data:post.body JE? NI KWELI MAZIWA YANASAFISHA MAPAFU BAADA YA KUVUTA HEWA CHAFU? ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

JE? NI KWELI MAZIWA YANASAFISHA MAPAFU BAADA YA KUVUTA HEWA CHAFU?

Katika mazingira ya kitanzania sio ajabu kusikia kwamba mtu ambaye ametoka sehemu yenye vumbi sana, hewa chafu sana au kuvuta sigara anaambiwa anywe maziwa ili yaingie ndani yasafishe mapafu.
ni kitu ambacho kila mtu amekua amekisikia tangu utotoni na kukifuata bila kuhoji kwa undani ili kupata ufumbuzi.                                       

ukweli ni upi?
kimsingi hakuna mahusiano kati ya maziwa na kusafisha mapafu, lakini pia maziwa yana kirutubisho kinaitwa casomorphin ambacho kimeonekana kutengeneza utando au kamasi kwenye utumbo wa binadamu lakini pia wataalamu wamewahi kutest maabara na kugundua kwamba utando huo unatokea kwenye mapafu pia.
sasa katika hali ya kawaida huwezi kuongeza utando kwenye mapafu na kutegemea kwamba vumbi ndio litatoka, zaidi ndio litaganda kabisa huko.
baaadhi ya vyakula ambavyo havishauriwi kabisa kwa watu wenye magonjwa ya mapafu ya muda mrefu ni maziwa.
kwa mantiki hii hakuna sababu ya kuendelea kuamini kwamba maziwa yanasafisha mapafu.

nini cha kufanya ili usafishe mapafu baada ya kutoka sehemu yenye uchafu sana?
kunywa maji mengi kuongeza mzunguko wa damu mwilini lakini pia kaa sehemu yenye uwazi yenye hewa safi na mapafu yako yataanza kua safi yenyewe lakini pia fanya mazozi ya kuvuta pumzi kwa nguvu na kuiachia.
         
                                                      STAY ALIVE
                         DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

                                      0760846183/0653095635

0 maoni:

Chapisha Maoni