data:post.body HAYA NDIO MAKOSA WANAYOFANYA WATU WANAOJIPIMA UKIMWI NYUMBANI. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HAYA NDIO MAKOSA WANAYOFANYA WATU WANAOJIPIMA UKIMWI NYUMBANI.

Watu wengi siku hizi wanapenda kujipima ukimwi wenyewe bila kwenda hospitali, ni kitu ambacho hata serikali sasa hivi imeanza kuunga mkono kampeni hizi ili kupata wagonjwa zaidi wa kuanza matibabu.
sababu kuu ya kujipima ni hofu ya kujulikana iwapo mtu atapima na mpenzi kwa wakati mmoja na wengine hupenda kupima na wapenzi wao wapya kabla hawajaanza kushiriki tendo la ndoa.
vipimo ambavyo vinapatikana kwa sasa nchi nzima ni vile vya damu japokua sasa hivi vipo vya kutumia mate lakini bado havipatikani nchi nzima.
kuna vipimo vikuu vitatu vya  kupima ukimwi hapa nchini kwetu kwa majina ya SD BIOLINE,UNIGOLD, na DETERMINE.

jinsi ya kupima ukimwi nyumbani.
1.chukua spirit futa kwenye kidole ambacho unataka kutoa damu
2.choma sindano toa damu kidogo kisha weka kwenye kipimo ambacho unacho.
3.mimina tone moja au mbili za damu kwenye kipimo.
4.weka tone moja au mbili ya dawa ya kupimia.
5.subiri dakika tano kisha soma majibu.

jinsi ya kusoma majibu
  • kipimo kitakisoma mstari mmoja wa controll kama hujaathirika.
  • kipimo kitasoma mistari miwili kama umeathirika na aina moja ya virusi vya ukimwi.
  • kipimo kitasoma mistari mitatu kama kama umeathiriwa na aina mbili ya virusi vya ukimwi.

makosa ambayo yanafanyika wakati wa kujipima ukimwi.
kukubali majibu ya vipimo vya mwanzo;  vipimo pekee ambavyo vinaruhusiwa kutoa majibu ya ukimwi ni kipimo cha UNIGOLD, kama ukipima ukimwi na kipimo cha bioline au determine kisha majibu yakasoma umeathirika inabidi ukahakikishe na kipimo cha UNIGOLD.
lakini kama umepima na vipimo vya determine na bioline ikaonekana huna ukimwi basi huhitaji kuendelea na vipimo zaidi.
kusoma majibu baada ya dakika tano; majibu ya ukimwi yanatakiwa yasomwe ndani ya dakika tano tu, ukikaa na kipimo muda mrefu kitaonyesha mstari wa pili, kitu ambacho kinaweza kumfanya muhusika aanze kupaniki akidhani kaathirika lakini hajaathirika.
kupima mara moja; mkiwa wapenzi wapya ni vizuri kupima tena baada ya miezi mitatu kuhakikisha kweli kwamba mko salama kabla ya kuvua kondom.
kuanza kufanya ngono nzembe baada ya kipimo kimoja ni hatari kwani mwenza wako anaweza kua ameshaathirika lakini vipimo bado havijaanza kusoma majibu yake.


                                                       STAY ALIVE

                                    DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                             0769846183/0653095635

Maoni 1 :

  1. Je ikiwa damu imejaa na bila kuvuka msitari wa c je hili lina maana gani

    JibuFuta