data:post.body HIVI NDIO UNAVYOWEZA KUACHA DAWA ZA KISUKARI KWA CHAKULA NA MAZOEZI. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIVI NDIO UNAVYOWEZA KUACHA DAWA ZA KISUKARI KWA CHAKULA NA MAZOEZI.

Ugonjwa wa kisukari ni moja ya magonjwa tishio ambayo yapo kwenye kikundi cha magonjwa ambayo sio ya kuambukizwa, ukitaka kujua zaidi kuhusu ugonjwa huu soma hapa....http://www.sirizaafyabora.info/2016/04/kabla-ya-ukoloni-utafiti-unaonyesha.html
                                                                 
wagonjwa wengi sana pamoja na kutumia dawa mbalimbali bado hujikuta wanashindwa kuiweka sukari katika hali ya kawaida hivyo kujikuta wanakua na kiwango cha sukari juu muda wote.
kiukweli hakuna mtu anayependa kumeza dawa au kuchoma sindano na ikitokea njia mbadala wa kuacha vitu hivyo kila mtu atafurahi kutumia njia hiyo.
sasa katika matibabu ya kisukari wataalamu wengi na wagonjwa wengi husahua matibabu ya kwanza kabisa ambayo mgonjwa anatakiwa aanze nayo na ikishindikana ndio aanze dawa.

matibabu ya kwanza ya kisukari ni yapi?
kwa wagonjwa kisukari aina ya kwanza au type 1[ambayo hupata watoto wadogo mara nyingi] unatakiwa kuanza dawa hapo hapo kwani mgonjwa anakua hana insulin hata kidogo mwilini lakini kwa aina ya pili kitaalamu kama type 2 mgonjwa anatakiwa aanze mazoezi na diet kwanza kwani anakua anayo insulini mwilini lakini imeshindwa kufanya kazi vizuri sababu ya unene au insulin inazalishwa kidogo sana.
watu wengi huanzishiwa dawa kwa kukosa nidhamu ya chakula na mazoezi lakini ukiwa na nidhamu hiyo huhitaji dawa kabisa.

kwanini wagonjwa hawa wanaweza kutibiwa kwa mazoezi na chakula tu?
sababu watu hawa tayari wana insulini mwilini ambayo haijaitoshelezi hivyo ukifanya mazoezi mwili husukuma sukari ndani ya misuli na kuipunguza kwenye damu na ukila vizuri kiwango cha sukari kitabaki kawaida na hautahitaji dawa kabisa.
kimsingi mtu ambaye anahitaji nguvu za mwili kwa kutumia chakula cha wanga ndio ambaye sukari ni tatizo kwake lakini ukitumia njia tofauti kupata nguvu kama kwa kula vyakula vya protini na mafuta basi kisukari hakina ujanja.
 kiufupi ni kwamba kisukari ni ugonjwa wa watu ambao ni lazima wale wanga kama ugali, wali, viazi, mihogo, mikate, maandazi, chapati na kadhalika hivyo ukiamua kuachana na wanga basi umepona.

mtu ambaye ameshatumia dawa miaka mingi anaweza kuacha dawa?
ndio, kama ukiweza kufauata masharti ya chakula na mazoezi basi unaweza ukaacha dawa kabisa, kikubwa maisha hayo mapya yanatakiwa kua sehemu ya maisha yako sio kwamba ufanye hivyo kwa muda tu halafu uache.
kimsingi watu wengi huugua kisukari na magonjwa mengine yasio ya kuambukizwa kwa kushindwa kula vizuri na kufanya mazoezi hivyo hata ambao hawaumwi wanatakiwa waishi kwa makini kwa kufanya mzoezi na kula vizuri.

chakula gani cha kutumia kwa wagonjwa hawa ili waweze kuacha dawa?
kwa mgonjwa ambaye tayari anatumia dawa au hatumii dawa diet ifuatayo kitaalamu kama ketogenic diet anatakiwa aanze nayo,  diet hii inalenga kuondoa kabisa vyakula vya wanga kwenye chakula chako na kuacha kiasi kidogo sana, ukitaka kujua zaidi kuhusu diet hii soma hapa......http://www.sirizaafyabora.info/2018/06/jinsi-unavyoweza-kupunguza-uzito-kwa.html

mfano wa diet hiyo...

asubuhi;
yai mbili za kuchemshwa, kipande cha parachichi moja na chai ya rangi au maziwa isiyokua na sukari.

mchana;
 samaki mmoja mkubwa au mdogo au dagaa  au robo kuku, mboga za majani nyingi, kipande cha parachichi moja na ndizi moja ya kupika au chapati.

usiku; 
samaki au  dagaa au robo kuku, mboga za majani za kutosha na kipande cha  parachichi.

kumbuka kunywa maji mengi ya kutosha, baada ya kuanza diet hii kua makini na kiwango chako cha sukari  cha damu kwani utakiwa upunguze kiasi cha dozi ya dawa unazotumia au kuacha kabisa dawa ndani ya muda mfupi hivyo ukianza diet hii anza kupima sukari kila siku kuifuatilia.
usile vayakula zaidi ya hivi nilivyotaja hapo juu ukiwa unaanza hata kama ni matunda usile kwani baadhi ya matunda ya sukari nyingi sana...unaweza ukapata hamu ya vyakula vingine kama binadamu lakini unaweza kujipangia kuvila siku maalumu kama kwenye sherehe au siku moja ya weekend kwa wiki kisha unarudi kwenye mfumo wako.
kama kiwango chako cha lehemu au cholestrol kiko vizuri unaweza kula na nyama ya ngombe, mbuzi au nguruwe.
kumbuka, pamoja na faida za  kuacha dawa, diet hii itakupunguza sana uzito kitu ambacho ni muhimu sana kwa wagonjwa wa kisukari.

mazoezi gani unaweza kufanya?
nunua kamba kaa nayo nyumbani kwani watu wengu hukosa muda wa kwenda gym kisha fanya mazoezi ya kuruka kamba angalau kuruka mara 500 kila jioni au asubuhi.
unaweza ukafanya haya mazoezi angalau mara tatu au nne kwa wiki.
kama una nafasi ya kufanya mazoezi ya aina ya aina nyingine pia unaweza kufanya, kama kazi zako ni ngumu za kutoa jasho  au unatumia baiskeli kwenye shughuli zako basi hauhitaji tena mazoezi.

mifano hai;
kuna watu wengi mabao wameacha dawa kwa kufauta masharti haya, mwezi uliopita kaka yangu mmoja alinipigia simu,  sukari ikiwa imemuanza kwa mara ya kwanza maishani mwake akiwa na sukari ya 26mmol/l na alikua ameshapewa dawa za kuanza.
nikamwambia aanze diet hii, na baada ya siku tatu sukari tu  yake ilikua 4.6mmol/l ambayo ni kawaida kabisa.
lakini pia ukiingia mtandaoni utakutana na watu wengi sana walio acha dawa kwa kutumia hii ketogenic diet.


                                                                            STAY ALIVE

                                              DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                             0653095635/0769846183
                                                              

0 maoni:

Chapisha Maoni