya kushiriki tendo la ndoa na huenda hujawahi kufuatilia ili kujua chanzo ramsi cha kifo hicho ni nini.
 Naomba nikwambie kwamba moja ya sababu ya kufia chumba cha wageni ni matumizi ya dawa hizi za viagra kiholela bila kujua kama afya yako inaruhusu matumizi ya dawa hii.
                                                                     
Leo ntaenda kuzungumzi makundi ya watu ambao hawaruhusiwi kutumia dawa hizi kama ifuatavyo.
wagonjwa wa moyo; wagonjwa wengi wa moyo hawaruhusiwi hata kushiriki tendo la ndoa kutokana na uwezo wao mdogo wa kuhimili mazoezi lakini pia dawa ya viagra inafanya kazi kwa kusukuma damu nyingi kwenda sehemu za siri na kupanua mishipa ya damu kitu ambacho hakiwezi kuvumilika kwa wagonjwa hawa.
Mshtuko wa moyo, kusimama kwa moyo na vifo vya ghafla vimeripotiwa sana sababu ya matumizi ya dawa hii ya viagra kwa wagonjwa wa moyo.
wagonjwa wa presha ya kushuka: dawa ya viagra ilitengenezwa mwanzoni kabisa kwa ajili ya kushusha presha ya kupanda lakini baadae ikaonekana kwamba madhara yake ni kuongeza nguvu za kiume hivyo ikabidi iondolewe kwenye dawa za presha.
Hivyo kama wewe presha yako ina tabia ya kushuka basi dawa hii inaweza kukushusha mpaka presha ya sifuri na huo ndio ukawa mwisho wako.
wanaotumia dawa za presha ya kupanda;  hawa wagonjwa hutumia dawa za kushusha presha kila siku, sasa kama nilivyosema hapo juu.
viagra pia inatabia ya kushusha presha hivyo kama ukiamua kuimeza basi dawa zako za presha ni vizuri usizimeze kwani presha itashuka sana na kuhatarisha maisha yako.
wagonjwa wa macho; kama una tatizo lolote la macho ukatumia dawa hii ukaona giza ghafla basi achana nayo kwani hiyo ni kengere ya hatari na unatakiwa uwahi hospitali kuonana na daktari kwani ukiendelea kutumia itakumaliza macho kabisa.
wagonjwa wa siko seli; moja ya matatizo ya siko seli ni kuzuia damu kwenye uume na kushindwa kutoka kitaalamu kama priapism.
Tatizo hili ni kubwa na huweza kusababisha kufanyika kwa upasuaji, sasa mgonjwa wa siko seli akimeza dawa hii anaongeza hatari ya kushikwa na hali hiyo kwa maana nyingine dawa hii sio salama kwake, wagonjwa wa saratani ya damu pia wana hatari hii.
wagonjwa wa chembe ya moyo;  huu ugonjwa kwa kitaalamu unaitwa angina pectoris, ni maumivu ya misuli ya moyo pale moyo unapokosa hewa ya kutosha sababu ya mishipa inayopeleka damu kwenye moyo kuzibwa na mafuta au kukakamaa.
sasa wagonjwa hawa mara nyingi hupewa dawa zinaizwa isosorbide mononitrate or dinatrate, dawa hizi hupanua mishipa ya damu na kuwafanya wapate nafuu huku dawa hizo zikishusha presha kama moja ya madhara yake, hivyo zikitumika na viagra ambayo kazi yake ni kushusha presha pia huweza kumuua mgonjwa.
wanawake; kuna watu hufikiri dawa za viagra zinaweza kuwasaidia wanawake kupata hamu ya tendo la ndoa, kitu hicho sio kweli na hakuna utafiti ulionyesha kitu kama hicho.
matumizi ya dawa hii kwa wanawake haina faida yeyote zaidi ya kushusha presha bure.
kuchanganya na baadhi ya dawa; dawa ya viagra ikishafanya kazi mwilini inaondolewa na maini kwa kutumia enzyme moja inayoitwa cytchrome p450, sasa baadhi ya dawa kama erythromycin, ritonavir na cimetidine hufanya kazi kwa kuzuia enzyme hiyo na kinachotokea ni kwamba viagra haitoki mwilini na inazidi kua nyingi kwenye mfumo wa damu,
Hivyo kua makini usitumie dawa hizi na pamoja na viagra.
MWISHO: viagra ni dawa hatari sana na inatakiwa itolewe kwa kibali maalumu cha daktari pale anaothibitisha kweli hakuna mazingira yeyote yanaweza kuhatarisha afya yako wa matumizi ya dawa hizo.

                                                                       STAY ALIVE
                                             DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                          0653095635/0769846183

FAHAMU KWANINI MWILI WA BINADAMU UNAELEA BAADA YA KIFO.

Katika hali ya kawaida binadamu akiwa hai anakua ni mwepesi kuliko maji hivyo hawezi kuzama chini ya maji akiwa bado anapumua, naomba hilo lieleweke vizuri.
Misuli ni mizito kidogo kuliko maji, mifupa ni mizito kidogo kuliko maji, mafuta ni mepesi kuliko maji lakini pia mapafu ya binadamu ya hewa ambayo yanamfanya binadamu awe kama boya la kuogelea.

binadamu akifa inakuwaje?
Sasa binadamu akifia kwenye maji, basi maji mengi yataingia kwenye mapafu na kuupoteza ule uwezo wa binadamu kuelea yaani atakua mzito kuliko maji na matakeo yake atazama chini ya maji kwa muda.
baada ya masaa kadhaa binadamu huyo ataanza kuharibika, wakati wakuharibika binadamu hutoa hewa nyingi ambayo hutokana na kazi ya bacteria wanaomshambulia.
Hewa ile itajaa sehemu mbalimbali za mwili wake na kumfanya avimbe, sasa hapo ndio atakua mwepesi tena kama boya, kama alivyokua mwanzo kabla ya kufa hivyo mwili utarudi juu na kuelea.

mwili unachukua masaa mangapi mpaka kuelea?
kutokana na hali ya hewa ya eneo husika, sehemu yenye joto mwili unaharibika haraka hivyo utaelea ndani ya masaa 24, lakini sehemu yenye baridi kali sana ambapo kuoza kunachelewa basi mwili unaweza kukaa chini hata wiki kadhaa bila kuelea.

                                            DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                   0653095635/0769846183

                                                           STAY ALIVE.

JINSI YA KUJUA KAMA MTU ALIKUFA MAJI AU ALIUAWA NA KUTUPWA MAJINI.

Mtu anaweza ukamuua mtu kisha akamtupa kwenye maji ali aonekane amekufa maji, kama mtu huyo hakua na vidonda vya kupigwa ni ngumu sana kujua kama mtu huyu alikufa kwa kuzama kwenye maji au aliuawa kwanza kisha akatupwa kwenye maji.
                                                             
nini hufanyika kutambua mtu aliuawa kisha kutupwa kwenye maji?
Mtu akifa kwa kuzama kwenye majini, kwanza anavuta kiasi kikubwa sana cha maji ambacho kinaingia mapafuni na kuyafanya yapanuke na kuongezeka uzito.
Lakini mtu akitupwa kwenye maji baada ya kufa hawezi kuvuta tena hewa, kiasi kidogo cha maji kitaingia mapafuni.
Hivyo ukifungua kifua cha marehemu kisha ukakata kiasi cha mapafu na kukiweka kwenye ndoo ya maji basi kitazama kama marehemu alikufa maji ila kama marehemu alikufa kisha akatupwa kwenye maji, kipande hicho cha pafu kitaelea juu ya maji.

                                                                   STAY ALIVE