data:post.body TAFITI MPYA:KUNYWA MAJI YA BARIDI SANA KUNASAIDIA KUPUNGUZA UZITO NA KITAMBI. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

TAFITI MPYA:KUNYWA MAJI YA BARIDI SANA KUNASAIDIA KUPUNGUZA UZITO NA KITAMBI.

Ni wazi kwamba watu wengi sana wanafahamu kwamba kunywa maji ya uvuguvugu hasa wakati wa asubuhi kunasaidia sana kupunguza uzito kwa kuongeza joto la mwili na kuongeza kasi ya uchomaji wa mafuta mwilini.
                                                               
na hii njia imekua ikitumika kwa miaka mingi sana na baadhi ya watu wamekua wakiongeza na limao ili kupata matokeo zaidi.
lakini pia watu walikua wakiyaogopa maji ya baridi sana kwa kuamini kwamba yanagandisha mafuta tumboni na kuongeza kitambi.
lakini tafiti mpya hivi karibuni zimeonyesha tofauti na watu walivyokua wanafikiria mwanzo.

tafiti mpya zinasemaje?
maji ya baridi sana au yenye barafu kabisa yanasaidia kupunguza uzito zaidi kwani maji yakiingia tumboni yakiwa ya baridi sana, mwili unalazimika kutumia nguvu za ziada kuyachemsha yawe katika kiwango kinachohitajika na mwili kabla ya kuanza kuyatumia.
sio kwamba maji ya uvuguvugu hayasaidii tena lakini tafiti zinaonyesha maji ya baridi sana ni bora zaidi kuliko ya uvuguvugu.
lakini pia tafiti hizo zinaongeza kwamba sio kwenye kunywa tu lakini hata utafiti uliofanyika kwa watu wanao ogelea kwenye maji ya baridi sana huweza kupungua uzito haraka kutokana na njia hiyo hiyo.

nini cha kufanya?
hii ni habari njema hasa kwa watu ambao wanashi maeneo ya joto, kwani walikua wakilia sana kunywa maji ya uvuguvugu kipindi cha joto kali.
sasa hivi wanaweza kunywa maji ya baridi sana bila wasiwasi wa kuhisi kwamba watanenepa zaidi.

                                                                     STAY ALIVE

                                          DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                          0769846183/0653095635  

Maoni 2 :