Watanzania wengi kama sio wote wanafahamu kwamba mtu akinywa sumu basi matibabu ya haraka ni maziwa.
hichi ni kitu ambacho kimetulea na mpaka leo tunafanya hivyo katika maisha yetu ya kila siku yaani akitokea mtu amekunywa sumu basi matibabu yake ni maziwa.
bahati mbaya katika matibabu haya sidhani kama kuna mtu ambaye ameshawahi kuchunguza na kuangalia matokeo ya matibabu ya hao watu wanaokunywa maziwa kama ni mazuri au mabaya.
ukweli ni upi?
kiukweli maziwa sio dawa ya sumu, yaani nafasi ya maziwa kwenye kutumika mtu akinywa sumu haina tofauti kubwa sana na maji ya kunywa.
sumu pekee ambayo mtu anaweza kunywa kisha maziwa au maji yakamsaidia ni tindikali tu ambayo inaweza kupunguzwa nguvu na maziwa.[acid vs base].
sumu zingine vipi?
sumu zingine zote unazofahamu wewe hazisaidiwi kwa chochote na maziwa, yaani kitu pekee ambacho unaweza kumsaidia mtu aliyekunywa sumu za aina tofauti ni kumpeleka hospitali haraka.
hii ni kwasababu kwamba sumu karibia zote hua zina dawa yake maalumu hospitali ambayo kazi yake ni kupambana na sumu uliyotumia kitaalamu kama antidote.
lakini pia hata kama dawa ya sumu uliyotumia haipo hospitali, wao wanafahamu njia gani wanaweza kukusaidia kuindoa sumu ikiwa bado iko tumboni kabla haijasambaa mwilini,[gastric lavage] sio njia hizi za kienyeji za kutapisha watu ambazo zina madhara zaidi kwa mgonjwa.
mfano wa sumu zingine ambazo maziwa hayawezi kusaidia ni..
hichi ni kitu ambacho kimetulea na mpaka leo tunafanya hivyo katika maisha yetu ya kila siku yaani akitokea mtu amekunywa sumu basi matibabu yake ni maziwa.
bahati mbaya katika matibabu haya sidhani kama kuna mtu ambaye ameshawahi kuchunguza na kuangalia matokeo ya matibabu ya hao watu wanaokunywa maziwa kama ni mazuri au mabaya.
ukweli ni upi?
kiukweli maziwa sio dawa ya sumu, yaani nafasi ya maziwa kwenye kutumika mtu akinywa sumu haina tofauti kubwa sana na maji ya kunywa.
sumu pekee ambayo mtu anaweza kunywa kisha maziwa au maji yakamsaidia ni tindikali tu ambayo inaweza kupunguzwa nguvu na maziwa.[acid vs base].
sumu zingine vipi?
sumu zingine zote unazofahamu wewe hazisaidiwi kwa chochote na maziwa, yaani kitu pekee ambacho unaweza kumsaidia mtu aliyekunywa sumu za aina tofauti ni kumpeleka hospitali haraka.
hii ni kwasababu kwamba sumu karibia zote hua zina dawa yake maalumu hospitali ambayo kazi yake ni kupambana na sumu uliyotumia kitaalamu kama antidote.
lakini pia hata kama dawa ya sumu uliyotumia haipo hospitali, wao wanafahamu njia gani wanaweza kukusaidia kuindoa sumu ikiwa bado iko tumboni kabla haijasambaa mwilini,[gastric lavage] sio njia hizi za kienyeji za kutapisha watu ambazo zina madhara zaidi kwa mgonjwa.
mfano wa sumu zingine ambazo maziwa hayawezi kusaidia ni..
- sumu ya panya
- sumu ya mafuta ya taa.
- sumu ya oyaga
- sumu ya dawa
- sumu za wanyama
- sumu za chakula
- sumu za bacteria mbalimbali
- sumu zingene zote unazozijua wewe.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
0 maoni:
Chapisha Maoni