data:post.body HIZI NDIO NJIA ZINAZOTUMIKA KUBADILI JINSIA (TRANSGENDER) ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIZI NDIO NJIA ZINAZOTUMIKA KUBADILI JINSIA (TRANSGENDER)

Watu wengi duniani ambao ni wa jinsia fulani hua wanahisi kwamba walizaliwa na jinsia ile kimakosa hivyo wanatamani wangezaliwa na jinsia tofauti.
                                                     
           
Baadhi yao hukubaliana na hali yao lakini wengine huamua kuchukua hatua ya kujibadilisha jinsia ili wawe tofauti na mwanzo.
Inakadiriwa kwamba zaidi ya watu laki saba nchini marekani walibadilisha jinsia baada ya kutoridhika na jinsia zao za mwanzo.
Ukishabadilisha jinsia, unaruhusiwa kubadilisha jina na jinsia yako kwenye vyeti vyako vya kuzaliwa na vitambulisho vyako vyote.
zifuatazo ni hatua za kitaalamu zinazofuata kubadilisha jinsia.

hatua ya kwanza; kupimwa akili.
kabla ya kuanza hatua za kitatbibu za kubadilisha jinsia, madaktari bingwa wa mambo ya akili na saikolojia hukaa na mgonjwa ili kujua kweli kwamba ana tatizo la kisaikolojia ambalo linamfanya ahisi kwamba yeye hafai kua jinsia fulani.
kitaalamu ugonjwa huu unaitwa gender dysphoria.
baada ya hapo wataalamu hawa watakwambia hatua ambazo utapitia ili ubadilishe jinsia yaani kwanzia dawa mpaka upasuaji wa kubadilisha viungo vya uzazi.
watakwambia madhara yote ambayo huambatana na hatua utakazo pitia ili kufika huko lakini mwisho watahitaji kujua watu ambao watakua pamoja na wewe na kusapoti mabadiliko hayo kwani kila mtu akikupinga utaishi kwa shida sana.

hatua ya pili; matibabu ya homoni
homoni hizi ndio hatua ya kwanza kabisa ya kubadilisha maumbile ya mtu,  hubadilisha maumbile ya kike kua ya kiume au maumbile ya kiume kua ya kike.
wanawake ambao wanataka kua wanaume huanza kutumia homoni za kiume kitaalamu kama adrogens ambazo ndio huanza kuwabadilisha kua wanaume kwa kufanya yafuatayo.

  • huongeza misuli
  • kuleta sauti nzito
  • kuleta manyonya kwenye ngozi
  • kuongeza ukubwa wa kinembe.
wanaume ambao wanataka kubadilisha jinsia na kua wanaume hutumia homone za kike ambazo zinaweza kubadilisha maumbile yao yakawa ya kike mfano oestrogen.
dawa hizo 
  • hupunguza homoni za kiume aina ya testosterone mwilini.
  • hupunguza manyoya kwenye ngozi.
  • kuongeza matiti.
  • kugawanya mafuta ya mwili.
mabadiliko huanza mapema ndani ya mwezi mmoja na huweza kufika hatua ya mwisho kabisa ndani ya miaka mitano.
mfano mwanaume anayaetaka kua mwanaumke mpaka matiti yatokee  huchukua miaka mitatu mpaka mitano.
matumizi ya dawa hizi yana madhara mbalimbali kama magonjwa ya moyo, ugumba, damu kuganda, na kadhalika hivyo ni vizuri kufanya vipimo mbalimbali wakati wa kuanza dawa ilikuona kama mwili unaenda vizuri na dawa hizo.
wakati mwingine watumiaji wa dawa hupata msongo wa mawazo kutokana na kutokua na uhakika wa kitu ambacho wameamua hivyo ni vizuri kutembelea wataalamu wa ushauri.

hatua ya tatu; upasuaji
Hii ni hatua ya  mwisho kabisa wa kubadilisha baadhi ya viungo ambavyo haviwezi kubadilika kwa matumizi ya homoni tu.
Lakini asilimia sabini na tano ya watu ambao hujibadilisha jinsia zao hawapendi kufanya upasuaji kutokana na gharama kubwa sana pamoja na madhara ambayo hayawezi kubadilika baada ya kutoa maamuzi.
viungo kama matiti ya wanawake, uume kwa wanaume, korodani, kizazi na mirija ya uzazi ya kike huweza kuondolewa.
wanaume hufanyiwa upasuaji na kuwekewa uke lakini pia wanawake hufanyiwa upasuaji na kuwekewa uume.
upasuaji wa kuweka uke hua una matokeo mazuri lakini upasuaji wa kuweka uuume mpya kitaalamu kama phalloplasty hauna matokeo mazuri sana ndio maana wanawake wengi wanaotaka kua wanaume hawapendi kufanya upasuaji huo.

je unaweza kurudi kwenye jinsia yako ya zamani baada ya kubadilika?
baadhi ya watu waliojibadilisha jinsia hujutia maamuzi yao hivyo huamua kurudi kwenye jinsia zao za zamani.
mabadiliko ambayo yanafanywa na homoni mara nyingi yanaweza kurudi kama mwanzo iwapo ukiacha dawa japokua tafiti zinaonyesha kuna mabadiliko ambayo huletwa na homoni za kiume kwa wanawake yanaweza yasirudi kama mwanzo.
baadhi ya watu wamefanikiwa kurudi katika hali zao za zamani japo sio kwa asilimia mia moja.
Mabadiliko ya upasuaji hayawezi kurudi kama mwanzo.

                                                                
                                                          STAY ALIVE

                                     DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                             0769846183/0653095635

                                      

0 maoni:

Chapisha Maoni