data:post.body JINSI UNAVYOWEZA KUPUNGUZA UZITO KWA KULA VYAKULA VYA MAFUTA.[ketogenic diet] ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

JINSI UNAVYOWEZA KUPUNGUZA UZITO KWA KULA VYAKULA VYA MAFUTA.[ketogenic diet]

Dunia nzima iliaminishwa zamani kwamba watu wanaonenepa ni wanaokula vyakula vya mafuta, kitu ambacho kimeonekana sio kweli baada ya tafit nyingi za hivi karibuni.
                                                             
kimsingi uzito unaongezwa na ulaji mkubwa wa vyakula vya wanga na sukari kwa ujumla lakini ulaji wa vyakula vya mafuta unasababisha kupungua uzito na sio kuongezeka.

ketogenic diet ni nini?
hii ni diet ambayo inakua na asilimia 75% ya vyakula vya mafuta, asilimia 20 vyakula vya protini huku asilimia tano tu ndio vyakula vya wanga.
hii ina maana kwamba badala ya kula sahani moja ya wali na samaki au nyama kidogo basi unakula sahani moja ya nyama na wali kidogo au ugali mdogo sana na wakati mwingine unaweza kula nyama tupu au samaki tupu mboga za majani na matunda.
kimsingi hii ni moja ya njia pekee mtu anaweza kupungua uzito bila kufanya mazoezi kabisa.

ketogenic diet inafanya vipi kazi?
kwa kawaida mwili wa binadamu hutumia glucose kutoka kwenye vyakula vya wanga na sukari kukupa nguvu, na glucose ikibaki hubadilishwa kua mafuta na kuhifadhiwa sehemu mbalimbali za mwili.
sasa unapokula vyakula vya mafuta kwa wingi inafika hatua wanga ni kidogo mwilini, mwili unaanza kutumia mafuta mwilini mwako ili kutengeneza nguvu.
hali hii kitaalamu inaitwa  ketosis yaani kunakua kumetengenezwa vitu ambavyo vinaitwa ketones sababu ya uchomaji wa mafuta mwilini.
ukitaka kujua umeingia kwenye ketosis nenda kapime mkojo na utaambiwa kuna ketone bodies kwenye mkojo wako na hiyo ni dalili nzuri.
ukiendelea na diet hii mwili utandelea kuchoma mafuta kutengeneza nguvu na ndipo hapo uzito wako unaanza kupungua kwa kasi sana.
lakini pia diet hii inakufanya ujisikie kushiba muda wote na kukosa hamu ya kula kwani mafuta yanakaa sana tumboni hii itakufanya usile  sana tofauti na ulaji wa vyakula vya wanga ambao unamfanya muhusika apende zaidi kula kwani hamu yake ya kula inaongezeka.
mwanzoni diet hii inaweza kua ngumu kidogo kwa kujisikia umeshiba lakini huna nguvu za kutosha lakini hali hii itaisha.

faida zingine za ketogenic diet ni zipi?
ketogenic diet imeanza kutumika kutibu magonjwa mengine mbalimbali kama ifuatavyo
magonjwa ya moyo; diet hii inapunguza cholestrol au lehemu mbaya mwilini, kupunguza sukari na mafuta mwilini na kukufanya uwe na afya bora zaidi.
kifafa; tafiti zinaonyesha kwamba diet hii inapunguza sana mgonjwa wa kifafa kuanguka mara kwa mara na kumfanya aishi masiha ya kawaida.
kisukari; diet hii huwasaidaia wagonjwa wa kisukari kupungua uzito, kushusha kiasi cha sukari  na homoni ya insulini mwilini, hali hii hufanya uwezo wa insulini kufanya kazi huongezeka.
taiti zilizofanyika zimegundua kwamba kati ya watu 24 wenye kisukari waliotumia diet hii basi 7 kati yao waliacha dozi kabisa na 92% walipunguza dozi ya dawa.
lakini pia wengi wao walipungua uzito kwa kilo 11.
chunusi; diet hii huondoa kabisa chunusi na kuiacha ngozi yako kama ya mtoto mdogo.
alzheimers disease;  huu ni ugonjwa wa mfumo wa ubongo ambao humfanya mgonjwa kusahau kila kitu, huweza kupata nafuu kwa diet hii.
ajali ya kichwa; watu waliopoteza fahamu kwa kuumia kichwani huweza kupata nafuu haraka kwa kuanzishiwa diet hii.
polycystic ovarian syndrome; wagonjwa wenye uvimbe kwenye mayai ya uzazi huweza kupata nafuu kwa diet hii kwani hupunguza sana kiasi cha insulini mwilini.
parkinston disease; huu ni ugonjwa wa kutetemeka mikono sababu ya matatizo ya kwenye ubongo na mishipa ya fahamu, huweza kupata nafuu kwa diet hii.

vyakula gani vya kutumia ukitaka kufuata diet hii?

  • nyama
  • samaki
  • mayai
  • maparachichi
  • karanga na korosho
  • mboga za majani
  • siagi
  • mafuta ya kula ya asili.
  • maziwa
vyakula gani vya kuepuka?
  • vyakula vyote vya sukari mfano keki,soda, ice cream, pipi, jojo na kadhalika
  • wali, tambi, ugali, 
  • maharage,njegere
  • viazi vitamu,chipsi,ndizi
  • punguza mafuta ya kutengeneza viwandani mfano mayonise na mengine ya kula
  • pombe; kwani nyingi zina wanga wa kukuondoa kwenye diet
  • sugar free diet; hivi ni vyakula na vinywaji ambavyo vimetengenezwa kiwandani bila sukari lakini vina sugar alcohol ambayo sio nzuri. mfano pepsi diet au coca zero.
  • matunda yote yenye sukari mfano machungwa,embe, ndizi, tikiti maji, chenza  na kadhalika.
  • asali
madhara gani madogomadogo unapoanza diet hii?
ukianza diet hii unaweza kua unapata njaa wakati mwingine hivyo jitahidi kunywa maji mengi, kuishiwa nguvu, mafua, kukosa usingizi, kushindwa kufanya mazoezi, na akili kushindwa kufanya kaz kwa makini.
kupunguza madhara haya unatakiwa ule vyakula vya wanga kidogo na diet hio kwa wiki chache za kwanza mpaka utakapozoea hali hii.

je hutakiwi kula tena vyakula nilivyokataza?
mwanzoni hutakiwi uvile kabisa na kama ukila iwe kwa kiasi kidogo sana kama unaona unaishiwa nguvu lakini baada ya miezi mitatu unaweza kula chakula kama sasa hivi kwenye siku maalumu kabda harusi au sherehe fulani lakini unarudi haraka kwenye diet yako.


kuna madhara ya diet hii?
watu wengi huchanganya ketoacidosis ambayo ni hali ya hatari kwa watu wenye sukari na ketosis ambayo ni kawaida kabisa kwa binadamu wa kawaida hivyo hakuna madhara yeyote.

mfano wa mpangilio wa chakula.
asubuhi; yai moja,mbili hata tano ya kuchemshwa au kukaangwa na maziwa ambayo hayana sukari.
mchana; nyama ya ngombe au dagaa au kuku au samaki,parachichi na mboga za majani.
usiku kabla ya saa moja; nyama au dagaa au  kuku au samaki, mboga za majani.

NB; huo juu ni mfano tu, unaweza kuchanganya vyakula unavyopenda kulingana na vyakula unavyovipata kwako, kama hauli chakula kingine chochote unaweza kula hata mayai 15 kwa siku. yaani matano asubuhi, mtano mchana matano jioni.
mfumo wa ulaji wa kiafrika wa kula wanga zaidi ndio chanzo kikuu cha unene katika nchi zetu hata ulaya.


                                                                  STAY ALIVE

                                         DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                      0653095635/0769846183

0 maoni:

Chapisha Maoni