data:post.body HUU NDIO UMRI AMBAO MBEGU ZA KIUME ZINAANZA KUPOTEZA UBORA WAKE. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HUU NDIO UMRI AMBAO MBEGU ZA KIUME ZINAANZA KUPOTEZA UBORA WAKE.

Inafahamika kwamba mwanaume anaweza kuzalisha mwanamke kwa kipindi chote cha maisha yake kwani mwanaume aliyerekodiwa kumpa mwanamke mimba akiwa na umri mkubwa kabisa alikua na miaka 96.                                                    

Lakini linapokuja swala la kubeba mimba salama na kuzaa watoto salama umri wa mwanaume ni muhimu sana kama jinsi umri wa mwanamke ulivyo muhimu, kama una mpango wa kuzaa ni vizuri kuzaa mapema sana ili kuepuka matatizo ambayo yanatokana na umri mkubwa.
baadhi ya magonjwa ya watoto kama kua bubu, magonjwa ya akili na baadhi ya saratani husababishwa na mwanaume kua na umri mkubwa.

ubora wa mbegu unapungua mtu akiwa na miaka mingapi?
Kadri umri unavyozidi kua mkubwa uwezo wa mwanaume kumpa mwanamke mimba unazidi kupungua, mwanaume akifikisha miaka 40 uwezo wa kumpa mwanamke mimba ndio unaanza kupungua rasmi.
kipindi hiki mwanaume humpa mwanamke mimba kwa shida sana na hata akifanikiwa uwezekano wa mimba kuharibika hua mkubwa sana.
sio kwamba wanaume wote wenye umri zaidi ya miaka 40 watapata shida hizi lakini hichi ni kipindi cha bahati nasibu sana hivyo kama una mpango wa kubeba mimba na kuzaa basi hakikisha unafanya maamuzi mapema.

nini cha kufanya?
kuna baadhi ya wanaume huchelewa kuoa kwasababu mbalimbali ambazo zinakua nje ya uwezo wao lakini kumbuka hakuna mahusiano kati ya ndoa na kuzaa kwenye dunia ya sasa.
unaweza kuanza uzazi hata kama huna uwezo wa kugharamia harusi au hauko tayari kwa sasa kuingia kweye majukumu hayo lakini ukafuga ndoa baadae lakini mtoto hasubiri.
lakini pia kama tayari ndio umri sahihi wa kuzaa umeshakutupa mkono na una nia ya kupata watoto basi ni vizuri mimba hiyo ifuatiliwe kwa makini sana huku ikifanyiwa vipimo mbalimbali ili kujua kama mtoto mtarajiwa ana tatizo lolote na kama tatizo likionekana basi hatua ichukuliwe mapema.

                                                                        STAY ALIVE

                                                        DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO\
                                                                     0653095635/0769846183

0 maoni:

Chapisha Maoni