data:post.body Agosti 2018 ~ SIRI ZA AFYA BORA...
  • Karibu kwenye blog ya SIRI ZA AFYA BORA ujifunze mbinu bora za afya ili uweze kuwa na afya bora.

Recent Posts

KIASI GANI CHA POMBE KINAWEZA KIKAKUUA?

Kama ni mfuatiliaji mzuri wa habari, utakua umeshasikia vifo vingi ambavyo hua vinatokea kwenye mashindano ya kunywa pombe.
                                                                       
mwili wa binadamu una kiasi ambacho ukifika huwez kuendelea kuvumilia pombe yaani utakufa tu.
ripoti za umoja wa mataifa zinasema kwamba kila mwaka watu milion 3 hufariki kwa sababu ambazo zinasababishwa na unywaji wa pombe...yaani kwa pombe yenyewe au ajari na madhara mengine ya unywaji wa pombe.
kutokana na wingi wa matangazo ambayo yanaisifia pombe basi vijana wengi hua hawaamini kitu hichi na kuhisi kwamba ni sheria tu ambazo zinawekwa ili kuwanyima uhuru wa kunywa pombe.

kiasi gani cha pombe kinatakiwa kiafya?
kimsingi mwanaume anatakiwa anywe unit mbili za pombe kama bia mbili hivi au  glass moja ya wine au robo glass ya pombe kali.
mwanamke anatakiwa anywe unit moja sawa na nusu ya vitu nilivyotaja hapo kwa mwanaume.
kunywa zaidi ya hapo hakuwezi kukuua hapo hapo ila ni hatari kiafya.

kiasi gani cha pombe ambacho kinaua?
kabla mtu hajafa mara nyingi hupoteza fahamu au kutapika sana na kuishiwa maji mwilini, wakati mwingine kufa kwa pombe sio kwa kunywa pombe siku nzima au wiki nzima,mtu anaweza kufika bar akaizifakamia pombe nyingi ndani ya dakika 15 au 30 zikamuua.
sasa kitaalamu gramu 300 za pombe zinaweza kukuua, hii ni sawa na bia 30 za kawaida, lita moja ya pombe kali kama spirit na chupa nne za wine.
japokua kuna watu wachache sana wanaweza wakaponea hospitali kwa kunywa kiasi kikubwa cha pombe kama hichi au wengine walevi wa siku nyingi sana wanaweza wasife lakini uwezekano wa kufa ni mkubwa mno.
na ikitokea mlevi ameacha pombe kabisa halafu akazirudia kama baada ya mwaka mmoja na kunywa kiasi kile kile cha zamani wakati anacha basi uwezekano wa kufa ni mkubwa sana kwani mwili unakua haujazoea kama hapo mwanzo.
ni vizuri kunywa pombe taratibu ndani ya muda mrefu ili ukiona zimekukamata sana uweze kuacha kwanza.
lakini ile tabia ya kuzinywa nyingi haraka, zikianza kazi mwilini unaweza usiamke tena.

                                                               STAY ALIVE
                                 DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
          
                                                         0653095635/0769846183

HIVI NDIO UNAVYOWEZA KUACHA DAWA ZA KISUKARI KWA CHAKULA NA MAZOEZI.

Ugonjwa wa kisukari ni moja ya magonjwa tishio ambayo yapo kwenye kikundi cha magonjwa ambayo sio ya kuambukizwa, ukitaka kujua zaidi kuhusu ugonjwa huu soma hapa....http://www.sirizaafyabora.info/2016/04/kabla-ya-ukoloni-utafiti-unaonyesha.html
                                                                 
wagonjwa wengi sana pamoja na kutumia dawa mbalimbali bado hujikuta wanashindwa kuiweka sukari katika hali ya kawaida hivyo kujikuta wanakua na kiwango cha sukari juu muda wote.
kiukweli hakuna mtu anayependa kumeza dawa au kuchoma sindano na ikitokea njia mbadala wa kuacha vitu hivyo kila mtu atafurahi kutumia njia hiyo.
sasa katika matibabu ya kisukari wataalamu wengi na wagonjwa wengi husahua matibabu ya kwanza kabisa ambayo mgonjwa anatakiwa aanze nayo na ikishindikana ndio aanze dawa.

matibabu ya kwanza ya kisukari ni yapi?
kwa wagonjwa kisukari aina ya kwanza au type 1[ambayo hupata watoto wadogo mara nyingi] unatakiwa kuanza dawa hapo hapo kwani mgonjwa anakua hana insulin hata kidogo mwilini lakini kwa aina ya pili kitaalamu kama type 2 mgonjwa anatakiwa aanze mazoezi na diet kwanza kwani anakua anayo insulini mwilini lakini imeshindwa kufanya kazi vizuri sababu ya unene au insulin inazalishwa kidogo sana.
watu wengi huanzishiwa dawa kwa kukosa nidhamu ya chakula na mazoezi lakini ukiwa na nidhamu hiyo huhitaji dawa kabisa.

kwanini wagonjwa hawa wanaweza kutibiwa kwa mazoezi na chakula tu?
sababu watu hawa tayari wana insulini mwilini ambayo haijaitoshelezi hivyo ukifanya mazoezi mwili husukuma sukari ndani ya misuli na kuipunguza kwenye damu na ukila vizuri kiwango cha sukari kitabaki kawaida na hautahitaji dawa kabisa.
kimsingi mtu ambaye anahitaji nguvu za mwili kwa kutumia chakula cha wanga ndio ambaye sukari ni tatizo kwake lakini ukitumia njia tofauti kupata nguvu kama kwa kula vyakula vya protini na mafuta basi kisukari hakina ujanja.
 kiufupi ni kwamba kisukari ni ugonjwa wa watu ambao ni lazima wale wanga kama ugali, wali, viazi, mihogo, mikate, maandazi, chapati na kadhalika hivyo ukiamua kuachana na wanga basi umepona.

mtu ambaye ameshatumia dawa miaka mingi anaweza kuacha dawa?
ndio, kama ukiweza kufauata masharti ya chakula na mazoezi basi unaweza ukaacha dawa kabisa, kikubwa maisha hayo mapya yanatakiwa kua sehemu ya maisha yako sio kwamba ufanye hivyo kwa muda tu halafu uache.
kimsingi watu wengi huugua kisukari na magonjwa mengine yasio ya kuambukizwa kwa kushindwa kula vizuri na kufanya mazoezi hivyo hata ambao hawaumwi wanatakiwa waishi kwa makini kwa kufanya mzoezi na kula vizuri.

chakula gani cha kutumia kwa wagonjwa hawa ili waweze kuacha dawa?
kwa mgonjwa ambaye tayari anatumia dawa au hatumii dawa diet ifuatayo kitaalamu kama ketogenic diet anatakiwa aanze nayo,  diet hii inalenga kuondoa kabisa vyakula vya wanga kwenye chakula chako na kuacha kiasi kidogo sana, ukitaka kujua zaidi kuhusu diet hii soma hapa......http://www.sirizaafyabora.info/2018/06/jinsi-unavyoweza-kupunguza-uzito-kwa.html

mfano wa diet hiyo...

asubuhi;
yai mbili za kuchemshwa, kipande cha parachichi moja na chai ya rangi au maziwa isiyokua na sukari.

mchana;
 samaki mmoja mkubwa au mdogo au dagaa  au robo kuku, mboga za majani nyingi, kipande cha parachichi moja na ndizi moja ya kupika au chapati.

usiku; 
samaki au  dagaa au robo kuku, mboga za majani za kutosha na kipande cha  parachichi.

kumbuka kunywa maji mengi ya kutosha, baada ya kuanza diet hii kua makini na kiwango chako cha sukari  cha damu kwani utakiwa upunguze kiasi cha dozi ya dawa unazotumia au kuacha kabisa dawa ndani ya muda mfupi hivyo ukianza diet hii anza kupima sukari kila siku kuifuatilia.
usile vayakula zaidi ya hivi nilivyotaja hapo juu ukiwa unaanza hata kama ni matunda usile kwani baadhi ya matunda ya sukari nyingi sana...unaweza ukapata hamu ya vyakula vingine kama binadamu lakini unaweza kujipangia kuvila siku maalumu kama kwenye sherehe au siku moja ya weekend kwa wiki kisha unarudi kwenye mfumo wako.
kama kiwango chako cha lehemu au cholestrol kiko vizuri unaweza kula na nyama ya ngombe, mbuzi au nguruwe.
kumbuka, pamoja na faida za  kuacha dawa, diet hii itakupunguza sana uzito kitu ambacho ni muhimu sana kwa wagonjwa wa kisukari.

mazoezi gani unaweza kufanya?
nunua kamba kaa nayo nyumbani kwani watu wengu hukosa muda wa kwenda gym kisha fanya mazoezi ya kuruka kamba angalau kuruka mara 500 kila jioni au asubuhi.
unaweza ukafanya haya mazoezi angalau mara tatu au nne kwa wiki.
kama una nafasi ya kufanya mazoezi ya aina ya aina nyingine pia unaweza kufanya, kama kazi zako ni ngumu za kutoa jasho  au unatumia baiskeli kwenye shughuli zako basi hauhitaji tena mazoezi.

mifano hai;
kuna watu wengi mabao wameacha dawa kwa kufauta masharti haya, mwezi uliopita kaka yangu mmoja alinipigia simu,  sukari ikiwa imemuanza kwa mara ya kwanza maishani mwake akiwa na sukari ya 26mmol/l na alikua ameshapewa dawa za kuanza.
nikamwambia aanze diet hii, na baada ya siku tatu sukari tu  yake ilikua 4.6mmol/l ambayo ni kawaida kabisa.
lakini pia ukiingia mtandaoni utakutana na watu wengi sana walio acha dawa kwa kutumia hii ketogenic diet.


                                                                            STAY ALIVE

                                              DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                             0653095635/0769846183
                                                              

HII NDIO DAWA YA MBADALA WA P2 AMBAZO ZINAUZWA BEI RAHISI.

Dawa ya P2 imekua maarufu sana kwa matumizi ya wanawake wengi ambao wanaitumia kwa ajili ya kutaka kuzuia mimba baada ya tendo la ndoa.
                                                                                          

dawa hii haina tofauti na zile zinazomezwa kila siku kwenye uzazi wa mpango ila tofauti yake ni kiwango cha dawa,  ambapo hii p2 inakua na miligram nyingi kuliko dawa za uzazi wa mpango za kawaida.

P2 inatumikaje?
ili iweze kufanya vizuri inatakiwa imezwe angalau ndani ya siku tatu baada ya kushiriki tendo la ndoa bila kutumia kinga.

kwanini nazungumzia mbadala wa P2?
dawa hizi ni gharama sana kwa watu wenye uwezo wa chini, dozi huuzwa kwanzia shilingi 5000 mpaka 10000, na ikitokea ukajisahau tena utaingia gharama tena, kitu ambacho ni kigumu kidogo.

mbadala wa p2 ni upi?
kuna dawa zinitwa microgynon ambazo hutumika kumezwa kila siku kama njia ya uzazi wa mpango lakini pia zinatumika kama njia ya kuzuia mimba kama vile p2.
dawa hizi zinauzwa shilingi 500 mpaka 1000 inategemea na sehemu uliyonunua.

inatumika vipi?
nunua vidonge vya microgynon ambavyo vinakua 28 kwenye packet, chukua vidonge vinne kunywa kisha baada ya saa 12 meza vingine vinne na hapo utakua tayari uko salama.

pakua/download  app yetu hapa uwe wa kwanza kila siku kuona makala zetu kwenye simu yako http://www.tiny.cc/sirizaafyabora kisha share na marafiki.


                                                                  STAY ALIVE

                                   DR,KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                       0653095635/0769846183

FAHAMU JINSI YA KUCHELEWESHA SIKU ZAKO ZA HEDHI WAKATI HUZIHITAJI.

kuchelewesha siku za hedhi ni nini?
hii ni hali ya kuzuia siku zako za hedhi kutoka kwa muda fulani mpaka utakapokua tayari kuzipata.
                                                                   
kwanini wanawake hucheewesha siku hizi za hedhi?
sababu mbalimbali huchangia wanawake kuchelewesha siku zao za hedhi kama ifuatavyo..

  • siku hizo kuangukia kipindi ambacho yuko bize sana mfano kipindi cha mitihani au majukumu fulani.
  • maumivu makali ya hedhi ambayo yanaweza kuzuia shughuli muhimu unayotaka kufanya mwezi huo.
  • siku hizo za hedhi kutaka kutokea wakati wa honey moon baada ya ndoa kitu ambacho kikapoteza raha ya siku ile muhimu.
  • siku za hedhi kutaka kutokea kipindi ambacho mpenzi wako anayeishi  mbali sana anafika kuja kukuona.
  • kutaka kutokea kipindi wewe ni mgonjwa na maumivu ya hedhi yatakufanya uzidiwe kabisa.
njia gani hutumika kuchelewesha hedhi?

dawa za norethisterone hutumika kuzuia hedhi kwa kuzuia ukuta wa kizazi kutoa damu siku ya hedhi inapofika, dawa hii ina kiasi kikubwa cha homone ya progesterone ambayo ni maalumu kwa kazi hiyo.

jinsi ya kutumia.
siku tatu kabla ya kuanza kuona siku zako za hedhi, meza kidonge kimoja kutwa mara tatu na kisha endelea na dozi mpaka utakapokua tayari kupata hedhi.
siku ukiacha kutumia dawa, utakaa siku mbili mpaka tatu ndio utaanza kuona damu za hedhi.

watu gani hawaruhusiwi kumeza dawa hizi?
  • wajawazito
  • wanaonyonyesha
  • wenye kisukari
  • saratani mbalimbali
  • wenye matatizo ya kuganda kwa damu
  • maumivu makali ya kichwa[migraine headache]
  • kutokwa na damu ovyo sehemu za siri  na chanzo chake hakifahamiki.
onyo; dawa hizi hazitumiki kuzuia mimba na usitumie mara kwa mara kama dawa zingine, ni vizuri kutumia mara chache.

                                                              STAY ALIVE

                                     DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                 0653095635/0769846183