data:post.body Oktoba 2018 ~ SIRI ZA AFYA BORA...
  • Karibu kwenye blog ya SIRI ZA AFYA BORA ujifunze mbinu bora za afya ili uweze kuwa na afya bora.

Recent Posts

VYAKULA 7 MUHIMU SANA KWA WAGONJWA WA SHINIKIZO LA DAMU AU PRESHA.

Kama tayari wewe ni mgonjwa wa presha huenda tayari unafahamu kwamba ugonjwa wako ni wa kudumu yaani hakuna dawa ambayo itakuponywa moja kwa moja ila kuna uwezekano mkubwa ukameza dawa miasha yako yote.
ugonjwa wa shinikizo la damu ni ugonjwa unao ongeza msukumo wa damu kwenye kuta za mishipa ya damu na kusababisha madhara kwenye moyo, figo na mishipa ya damu. kama unataka kujua zaidi kuhusu ugonjwa wa presha soma hapa.......http://www.sirizaafyabora.info/2015/07/ufahamu-ugonjwa-wa-presha-ya-kupanda-na.html
katika matibabu ya ugonjwa wowote vyakula ni muhimu sana kwani ndio vinaujenga mwili wetu.. kimsingi muonekano wa miili yetu huchangiwa sana na chakula tunachokula.
vifuatavyo ni vyakula ambavyo ni muhimu sana kutumika na wagonjwa wa presha ili kupunguza presha hiyo ya damu.
mboga za majani; uwepo wa chumvi nyingi au sodium kwenye damu ni moja ya vyanzo vikuu vya presha kua juu kwa wagonjwa hawa wa presha.
potassium husaidia sana kuondoa kiasi kingi cha sodium mwilini au chumvi na kupunguza presha.
mboga za majani zenye potassium nyingi ni kama bamia, chainisi, spinachi, na mchicha ni nzuri sana kwa wagonjwa hawa.

berries; haya ni aina ya matunda ambayo yana kemikali inayoitwa flavonoids ambayo imethibitika  kuzuia ugonjwa wa shinikizo la damu na kushusha presha kwa wagonjwa hawa.
Mara nyingi hupatikana sana kwenye super market kubwa hapa nchini.
                                                                 

samaki; samaki ni chanzo kizuri cha protini kwenye mwili wa binadamu, samaki wa aina ya salmon kama anavyoonekana kwenye picha hapo chini ni chanzo kizuri cha kemikali ya omega 3 ambayo husaidia kushusha shinikizo la damu kwa kupunguza lehemu au cholestrol, na kuponya mishipa ya damu.              
                                   
mbegu; mbegu ni chanzo kizuri cha madini ya pottasium na magnesium ambayo husaidia kupunguza kiasi kikubwa cha chumvi mwilini na kupunguza presha.
Mbegu za maboga na alizeti ni nzuri zikiliwa na wagonjwa hawa.
                                             

vitunguu swaumu; hivi vina kiasi kikubwa cha kemikali ya nitric acid ambayo inafanya kazi ya kupanua mishipa ya damu, hii huongeza nafasi kubwa kwa ajili ya kupitisha damu vizuri kwenda sehemu mbalimbali za mwili bila kuongeza shinikizo la damu.
                                                               

ndizi mbivu; kama ilivyo kwa mboga za majani, ndizi mbivu ni muhimu sana kwani zina kiwango kikubwa cha potassium ambayo hutumika kuondoa chumvi nyingi mwilini ambayo husababisha presha kupanda.                        

                                               
tangawizi; hii hufanya kazi ya kulainisha damu kwa kupunguza uzito wake(blood thinner), na kupunguza shinikizo la damu kwa kiasi kikubwa sana.
unaweza kutumia unga wa tangawizi kwenye chai yako kila siku badala ya kutumia majani ya chai ambayo tunajua hayana faida yeyote.
                                                     


mwisho; kama wewe ni mgonjwa wa presha usipuuze kabisa ugonjwa wako, hakikisha unafuata maelekezo yote ya wataalamu uweze kuishi maisha salama.

                                                                 STAY ALIVE 
                                       DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                           
                                                     0769846183/0653095635

HIVI NDIO VYAKULA 5 MUHIMU ZAIDI KWA WAGONJWA WA SIKO SELI.

katika matibabu ya ugonjwa wa siko seli, mara nyingi nguvu nyingi zinawekwa kuhakikasha mgonjwa hapungukiwi na damu wala hapati maumivu makali ya mara kwa mara kwani hivyo ndio vyanzo vikuu vinavyosababisha vifo kwa wagonjwa hawa kwa kusababisha kufeli kwa baadhi ya viungo muhimu kama vigo, maini, mapafu na ubongo.
sasa kama wewe ni mama au baba una mgonjwa huyu ndani basi vyakula vifuatavyo visikose nyumbani kwako.
5.nyama nyekundu; nyama hii ina kiwango kikubwa sana cha madini ya chuma ambayo ni muhimu kwa mgonjwa wa huyu kwa ajili ya kuongeza kiasi cha damu mwilini.
kimsingi nyama nyekundu ina madini ya chuma mengi zaidi kuliko nyama  ya samaki na kuku. ule weupe wa nyama ya kuku na samaki ni taarifa ya kiasi kidogo cha madini ya chuma kilichomo.
Sijasema asile kuku wala samaki lakini nyama nyekundu ya ngombe na mbuzi ni muhimu zaidi.
Hivyo hakikisha hakosi nyama nyekundu angalau mara mbili kwa wiki huku ukimchanganyia na samaki na kuku siku zingine.
                                                     

4.matembele; hii ni mboga ya majani inayopatikana sehemu mbalimbali nchini kwetu, mboga hii ina kijani nzito kuliko mboga nyingi..
ukijani huu unaonyesha wingi wa madini ya folic acid ndani yake. Mboga zote za rangi ya kijani kama mchicha, chinese, kisamvu zina madini haya lakini matembele ndio kiboko yao.
folic acid ni muhimu sana kwa mgonjwa huyu kwani huungana na madini ya chuma kutengeneza seli nyekundu za damu ambazo ni muhimu sana kwa mgonjwa lakini pia ni husaidia kupunguza kiasi cha lehemu au cholestrol kinachopatikana kwenye ulaji nyama nyekundu.
                                                   
3.machungwa; haya ni jamii ya matunda ambayo yana kiasi kikubwa sana cha vitamin C. kazi ya vitamin hii ni kuusaidia mwili kuchukua madini ya chuma ambayo yanapatikana kwenye nyama unayokula.Hivyo hata ukimpa mtoto nyama  nyingi kiasi gani bila matunda unapoteza muda tu.
lakini pia matunda haya yana kemikali kitaalamu kama ant oxidant ambazo ni kinga ya mwili hasa kuzuia madhara ya ambatanayo na ulaji wa nyama nyekundu kama saratani, magonjwa nyemelezi na magonjwa ya moyo.

2.dagaa; dagaa zina kiasi kikubwa sana cha madini ya kashiamu kuliko kiwango kinachopatikana kwenye samaki.
sababu kubwa ni kwamba ukila dagaa unakula na mifupa yake ambayo ina kashiumu nyingi sana kuliko ukila samaki kwani sio rahisi kula samaki na mifupa yake.
wagonjwa hawa wanahitaji kashium nyingi kwa ajili ya kuimarisha mifupa yao, kusaidia mishipa ya fahamu na husaidia kuganda kwa damu haraka pale unapopata kidonda lakini pia dagaa zina madini ya chuma na huweza kua mbadala kwa watu ambao kununua nyama ni ngumu kwao.
kumbuka, kuvuja damu kidogo tu kwa mgonjwa huyu ni hatari na huweza kuleta kifo.
                                                      
        
 1.maji ya kunywa; asilimia sabini ya mwili wa binadamu ni maji tu, ni bora mgonjwa wa siko seli ashinde na kulala njaa kuliko kushinda na kulala bila kunywa maji.
maji ni muhimu sana kwa wagonjwa hawa kwani husaidia kusambaza seli zake sehemu mbalimbali za mwili bila kukwama.
mgonjwa huyu akikosa maji ya kutosha, seli za damu hukwama kwenye mishipa ya damu na kuanzisha maumivu makali sana au sickle cell crisis.
hivyo mgonjwa huyu akishinda na kulala bila kunywa maji basi majibu yake utayaona hapohapo kuliko kushinda na kulala njaa kwani damu haiwezi kupungua ghafla.
                                                                           

5.mwisho; kama mzazi wa mgonjwa wa siko seli basi ni vizuri ukawekeza kwenye elimu kujifunza kuhusu wagonjwa hawa ili uwe na elimu ya kutosha na kuweza kuwasaidia.
mgonjwa huyu anaweza kuishi maisha marefu kama watu wengine na tafit zinaonyesha mwanaume anaweza kuishi mpaka miaka 60 wakati mwanamke anaweza kuishi miaka 68.


                                                              STAY ALIVE
                                    DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

                                             0653095635/0769846183
                              







HIZI NDIO NJIA TISA ZA KUONDOA TATTOO KWENYE NGOZI.

Wakati mwingine katika maisha watu hufanya maamuzi ambayo huja kuyajutia baadae, moja ya maamuzi hayo ni kuchora tattoo ambayo baadae unaweza kujuta kwasababu huenda uliweka jina la mpenzi wako wa zamani au ulichora tattoo nyingi sana kiasi kwamba sasa zinakuathiri kupata baadhi ya fursa ambazo zinajitokeza.

Tattoo kikawaida hua haitoki lakini kutokana na ongezeko la watu ambao wanahitaji kuziondoa tattoo zao basi kuna njia mbalimbali ambazo zimeanzishwa za kuondoa tattoo japokua nyingi ni gharama sana au zinauma sana kama ifuatavyo.
laser; hii ni njia ya kutumia aina fulani ya mionzi kuondoa michoro ya tattoo kwenye ngozi, njia hii inauma na ni gharama sana kutumia.
huchukua muda mrefu kufuta kulingana na ukubwa wa tattoo yako lakini sio kazi ya siku moja hivyo utakua unaenda kila baada ya muda fulani.
gharama ni kama laki mbili na nusu kwa saa.
                                                               

kufunika na tatoo nyingine; wakati mwingine tattoo sio tatizo kwako lakini maneno uliyoandika ndio yanakukwaza.
Unaweza kuchora tattoo nyingine na kuifunika kwa maneno mengine ile tattoo ya kwanza ili iweze kupoteza maana yake ya zamani.
                                               

mafuta ya kutoa tattoo; kuna mafuta yamegunduliwa ya kuondoa tattoo lakini yanachukua muda mrefu sana kuifuta na ni gharama kutumia.
Uzuri wa mafuta haya hayana gharama sana lakini lazima uwe mvumilivu kwani itachukua muda mrefu na gharama kubwa.
ukiagiza mtandaoni chupa moja ni shilingi laki tatu.(amazon)
                                                                 

upasuaji; hii ni njia ya haraka ya kuondoa tattoo bila maumivu lakini gharama yake iko juu kidogo, ninachofanyika ni kwamba ngozi moja ya mwili wako hutumika kufunika sehemu ya ngozi ambayo imepakwa tattoo.
                                                             

kuisugua tattoo na chumvi; hii ni njia ambayo sio gharama ambayo unaisugua tattoo yako na chumvi kama mtu anayefanya scrubbing lakini kua makini usijiumize.
inachukua muda mrefu na baadhi ya madhara yake ni kuharibu muonekano wa ngozi.
                                                                 

limao: limao ni rahisi sana kupata kwenye mazingira yetu ya nyumbani, sio gharama kutumia lakini inataka uvumilivu na muda.
chukua maji ya uvuguvugu kisha osha sehemu yenye tattoo,baada ya hapo chukua limao na sugua sehemu yenye tatoo na usubiri mpaka pakauke.
baada ya hapo unaweza kuosha tena kwa maji ya uvuguvugu, fanya hivyo angalau mara moja kila siku.                                                  

asali;moja ya vitu bora kabisa kutumia kuondoa tattoo kwenye ngozi ni matumizi ya asali, jinsi ya kutumia;chukua kimiminika cha aloe vera, changanya na asali, maziwa ya mgando, na chumvi.
kisha changanya kimiminika hiki paka kwenye tattoo na uache mpaka ikauke.
kabla ya kupaka hakikisha umepaosha na maji ya uvuguvugu.
                                                                 

cream za kuondoa tattoo; kulingana na uhitaj mkubwa wa watu wengi kutaka kuondoa tattoo sasa hivi kuna makampuni mengi sana ya kutengeneza tattoo hizi, hivyo unaweza kuagiza tattoo mtandaoni kupitia amazon na ukazitumia kuondoa tattoo zako. bonyeza hapa  kuagiza.https://amzn.to/3vfeQpU
                                      


                                                      STAY ALIVE
                                DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

                                           0769846183/0653095635

VIPIMO FEKI VYA UKIMWI NI JANGA LA AFRIKA

Katika vita dhidi ya ukimwi hapa Afrika, kumekua na changamoto nyingi ikiwemo watu kupuuzia elimu ya kujikinga na ukimwi, kutokuwepo kwa dawa za kutosha za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi na watu kutojitokeza kabisa kupima ukimwi.
                                                                       

kulingana na muongozo wa shirika la afya duniani(WHO), mgonjwa hatakiwi kupewa majibu ya kua ameathirika na ukimwi mpaka apimwe na vipimo vya aina tofauti ambavyo vinahakikisha kweli ana maambukizi ya ukimwi.
shirika la doctor without borders(MSF) lilifanya utafiti  na kugundua kwamba vipimo havifanani nguvu hivyo kuleta makosa katika utoaji wa majibu na msisitizo mkubwa ukiwa katika watu ambao wanapewa majibu kwamba wameathirika wakati hawajaathirika kitaalamu kama false positive.
Ni kweli kuna baadhi ya watu ambao wanaweza kua na ukimwi vipimo vikaoneyesha hawana kitaalamu kama false negative lakini ni asilimia ndogo sana.

mtu kupewa majibu ya ukimwi kwamba ameathirika wakati hajaathirika huweza kuleta msongo mkubwa wa mawazo, maumivu ya kihisia na kuvunjika kwa mahusiano.

ushahidi wa hili ni upi?
Damu ilikusanywa kutoka kwa wagonjwa 2785 wa ukimwi ambao walikua wanahudhuria katika kliniki  mbalimbali za nchini kenya, uganda, congo, guinea na cameroon.
damu hiyo ilihifadhiwa vizuri na kutumwa ubeligiji kwa ajili ya vipimo vya ukimwi ili kuweza kuhakiki kama kweli wale watu ni wagonjwa wa ukimwi.
kati ya watu 2785 ambao damu zao zilichukuliwa, watu 1474 walikua hawana ukimwi na  watu 1306 pekee ndio walikua na virusi vya ukimwi kweli.
kwa maana nyingine hawa watu 1474 wamekua wakimeza dawa za ukimwi kwa muda wote huo kimakosa.

nchini Tanzania hali ikoje?
Hakuna tafiti kama hii iliyofanyika na kutangazwa rasmi nchini kwetu kuhusu hili lakini nitoe rai kwa wizara ya afya na wadau wengine wa afya kuliangalia swala hili kwa makini sana sababu kenya na uganda ni majirani zetu na sidhani kama teknolojia tunazotumia zimeachana mbali sana na teknolojia za kwao.
huenda na sisi tunatoa dawa kwa watu ambao sio wagonjwa.

                                                               STAY ALIVE
                                               DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

                                                       0769846183/0653095635

HAYA NDIO MAKOSA WANAYOFANYA WATU WANAOJIPIMA UKIMWI NYUMBANI.

Watu wengi siku hizi wanapenda kujipima ukimwi wenyewe bila kwenda hospitali, ni kitu ambacho hata serikali sasa hivi imeanza kuunga mkono kampeni hizi ili kupata wagonjwa zaidi wa kuanza matibabu.
sababu kuu ya kujipima ni hofu ya kujulikana iwapo mtu atapima na mpenzi kwa wakati mmoja na wengine hupenda kupima na wapenzi wao wapya kabla hawajaanza kushiriki tendo la ndoa.
vipimo ambavyo vinapatikana kwa sasa nchi nzima ni vile vya damu japokua sasa hivi vipo vya kutumia mate lakini bado havipatikani nchi nzima.
kuna vipimo vikuu vitatu vya  kupima ukimwi hapa nchini kwetu kwa majina ya SD BIOLINE,UNIGOLD, na DETERMINE.

jinsi ya kupima ukimwi nyumbani.
1.chukua spirit futa kwenye kidole ambacho unataka kutoa damu
2.choma sindano toa damu kidogo kisha weka kwenye kipimo ambacho unacho.
3.mimina tone moja au mbili za damu kwenye kipimo.
4.weka tone moja au mbili ya dawa ya kupimia.
5.subiri dakika tano kisha soma majibu.

jinsi ya kusoma majibu
  • kipimo kitakisoma mstari mmoja wa controll kama hujaathirika.
  • kipimo kitasoma mistari miwili kama umeathirika na aina moja ya virusi vya ukimwi.
  • kipimo kitasoma mistari mitatu kama kama umeathiriwa na aina mbili ya virusi vya ukimwi.

makosa ambayo yanafanyika wakati wa kujipima ukimwi.
kukubali majibu ya vipimo vya mwanzo;  vipimo pekee ambavyo vinaruhusiwa kutoa majibu ya ukimwi ni kipimo cha UNIGOLD, kama ukipima ukimwi na kipimo cha bioline au determine kisha majibu yakasoma umeathirika inabidi ukahakikishe na kipimo cha UNIGOLD.
lakini kama umepima na vipimo vya determine na bioline ikaonekana huna ukimwi basi huhitaji kuendelea na vipimo zaidi.
kusoma majibu baada ya dakika tano; majibu ya ukimwi yanatakiwa yasomwe ndani ya dakika tano tu, ukikaa na kipimo muda mrefu kitaonyesha mstari wa pili, kitu ambacho kinaweza kumfanya muhusika aanze kupaniki akidhani kaathirika lakini hajaathirika.
kupima mara moja; mkiwa wapenzi wapya ni vizuri kupima tena baada ya miezi mitatu kuhakikisha kweli kwamba mko salama kabla ya kuvua kondom.
kuanza kufanya ngono nzembe baada ya kipimo kimoja ni hatari kwani mwenza wako anaweza kua ameshaathirika lakini vipimo bado havijaanza kusoma majibu yake.


                                                       STAY ALIVE

                                    DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                             0769846183/0653095635

HIVI NDIO MAITI INAVYOWEZA KUMPA MWANAMKE MIMBA.

Hii habari unaweza kua umeshaisikia lakini mpaka leo hujaamini kwasababu haiingii alikini hata kidogo kwa maiti ya kiume kushiriki tendo la ndoa.
                                                                           

Historia ya dunia inaonyesha kwamba askari wengi ambao walikua wakirudisha miili ya marehemu kutoka vitani kwenda nyumbani walishiriki nazo tendo la ndoa.
tendo hili la ndoa lilihusisha miili ya jinsia zote yaani wanawake na wanaume.
hii ilifikia hatua kwamba baadhi ya wafalme na viongozi wakubwa walikua wana tabia ya kuuweka mwili wa marehemu kwa siku nne ndio uharibike  wawape watu wa kuzika.

necrophilia ni nini?
hii ni hali ambayo sio ya kawaida ambayo mtu ambaye yuko hai anavutiwa sana na kulala na wafu, mtu huyu anaweza hata kumchukua mwanamke au mwanaume ambaye yuko hai kisha akamuua wakati wa tendo la ndoa kwa kumkaba au kumnyima hewa kisha ashiriki naye tendo la ndoa baada ya kifo.
kwa mwili wa mwanamke kuingiliwa na mwanaume inaeleweka kabisa kwamba inawezekana kwa hali ya kawaida hata kama mwanamke amekufa.

je mwananaume mfu anaweza kushiriki vipi tendo la ndoa?
sisi wote tunafahamu kwamba uume hauwezi kusimama baaada ya kifo kwenye miili mingi, lakini hua kuna wanaume tofauti kidogo katika hili.
katika hali isiyo ya kawaida mwanaume anaweza anaweza akafa na uume ukabaki umesimama.
hali hii hutokea pale sehemu ya ubongo kwa jina ya celeberum inapokua imekandamizwa wakati wa kifo.
vyanzo vya vifo ambavyo uume huendelea kusimama ni kupigwa risasi ya kichwa, kunyongwa, kupewa sumu na kifo kinachosababishwa na kumeza dozi kubwa ya viagra.(dawa za kuongeza nguvu za kiume)
hali kama hii ikitokea ndipo mwanamke ambaye anapenda kulala na marehemu anapoamua kujiridhisha kwa kulala na mwili huu wa mwanaume.

je mwanaume mfu anaweza kumpa mtu mimba?
baada ya kifo mbegu za mwanaume hukaa masaa 24 kabla hazijaharibika, lakini mbegu hizi haziwezi kumpa mimba mwanamke kwa njia ya kawaida ya tendo la ndoa mpaka mbegu zile zichukuliwe na ziingizwe ndani ya kizazi cha mwanamke kitaalamu.
historia inaonyesha kwamba mtoto wa kwanza kuzaliwa kwa kutumia mbegu za mwanaume mfu alipatikana duniani mwaka 1999 na kazi hii ilifanyika nchini marekani.

                                                        STAY ALIVE

                                  DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                            0653095635/0769846183