Kuoza meno ni nini?
hili ni tatizo ambalo husababishwa na bacteria kujificha ndani ya sehemu za meno kisha kumwaga tindikali ambayo huenda kuondoa madini ambayo yapo kwenye meno na kufanya meno kuanza kupungua ukubwa na kutoboka.
kitaalamu bacteria ambao wanaishi kwa kula sukari au wanga mdomoni ndio hutengeneza tindikali ambayo huharibu meno.
mdomoni mwa binadamu kuna kiwango cha tindikali{pH] kwanzia 6.2 mpaka 7 ambayo huongezeka pale mtu anapoanza kutumia sukari, soda, biskuti, chocolate au vyakula vya wanga kwani bacteria huanza kazi ya kutengeneza tindikali kila unapokula milo hiyo.
kiwango cha tindikali kikiwa kingi sana mdomoni basi tindikali huanza kutoboa matundu kwenye meno na hapo ndio chanzo cha meno kuanza kuharibika.
kama tatizo hili lisipowahiwa basi jino litashambuliwa mpaka kwenye mzizi na kitakacho baki itakua kuling'oa tu.
watu gani wako kwenye hatari ya kuharibika meno?
,
hili ni tatizo ambalo husababishwa na bacteria kujificha ndani ya sehemu za meno kisha kumwaga tindikali ambayo huenda kuondoa madini ambayo yapo kwenye meno na kufanya meno kuanza kupungua ukubwa na kutoboka.
kitaalamu bacteria ambao wanaishi kwa kula sukari au wanga mdomoni ndio hutengeneza tindikali ambayo huharibu meno.
mdomoni mwa binadamu kuna kiwango cha tindikali{pH] kwanzia 6.2 mpaka 7 ambayo huongezeka pale mtu anapoanza kutumia sukari, soda, biskuti, chocolate au vyakula vya wanga kwani bacteria huanza kazi ya kutengeneza tindikali kila unapokula milo hiyo.
kiwango cha tindikali kikiwa kingi sana mdomoni basi tindikali huanza kutoboa matundu kwenye meno na hapo ndio chanzo cha meno kuanza kuharibika.
kama tatizo hili lisipowahiwa basi jino litashambuliwa mpaka kwenye mzizi na kitakacho baki itakua kuling'oa tu.
watu gani wako kwenye hatari ya kuharibika meno?
- ulaji wa vyakula vya wanga
- ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi.
- kutopiga mswaki kwa wakati.
- kurithi kwa wazazi.
dalili za ugonjwa huu ni kama ifuatavyo...
- hatua ya kwanza ya ugonjwa; meno yanakua yametoboka kidogo sana na hapa hua hakuna dalili kabisa ambayo mgonjwa ataisikia.
- hatua ya pili ya ugonjwa; hapa meno yanakua yametoboka zaidi na mgonjwa huanza kusikia dalili za maumivu kwa mbali sana hasa akila vyakula vyenye sukari sana.
- hatua ya tatu ya ugonjwa; meno yanatoboka zaidi na kipindi hiki maumivu hua makali mgonjwa akila chakula cha moto sana au cha baridi sana.
- hatua ya nne ya ugonjwa; jino kwa sasa limetoboka sana na maumivu hua ni makali mno kiasi kwamba ikifika usiku mtu hawezi kulala na hata akimeza dawa za maumivu hizi ndogo ndogo bado maumivu hayaishi.
- hatua ya tano ya ugonjwa; hii ni hatua ambayo jino limekua limechimbika sana na kuleta jipu sehemu ya eneo la jino, maumivu ni makali sana na homa huwa juu.
matibabu
matibabu ya meno hutegemea sana hatua ya kuharibika ambayo meno yamefikia kama ifuatavyo.
hatua ya kwanza na ya pili; haihitaji matibabu lakini mgonjwa anashauriwa kuacha kutumia vyakula vyenye sukari na wanga sana kisha hushauriwa kupiga mswaki kila baada ya mlo ili kuonoda mabaki ya vyakula mdomoni.
hatua ya tatu; hii ni hatua ambayo jino limetoboka na na maumivu yanakua makali kwa kunywa maji ya baridi ya ya moto sana.
huu ni muda muafaka wa kuziba jino hili.
hatua ya nne; hii ni hatua ambayo maumivu ni makali sana hasa usiku na mgonjwa kushindwa kulala kitaalamu kama pulpitis.
matibabu pekee ni kuondoa sehemu ya ndani ya jino iliyoharibika kisha kuijaza kitaalamu kama root canal, lakini sababu sehemu nyingi hawafanyi matibabu haya ya root canal wengi huishia kung'olewa jino.
hatua ya tano; hii ni hatua ambayo mtu anapata jipu la kwenye jino, matibabu yanayohusika hapa ni kuliodoa jino na kufanya upasuaji mdogo kuondoa usaa.
jinsi ya kuzuia kuharibika kwa meno.
hatua ya kwanza na ya pili; haihitaji matibabu lakini mgonjwa anashauriwa kuacha kutumia vyakula vyenye sukari na wanga sana kisha hushauriwa kupiga mswaki kila baada ya mlo ili kuonoda mabaki ya vyakula mdomoni.
hatua ya tatu; hii ni hatua ambayo jino limetoboka na na maumivu yanakua makali kwa kunywa maji ya baridi ya ya moto sana.
huu ni muda muafaka wa kuziba jino hili.
hatua ya nne; hii ni hatua ambayo maumivu ni makali sana hasa usiku na mgonjwa kushindwa kulala kitaalamu kama pulpitis.
matibabu pekee ni kuondoa sehemu ya ndani ya jino iliyoharibika kisha kuijaza kitaalamu kama root canal, lakini sababu sehemu nyingi hawafanyi matibabu haya ya root canal wengi huishia kung'olewa jino.
hatua ya tano; hii ni hatua ambayo mtu anapata jipu la kwenye jino, matibabu yanayohusika hapa ni kuliodoa jino na kufanya upasuaji mdogo kuondoa usaa.
jinsi ya kuzuia kuharibika kwa meno.
- punguza ulaji wa sukari na vyakula vya wanga.
- piga mwaki kila baada ya mlo.
- muone daktari wa meno akuchunguze angalau mara nne kwa mwaka.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0753095635/0769846183
0753095635/0769846183
,
very helpfull.. asante
JibuFutawelcome
Futa