Jana imetokea taharuki nchini Tanzania huko mkoani kigoma baada ya binti mmoja aliyekua amethibitika kufariki katika hospitali ya baptist kuamka tena na kua mzima baada ya kurudishwa nyumbani kwa ajili ya mazishi.
maswali mengi yamezuka kutoka kwa wananchi na wataalamu baada ya hali hii, wengine wakidhani ni imani za kishirikina huku wengine wakimtupia lawama daktari kwamba huenda utaalamu wake ulikua finyu.
je ukweli ni upi?
kitaalamu mtu akishakufa kabisa hawez kurudi tena kwenye uhai kwani ubongo huanza kuharibika ndani ya dakika tano tu baada ya kufariki huku viungo vingine vilivyobaki vikiendelea kuharibika taratibu ndani ya masaa machache baada ya kifo chake, hivyo kwa hali yeyote mtu aliyekua imesemekana amekufa afu akarudi kwenye uhai basi ujue huyo alikua hajafa.
kitu gani kinatokea mpaka watu wanahisi mtu amekufa wakati bado yuko hai?
hii hali kitaalamu inaitwa suspended animation, ni hali ambayo hutokea pale ambapo moyo, ubongo na mfumo wa upuaji huanza kufanya kazi kwa kiwango cha chini sana ambacho hukaribia hali ya kifo kabisa lakini unakua hujafa rasmi.
kiwango hicho cha ufanyaji wa kazi wa viungo kinaweza kushindwa kugundulika kwa hali ya kawaida au kwa vipimo vya kawaida ambavyo vimapatikana kwenye hospitali zetu na kama hauko makini sana kama daktari anaweza ukathibitisha kifo.
hali hii huweza kutokea baada ya kupewa dawa za usingizi kabla ya upasuaji, mshituko wa moyo, ugonjwa kipindupindu, sumu(narcotics), joto kali sana, kuumia kwa kichwa, au kwa mazoezi ya yoga.
tofauti kati ya kifo na hali hii ni kwamba mtu anaweza akarudi kwenye hali yake ya kawaida iwapo akipewa matibabu ya kushtua moyo kitaalamu kama cardio pulmonary resuscitation au anaweza akaamka mwenyewe.
hivyo kimsingi tunasema hali hii ni ya karibu kabisa na kifo lakini bado kifo hakijatokea rasmi.
watu wengi wa aina hii huweza kuota ndoto za ajabu au kuona maluweluwe na baadae wakaja kuhadithia kwamba walimuona yesu kitu ambacho sio kweli.
je kuna matukio kama haya ambayo yameshawahi kutokea?
ndio, kuna watu wengi sana ambayo yametokea ya watu koenekana kufufuka lakini ni machache sana ambayo yamerekodiwa mpaka sasa kama ifuatavyo.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
maswali mengi yamezuka kutoka kwa wananchi na wataalamu baada ya hali hii, wengine wakidhani ni imani za kishirikina huku wengine wakimtupia lawama daktari kwamba huenda utaalamu wake ulikua finyu.
je ukweli ni upi?
kitaalamu mtu akishakufa kabisa hawez kurudi tena kwenye uhai kwani ubongo huanza kuharibika ndani ya dakika tano tu baada ya kufariki huku viungo vingine vilivyobaki vikiendelea kuharibika taratibu ndani ya masaa machache baada ya kifo chake, hivyo kwa hali yeyote mtu aliyekua imesemekana amekufa afu akarudi kwenye uhai basi ujue huyo alikua hajafa.
kitu gani kinatokea mpaka watu wanahisi mtu amekufa wakati bado yuko hai?
hii hali kitaalamu inaitwa suspended animation, ni hali ambayo hutokea pale ambapo moyo, ubongo na mfumo wa upuaji huanza kufanya kazi kwa kiwango cha chini sana ambacho hukaribia hali ya kifo kabisa lakini unakua hujafa rasmi.
kiwango hicho cha ufanyaji wa kazi wa viungo kinaweza kushindwa kugundulika kwa hali ya kawaida au kwa vipimo vya kawaida ambavyo vimapatikana kwenye hospitali zetu na kama hauko makini sana kama daktari anaweza ukathibitisha kifo.
hali hii huweza kutokea baada ya kupewa dawa za usingizi kabla ya upasuaji, mshituko wa moyo, ugonjwa kipindupindu, sumu(narcotics), joto kali sana, kuumia kwa kichwa, au kwa mazoezi ya yoga.
tofauti kati ya kifo na hali hii ni kwamba mtu anaweza akarudi kwenye hali yake ya kawaida iwapo akipewa matibabu ya kushtua moyo kitaalamu kama cardio pulmonary resuscitation au anaweza akaamka mwenyewe.
hivyo kimsingi tunasema hali hii ni ya karibu kabisa na kifo lakini bado kifo hakijatokea rasmi.
watu wengi wa aina hii huweza kuota ndoto za ajabu au kuona maluweluwe na baadae wakaja kuhadithia kwamba walimuona yesu kitu ambacho sio kweli.
je kuna matukio kama haya ambayo yameshawahi kutokea?
ndio, kuna watu wengi sana ambayo yametokea ya watu koenekana kufufuka lakini ni machache sana ambayo yamerekodiwa mpaka sasa kama ifuatavyo.
- mwaka 1999 daktari wa sweeden kwa jina la Ana Bagenholm alitumbukia kwenye ziwa la barafu na kukaa kwa dakika 40 huku moyo wake ukiwa umesimama na baadae aliokolewa ubongo wake ukiwa mzima kabisa na akaishi tena.
- mwaka 2006 Mitsutaka Uchikosh ambaye ni mjapani alipoteza fahamu na kukaa sehemu yenye baridi kali kwa siku 24 bila kula wala kunywa akiwa kwenye hali ya herbanation yaani katikati ya uhai na kifo.
- mwaka 2001 mtoto Erica nordby alikaa masaa mawili bila mapigo ya moyo huku joto laki likishuka mpaka nyuzi joto 16 kama mfu wakati joto la binadamu wa kawaida ni nyuzi joto 37.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
0 maoni:
Chapisha Maoni