data:post.body HIZI NDIO SABABU ZINAZOPELEKEA MWANAUME KUA SHOGA. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIZI NDIO SABABU ZINAZOPELEKEA MWANAUME KUA SHOGA.

Swala la ushoga limeleta mijadiliano mikali sana kwenye nchi mbalimbali huku nchi zingine zikiwaunga mkono mashoga, wakati huo huo nchi zenye misimamo mikali ya kidini zikiwapa adhabu kali za vifungo vya gerezani.
                                                                 
mashoga hupingwa sana na dini mbalimbali za kikikristo na kiislam, dini hizo zikidai kwamba wanachokifanya ni chukizo mbele za mungu na wataishia motoni.
lakini pia mashoga hupingwa sana na kwenye nchi za afrika ambazo zina maadili yao amabyao hayaamini kwenye ushoga tofauti na nchi zilizoendelea ambazo ubaguzi wa mashoga hauna nguvu sana.
baadhi ya nchi zilizoendelea mashoga ni kundi maaalumu ambalo hupewa vipaumbele hata kwenye ufadhili wa kusoma vyuo vikuu.

msimamo wa kitaalamu kuhusu mashoga ukoje?
kitengo cha madaktari wa akili huko nchini marekani kinachofahamika kama THE AMERICAN PSYCHIATRIC  ASSOCIATION ilikua ikiwatambua mashoga wote au watu wote wenye mahusiano na jinsia moja kama wagonjwa wa akili.
lakini mwaka 1970 kitengo hichi kiliacha kuwatambua watu hawa kama wagonjwa wa akili sababu waliweza kuendelea na shughuli zao za kikazi kama kawaida kama watu wengine bila msaada wowote hivyo waliona hakuna haja ya kuwatambua watu hawa kama wagonjwa wa akili.
lakini bado swali linakuja, je kwanini mtu anaamua kua shoga? tafiti mbalimbali zilizofanyika zilikuja na majibu yafuatayo.
Genetics; mwaka 1990 utafiti ulifanyika na ambao ulikuja na majibu kwamba chromosome X ambayo inatoka kwa mama kwenda kwa mtoto wa kiume hua inakua imebeba vinasasaba tofauti tofauti ambavyo vinaweza kumfanya mtoto huyu wa kiume akawa shoga.
tafiti hii iligundua kuwepo kwa vinasasaba hivi kwenye asilimia hamsini mpaka sitini ya mashoga waliofanyiwa utafiti.
sababu kibailojia;  tafiti zingingine mpya zinasema kwamba kuna mabadiliko ya homoni ambayo yanatokea kwenye mfuko wa uzazi wa mama kabla mtoto hajazaliwa.
mabadiliko haya huathiri ubongo wa mtoto kwa njia ambayo haijafahamika na kumfanya atoke akiwa na tabia hizi za kushiriki mapenzi ya jinsia moja.
kitaalamu mwanaume akiwa kwenye mfuko wa uzazi anakua na vinasasaba vya kiume yaani XY lakini anakua na maumbile ya kike mpaka wiki sita ambapo homoni za kiume huingilia kati na kuanza kumtengenezea maumbile ya kiume, lakini homoni hii ikipata shida kidogo mtu anaweza akatoka na maumbile ya kiume lakini hajakamikika.
ushahidi kwamba mwanaume alikuwa mwanamke kabla ni uwepo wa matiti kwa mwanaume ambayo hayana kazi, na kufanana sana kwa kazi kati ya kinembe na uume.
mazingira; baadhi ya tafiti zinaamini kwamba mazingira ambayo mtoto anakuziwa yanaweza kumfanya awe shoga.
yaani kutunzwa na mama muda mwingi na kua na baba mkali ambaye hana muda na mtoto, kuishi na dada zake tu bila kuwepo watoto wengine wa kiume, kuanza kuingiliwa kinyume na maumbile akiwa mtoto mdogo, kuona swala la ushoga kwenye TV na kulichukulia kawaida, kutokemewa kwa tabia za kishoga akiaanza kuzionyesha utotoni na  umaskini wa kipato.
lakini pia baadhi ya watu hua mashoga sababu ya kuiga mambo au kujaribu kila kitu ujanani.
kuna watu ambao ukiwaona mtaani hawana dalili hata moja ya ushoga kimuonekano lakini ni mashoga.
mfano ukiangalia soko la mitindo au modeling Tanzania lina watu wengi sana wa mapenzi ya  jinsia moja ambao kwa hali ya kawiada ni rahisi kujua kwamba hawa watu wanafanya mambo haya kama kwa kuigana au kulazimika kufanya hivyo sababu ya shida sio kwamba walizaliwa hivo.
lakini pia baadhi ya tafiti zilikuja kupinga hoja kwamba watoto waliozaliwa kwenye mazingira ya kishoga hua mashoga kwani kuna watu wengi ambao wamelelewa na wapenzi wa jinsia moja lakini wakakua na kutojihusisha na mambo hayo ya ushoga na pia kuna wazazi ambao wamezaa watoto mashoga japokua wao sio jinsia moja.
baadhi ya mashoga walihojiwa wanasema kwamba wao walizaliwa wa kiume japokua moyoni walijihisi wa kike.
walipambana sana ili wasiingie kwenye tabia hiyo ya jinsia moja kwa kutafuta wapenzi wa kike na hata kujaribu kushiriki tendo la ndoa na wanawake lakini hawakupata hisia zozote huko na baadae walaiamua kukubaliana na hali zao za jinsia moja.
mwisho; wataalamu wanaamini kwamba asilimia kubwa ya watu ambao ni mashoga hawakua vile kwa kuamua lakini kwa kuwepo kwa sababu mbalimbali za kibailojia, mabadiliko ya homoni, na mazingira waliyokulia.
japokua baadhi ya tabia za kishoga kwa baadhi ya mashoga zingeweza kuzuiliwa kwa kuzikemea tabia hizi, hasa zinazosababishwa na mazingira.

                                                               STAY ALIVE...

                                    DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                  0769846183/0653095635

0 maoni:

Chapisha Maoni