data:post.body KWA MARA YA KWANZA MWANAMKE ALIYEWEKEWA KIZAZI CHA MAMA ALIYEFARIKI AJIFUNGUA ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

KWA MARA YA KWANZA MWANAMKE ALIYEWEKEWA KIZAZI CHA MAMA ALIYEFARIKI AJIFUNGUA

Huko nchini brazili katikati ya jiji la sao paul yametokea maajabu makubwa katika mapinduzi ya  sayansi kwa mara ya kwanza kabisa duniani.
                                                                   
katika majaribio 39 ambayo yameshawahi kufanyika ya kuchukua vizazi vya wanawake walioko hai na kuvipandikiza kwa wanawake wengine ambao wana matatizo ya uzazi, ni watoto 11 tu ambao walipatikana huku wengine 28 waliowekewa vizazi wakishindwa kabisa kupata watoto kwa mimba kushindwa kuingia kabisa au mimba kuharibika.
lakini pia kumekua na utafiti ambao wanawake 10 waliwekewa vizazi vya watu ambao ni wafu lakini wote hawakufanikiwa kupata watoto.
leo hii huko nchini brazili mtoto wa kwanza amezaliwa baada ya kizazi cha mwanamke ambaye alikua amefariki kupandikizwa kwa mwanamke mwingine.

kazi ilifanyika vipi?
mama mmoja mwenye umri wa miaka 40 ambaye alikua na watoto watatu alifariki baada ya kuvuja damu kwenye ubongo wake, ndani ya muda mfupi viungo vyake ikiwemo mfuko wa uzazi vilihifadhiwa,
mwanamke ambaye alizaliwa na tatizo la kizazi chake kushindwa kuumbika vizuri tangu utotoni alifanyiwa upasuaji na kuwekewa kizazi hichi cha mama mfu.
baadae mayai  ya mwanamke huyu mzima yalichukuliwa na kuchanganywa na mbegu za mme wake huko maabara kisha kuhifadhiwa vizuri.
baada ya wiki sita mwanamke huyu alianza kupata hedhi kama kawaida na alipofika wiki ya saba yai lake ambalo lilihifadhiwa, likiwa limeritubishwa tayari liliwekwa ndani ya kizazi chake.

matokeo
baada ya miezi tisa ya mimba kama kawaida, mtoto wa kike mwenye kilo mbili na nusu alizaliwa kwa upasuaji akiwa hai.
haya ni maendeleo mkubwa sana kwani katika viungo ambavyo ni ngumu kupata ni kizazi hasa kutoka kwa watu ambao wako hai.

                                                                 STAY ALIVE
                                        DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                          
                                                    O769846183/0653095635

0 maoni:

Chapisha Maoni