Kila mtu hua ana ushahidi wa kua na rafiki yake ambaye hata ale chakula kiasi gani hawezi kunenepa, lakini wewe binafsi unahisi ukila kidogo tu unanenepa kupindukia na unashindwa kuelewa ni kitu gani kinasababisha hivyo.
Kimsingi ni kwamba asilimia 60 mpaka 70 ya unene au wembamba wa mtu unategemea urithi wa kibailojia kutoka kwa wazazi na mababu zake.(genetics)
lakini pia watafiti wanaongeza kwamba mambo mengine kama mazoezi na chakula tunachokula kinachangia uzito au muonekano wa miili yetu kwa asilimia 30 mpaka 40.
hivyo ukiwa unafanya mazoezi na kufanya diet kumbuka kwamba unapambana na asilimia 30 mpaka 40 tu, na zingine zilizobaki zinaamuliwa na genes zako.
watafiti wameshagundua genes ambazo zinaamua ukubwa wa miili yetu lakini mpaka leo hawaelewi genes hizo zinafanya kazi vipi, kama ukichunguza vizuri utagundua kuna baadhi ya ukoo watu ni wanene watupu wakati koo zingine ni wembamba watupu.
chanzo ni nini?
mwili wa binadamu una aina mbili za mafuta yaani mafuta meupe na mafuta ya kahawia, kimsingi mafuta ya kahawia ambayo yanapatikana shingoni na mgongoni kwa juu yana kiasi kikubwa cha mitochondria[sehemu ya mwili inayochuma chakula kutengeneza nguvu].
sasa kwa tabia hii ya mafuta kuchoma chakula kutengeneza nguvu hufanya watu ambao wana mafuta haya kuendelea kua wembamba na kuonekana vijana miaka yote.
hivyo kitaalamu mafuta haya tunaita mafuta mazuri kwani husaidia kuchoma chakula badala ya kuhifadhi mafuta.
mtoto akiwa mdogo anakua na mafuta ya kahawia mengi sana na ndio maana watoto wadogo huweza kula sana bila kunenepa na mafuta haya yanaendelea kupungua kadri mtoto anavyozidi kukua LAKINI mafuta meupe au white adipose tissue hayana uwezo kama mafuta ya kawahia.
mafuta meupe yana mitochondria kidogo na hufanya kazi ya kuhifadhi zaidi kuliko kuchoma, mafuta haya yanakua mengi zaidi mtu anavyokua mtu mzima na hayasaidii kuchoma chakula ili kupunguza uzito.
mafuta haya hupatikana karibia sehemu zote za mwili wa binadamu kama tumboni, makalioni, hips na sehemu mbalimbali.
watu weye mafuta meupe mengi hua wanene sana kutokana na asili ya mafuta haya kutochoma chakula sana kutengeneza joto.
sasa baadhi ya watu wana mafuta ya kahawia mengi zaidi kuliko meupe, watu hawa hawanenepi hata wale nini kwani miili yao huchoma chakula sana kutengeneza nguvu na joto.
watu wenye hii bahati ya kuzaliwa na mafuta mengi ya kahawia hua hawangaiki na swala la uzito kwenye maisha yao.
jinsi gani unaweza kuongeza mafuta ya kahawia mwilini?
kama unaona watu wengi kwenye ukoo wenu ni wanene, inawezekana kwenu kuna asili ya unene hivyo una mafuta mengi meupe.
mafuta ya kahawia yanaweza kuongezwa kwa kufanya mazoezi, kukaa sehemu yenye baridi kali ili kuulazimisha mwili kutengeneza joto, kula matunda ya apple, kupata usingizi wa kutosha, na kutojishindisha njaa kwa kula kwa kiasi.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0769846183/0653095635
Kimsingi ni kwamba asilimia 60 mpaka 70 ya unene au wembamba wa mtu unategemea urithi wa kibailojia kutoka kwa wazazi na mababu zake.(genetics)
lakini pia watafiti wanaongeza kwamba mambo mengine kama mazoezi na chakula tunachokula kinachangia uzito au muonekano wa miili yetu kwa asilimia 30 mpaka 40.
hivyo ukiwa unafanya mazoezi na kufanya diet kumbuka kwamba unapambana na asilimia 30 mpaka 40 tu, na zingine zilizobaki zinaamuliwa na genes zako.
watafiti wameshagundua genes ambazo zinaamua ukubwa wa miili yetu lakini mpaka leo hawaelewi genes hizo zinafanya kazi vipi, kama ukichunguza vizuri utagundua kuna baadhi ya ukoo watu ni wanene watupu wakati koo zingine ni wembamba watupu.
chanzo ni nini?
mwili wa binadamu una aina mbili za mafuta yaani mafuta meupe na mafuta ya kahawia, kimsingi mafuta ya kahawia ambayo yanapatikana shingoni na mgongoni kwa juu yana kiasi kikubwa cha mitochondria[sehemu ya mwili inayochuma chakula kutengeneza nguvu].
sasa kwa tabia hii ya mafuta kuchoma chakula kutengeneza nguvu hufanya watu ambao wana mafuta haya kuendelea kua wembamba na kuonekana vijana miaka yote.
hivyo kitaalamu mafuta haya tunaita mafuta mazuri kwani husaidia kuchoma chakula badala ya kuhifadhi mafuta.
mtoto akiwa mdogo anakua na mafuta ya kahawia mengi sana na ndio maana watoto wadogo huweza kula sana bila kunenepa na mafuta haya yanaendelea kupungua kadri mtoto anavyozidi kukua LAKINI mafuta meupe au white adipose tissue hayana uwezo kama mafuta ya kawahia.
mafuta meupe yana mitochondria kidogo na hufanya kazi ya kuhifadhi zaidi kuliko kuchoma, mafuta haya yanakua mengi zaidi mtu anavyokua mtu mzima na hayasaidii kuchoma chakula ili kupunguza uzito.
mafuta haya hupatikana karibia sehemu zote za mwili wa binadamu kama tumboni, makalioni, hips na sehemu mbalimbali.
watu weye mafuta meupe mengi hua wanene sana kutokana na asili ya mafuta haya kutochoma chakula sana kutengeneza joto.
sasa baadhi ya watu wana mafuta ya kahawia mengi zaidi kuliko meupe, watu hawa hawanenepi hata wale nini kwani miili yao huchoma chakula sana kutengeneza nguvu na joto.
watu wenye hii bahati ya kuzaliwa na mafuta mengi ya kahawia hua hawangaiki na swala la uzito kwenye maisha yao.
jinsi gani unaweza kuongeza mafuta ya kahawia mwilini?
kama unaona watu wengi kwenye ukoo wenu ni wanene, inawezekana kwenu kuna asili ya unene hivyo una mafuta mengi meupe.
mafuta ya kahawia yanaweza kuongezwa kwa kufanya mazoezi, kukaa sehemu yenye baridi kali ili kuulazimisha mwili kutengeneza joto, kula matunda ya apple, kupata usingizi wa kutosha, na kutojishindisha njaa kwa kula kwa kiasi.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0769846183/0653095635
0 maoni:
Chapisha Maoni