data:post.body HAWA NDIO MAPACHA WASIOWEZA KUAMBUKIZWA UKIMWI, WANAOTENGENEZWA CHINA. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HAWA NDIO MAPACHA WASIOWEZA KUAMBUKIZWA UKIMWI, WANAOTENGENEZWA CHINA.

CRISPR ni nini?
hili ni neno la kibailogia linalomaanisha uwezo wa kubadili vinasasaba au gene ya viumbe hai vya aina yoyote kwa ajili ya lengo fulani la faida za kimaisha.
                                                                     
CRISPR iligunduliwa nchini marekani mwaka 2012 na mtaalamu wa bailojia profesa Jennifer Doudna ambaye alikua akifanya tafiti ya jinsi ambavyo bacteria wanaweza kujikinga na kushambukiwa na virusi.

nini kimetokea china?
Baada ya wataalamu hawa kuitangaza teknolojia hii, nchi nyingi duniani zimekua zikiitumia teknolojia hii kubadili vinasasaba vya wanyama na mimea mbalimbali kwa ajili ya kupata ubora mkubwa zaidi kuliko ule wa mwanzo.
Sasa huko nchini china wataalamu kwa mara ya kwanza wamefanya kitu hicho kwa mapacha ambao bado hawajazaliwa.

mtaalamu huyo kutoka china ameondoa vinasasaba kwa jina la CCR5 ambavyo hutumika na virusi vya ukimwi kama njia ya kuingia kwenye seli nyeupe za damu na kuushambulia mwili.
Kwa maana nyingine hata virusi vikiingia ndani ya mtu, vitashindwa kuingia ndani ya seli za damu kwa ajili ya kuushambulia mwili hivyo baada ya muda vitakufa kwa kukosa virutubisho.
hivyo tunategenegemea kwa mara ya kwanza kabisa kuzaliwa kwa binadamu ambao hawawezi kupata ukimwi kwa njia yeyote ile.
mpaka sasa hivi kuna wazazi zaidi wameshajitolea kubeba mimba kwajili ya utafiti huu.

kwanini dunia inampinga?
wataalamu mbalimbali duniani wamepinga sana teknolojia hii kutumika kwa binadamu kwani inaenda kinyume na makubaliano ya umoja wa mataifa ambayo hayaruhusu vinasasaba vya binadamu kuchezewa kwa aina yeyeote ile ili kutunza kizazi cha binadamu halisi.
Dunia ina hofu kwamba yeknolojia hii itaondoa usawa wa kibinadamu.
watu watakua wana uwezo wa kuamua kuzaa mtoto wa urefu wanaotaka, mwili wanaotaka, na rangi wanayotaka.
Mwisho wa siku hata magonjwa ya aina fulani yatakua hayawahusu binadamu wengine.
Hii italeta aina mpya ya binadamu ambao hawajawahi kutokea na wengine watatumika vitani kama silaha kwa nchi zilizoendelea.
Teknolojia hii italeta watu wakubwa au giants ambao siku za usoni wanaweza wakatubadilikia wakaangamiza vizazi halisi vya binadamu.
Historia ya dunia kibiblia inaonyesha kwamba waliwahi kutokea binadamu wakubwa sana ambao walileta shida sana duniani lakini baadae waliangamizwa wakati wa nuhu na inasemekana mpaka leo kuna mabaki ya binadamu waliowahi kua wakubwa sana.

                                
nini faida ya teknolojia hii?
Teknolojia hii ikitumika vizuri inaweza kuondoa magonjwa yote ya kurithi kwenye ukoo, magonjwa ya saratani, kuzuia unene, na magonjwa yote ambaukizi ambayo yamekosa dawa, kwani wanasayansi watakua na uwezo wa kutengeneza binadamu imara yaani kama ku update version za binadamu mpya.
tatizo ni kwamba, teknolojia hii haitaweza kudhibitiwa na itaweza kuleta maafa makubwa duniani au kuleta magonjwa mapya ambayo yalikua yanazuiliwa na vinasasaba ambavyo tunaviondoa sasa hivi.


                                                                STAY ALIVE 

                                       DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                   0653095635/0769846183

0 maoni:

Chapisha Maoni