data:post.body LIFAHAMU TATIZO LA KUTOKWA NA DAMU NYINGI SANA WAKATI WA HEDHI NA MATIBABU YAKE. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

LIFAHAMU TATIZO LA KUTOKWA NA DAMU NYINGI SANA WAKATI WA HEDHI NA MATIBABU YAKE.

menorahgia ni nini?
hili ni tatizo la kutokwa na damu nyingi sana na kwa muda mrefu kipindi cha sili za hedhi, baadhi ya wanawake husumbuliwa na tatizo hili kitu ambacho huwakosesha amani na kushindwa kufanya shughuli zao za kawaida,
                                                                         

dalili za tatizo hili..

  • kujaza pedi moja damu ndani ya saa moja kwa muda wa saa kadhaa.
  • uhitaji wa kutumia pedi mbili kuzuia damu ya hedhi.
  • kuamka usiku ili kubadilisha pedi.
  • kutokwa damu zaidi ya wiki moja.
  • kushindwa kufanya shughuli zako sababu ya damu nyingi.
  • dalili za upungufu wa damu kama kuchoka sana, kushindwa kupumua vizuri na uchovu.
                                         chanzo cha tatizo hili.
magonjwa mbalimbali yanaweza kupelekea tatizo hili, ni vizuri kufanya uchunguzi wa kina ili kujua chanzo halisi cha tatizo hili ili kufanya matibabu ya uhakika.
tatizo la homoni; ili mwanamke akae kwenye mzunguko sahihi ambao unaeleweka lazima viwango vya homoni za oestrogen na progesterone viwe katika kiwango sahihi.
homoni hizi zikiwa kwenye kiwango ambacho sio sahihi damu nyingi huanza kutoka na kupelekea tatizo hili.
matatizo ya ovary; kama ovary zako zikishindwa kutoa mayai siku za hatari[anaovulation], mwili wako hauwezi kutoa homoni ya progesterone na hii huweza kupelekea kutokwa na damu nyingi sana siku ya hedhi.
uvimbe ndani ya kizazi;  uvimbe wowote ndani ya kizazi huweza kusababisha damu kutoka nyingi sana, mfano polyps, saratani  kizazi, fibroids.
kuharibika kwa mimba; wakati mwingine mwanamke anaweza kupata mimba bila kujua, akahisi labda siku zake zimechelewa tu lakini baadae akaona siku zake zinatoka na damu nyingi na mabonge.
hiii ni dalili kwamba mimba imeharibika na sio hedhi ya kawaida.
matatizo ya kuvuja damu ya kurithi; baadhi ya magonjwa ya kurithi ambayo husababisha damu kutoka nyingi kuliko kawaida pale mtu anapokua amejikata, pia huweza kupelekea tatizo hili.
mfano haemophilia diseases.
dawa; baadhi ya dawa za homoni[dawa za uzazi wa mpango], dawa za maumivu mfano [aspirini, diclofenac ] na dawa za kulainisha damu kama warfin huweaza kuleta tatizo hili.
baadhi ya magonjwa;  baadhi ya magonjwa ya figo na maini huweza kuleta tatizo hili.

                                                vipimo vinavyoweza kufanyika..

  • kipimo cha damu; kipimo hichi hufanyika ili kupima uwezo wa damu kuganda ili kuhakikisha kama mgonjwa ana matatizo uwezo wa damu kushindwa kuganda anapokua ameumia lakini pia huangalia kama umepata upungufu wa damu mwilini.
  • pap smear; hichi ni kipimo cha mlango wa uzazi kuangalia kama kuna dalili za magonjwa ya saratani.
  • biopsy; hichi nikipimoambacho sehemu ya nyama ya mlango wa uzazi au ndani ya kizazi huchukuliwa kwenda kupima kuangalia kama kuna saratani imeanza.
  • utrasound; hichi ni kipimo cha kuangalia sehemu za uzazi kama kizazi, mirija ya uzazi, mayai na mlango wa uzazi.
                                                                         matibabu
matibabu ya kuvuja damu nyingi kipindi cha hezi hutegemea na chanzo cha ugonjwa husika, baadhi ya matibabu yatolewayo ni kama ifuatavyo..
non steroidal ant inflamatory drugs; mfano wa dawa hizi ni ibuprofen, na naproxaten...dawa hizi hupunguza kiasi cha damu kinachotoka na kupunguza maumivu makali ya siku za hedhi,
dawa za uzazi wa mpango; dawa hizi za zina homoni ambazo huweza kurekebisha tatizo  la kutokwa damu nyingi kipindi cha hezi.
kitanzi; kitanzi cha uzazi wa mpango hupunguza ukubwa wa ukuta wa kizazi[endometrium] na kupunguza wingi wa damu.
tranexanamic acid; hupunguza kiasi cha damu siku za hedhi lakini imezwe siku za hedhi tu.

                                                       matibabu mengine
kama matibabu hayo juu yakishindikana kuna matibabu mengine huweza kutolewa kupambana na hali hi kama ifuatavyo.
dilatation and curratage; hii ni njia ya kusafisha sehemu za siri kwa kutumia vifaa maalumu, mara nyingi hufanyika mimba inapokua imeharibika na baadhi ya nyama hazijatoka.
uterine artery embolization; kwa akina mama ambao wa uvimbe kwenye vizazi vyao ambavyo vinatoa damu, mshipa wa damu unaopeleka damu kwenye kizazi huweza kufungwa ili kuzuia hali hiyo.
myomectomy; huu ni upasuaji unaofanyika kuondoa uvimbe[fibroids[ ndani ya kizazi kwa mwanmke ambaye anatokwa na damu nyingi sana kwasababu ya kua na uvimbe huo.
endometrial ablation; huu ni upasuaji wa kuondoa sehemu ya ndani kabisa ya kizazi ambayo inahusika na kuvuja damu wakati wa hedhi.
hysterectomy; huu ni upasauji wa kuondoa kizazi, unaweza kutoa kizazi tu au kutoa kila kitu yaani kizazi, mlango wa uzazi, mrija ya uzazi na mayai.

                                                                   STAY ALIVE

                                   DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                               0653095635/0769846183






0 maoni:

Chapisha Maoni