data:post.body FAHAMU KIFO CHA MAJI KINAVYOTOKEA NA JINSI YA KUJIOKOA.[IMMERSION DEATH] ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

FAHAMU KIFO CHA MAJI KINAVYOTOKEA NA JINSI YA KUJIOKOA.[IMMERSION DEATH]

Vifo vya maji sio vigeni kuviona au kuvisikia kwenye maisha yetu, vifo hivi ni moja ya vifo vibaya sana ambavyo mwanadamu yeyote asingependa kuvipitia kwenye maisha yake.
                                                                   

sio kila mtu anayekutwa kwenye maji anakua alikufa sababu ya maji, kuna wengine walikufa kabla hawajatumbukia kwenye maji na wengine waliuawa na magonjwa ambayo walikua nayo tangu zamani hasa magonjwa ya moyo.
ukiwa na tatizo la  moyo ukatumbukia kwenye maji ule uchovu mdogo tu wa kupambana na maji utasababisha moyo kusimama.

mtu anakufaje akiingia kwenye maji?
mtu akitumbukia kwenye maji anazama kidogo sababu ya uzito wake pamoja na kasi ya mvutano kitaalamu kama force of gravity lakini baada ya sekunde chache hurudi juu ya maji sababu ya uasili wa mwili kuelea.(boyancy).
kama akitumbukia kwenye maji ya baridi sana atavuta hewa kwa nguvu sababu ya mshtuko wa mwili ambao unatokea.(reflex from skin stimulation).
mtu huyu anaweza kushikilia pumzi kwa dakika chache lakini baada ya muda hewa ya carbondioxide itamzidia mwilini mwake na atajikuta anaanza kupumua na kuvuta maji kwenye mapafu yake.
kadri mtu huyu anavyozidi kulia kuomba msaada na kupambana ndio anavyozidi kuvuta maji mengi zaidi.
anaweza kutapika lakini anavyozidi kupambana ndio anazidi kuzama zaidi kwenye maji.
kuzama na kuibuka kwenye maji huendelea mpaka mtu anapata degedege na kupoteza fahamu ndani ya maji.
mtu akishapoteza fahamu hawezi kujiokoa tena na kifo kitamkuta hapa.
mara nyingi watu hupoteza fahamu kwanzia dakika ya tatu mpaka ya kumi ambapo ubongo hukosa hewa kiasi kwamba hauwez kupona hata mtu akikolewa muda huo.(irrevesible brain damage).

kifo kwenye maji ya yasiyo na chumvi.
maji ya mtoni na ziwani hua na chumvi kidogo kama 0.6% hivi, mtu akifa huvuta maji haya kwa kiasi kikubwa na kupitia mapafu huingia ndani ya damu.
ndani ya dakika moja damu inakua imeshachanganyikana na damu zaidi ya lita mbili na nusu, baada ya dakika tatu maji huzidi zaidi.
hii hufanya moyo kuzidiwa na kushindwa kusukuma kiasi kikubwa cha maji kilichoingia.
hii husababisha moyo kusimama na kuleta kifo.
                                                               


kifo kwenye maji ya chumvi.
kiasi kikubwa cha chumvi iliyoko kwenye maji huingia kwenye damu kupitia mapafu, muhanga hufariki kwa kukosa hewa safi ya oxygen.

nini cha kufanya?
jukumu la kulinda maisha lipo mikononi mwako, kama una shughuli zako ambazo zinakufanya upite kwenye maji hakikisha unamiliki life jacket yako kwenye begi ambayo utaivaa kila siku wakati wa kupita kwenye chombo hicho.
ukitumbukia kwenye maji na life jacket kitakachoweza kukuua na wanyama wa majini au njaa kitu ambacho sio rahisi.
kumbuka ukitumbukia kwenye maji ya baridi kali sana unaweza ukafa kwa sababu ya baridi kama jinsi watu wengi walivyokufa baada ya meli ya TITANIC kuzama.
wengi wao walikua na life jackets lakini bahari ya atlantic kazikazini ni baridi sana kiasi kwamba ukitumbukia unakufa ndani ya dakika 30.

                                                                      STAY ALIVE

                                                   DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                         0769846183/0653095635


                                                       

0 maoni:

Chapisha Maoni