data:post.body HIVI NDIO JINSI MWANAUME ANAVYOWEZA KUNASA KWENYE UKE WA MWANAMKE.[PENIS CAPTIVUS] ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIVI NDIO JINSI MWANAUME ANAVYOWEZA KUNASA KWENYE UKE WA MWANAMKE.[PENIS CAPTIVUS]

Watu wengi ambao hua wanasikia kwamba mwanaume amenasa kwenye uke wa mwanamke hua wanadhani labda kuna mambo ya kishirikina yamehusika hasa kama ni mme au ni mke wa mtu kitu ambacho hua sio kweli.
tatizo la uume kunaswa kwenye uke sio hadithi au imani kama watu wanavyofikiri, ila ni tatizo la kweli kabisa ambalo limewapata watu wachache sana tangu dunia kuumbwa.
hali hiyo huweza kuaibisha sana hasa pale ambapo inatakiwa kwenda hospitali kupata msaada.

nini kinasababisha uume kunasa kwa mwanamke?
kwa hali ya kawaida uume ukiwa ndani ya uke wa mwanamke huendelea kupata damu nyingi ili uendelee kua na nguvu ya kushiriki tendo la ndoa.
lakini pia mwanamke akifika kileleni misuli ya uke hujikunja sana kiasi kwamba mwanaume unaweza kuisikia hali ile kwa muda wa sekunde kadhaa na baadae kuachia.
katika hali ambayo sio ya kawaida misuli ya uke wa mwanamke huendelea kubana sana na uume kuendelea kusimama.
hali husababisha uume kushindwa kutoka kabisa na kujikuta watu wakipelekwa hospitali kuomba msaada wa kimatibabu.

je kuna ulazima sana wa kwenda hospitali hali hii ikitokea?
hali hii ikitokea mara nyingi wapenzi hupaniki sana na kupaniki kule hufanya hali ile iendelee kua mbaya zaidi.
lakini kawa waki relax na kutuliza mawazo na kuanza kufikiria mambo mengine basi hali ile huweza kuisha kabisa bila matibabu yeyote.

watu wangapi wamepatwa na hali hii?
historia inaonyesha ni watu wachache sana ambao wameshapatwa na hali hii, kimsingi wanyama hasa mbwa wamekua wakipata tatizo hili kuiko viumbe wengine wowote wale.
japokua uwezekano wa mtu kupata hali hii na mtu wake wakati wa tendo la ndoa ni mdogo sana lakini sio kwamba haiwezekani kabisa kutokea.
Mwaka 1980 Dr.Brendan Musgrave aliandika ripoti muhimu kwenye jarida la british medical journal kwamba kwa uzoefu wake mwenyewe akiwepo hospitali ya royal isle aliwahi kuona hali hii.
Anasema "nakumbuka niliona ambulance ikileta mke na mme waliokua honeymoon wakiwa wameshikana kwenye machela moja, bahati nzuri tuliweza kuwasaidia".
Mwaka 2016 hali kama hii pia ilionekana kenya ambapo inadaiwa kwamba muhisika mmoja alikua mke wa mtu, watu hawa walichukuliwa na kupelekwa kwa waganga wa kienyeji ambapo inasemekana walifanikisha kuwatenganisha.
Nchini china mzee mmoja mtu mzima alinasa kwenye uke wa mwanamke anyejiuza kisha akapata mshutuko wa moyo na kufariki hapohapo, mwanamke huyo ilibidi apelekwe hospitali ili kuweza kunasuliwa kutoka kwenye mwili huo.

matibabu gani hufanyika hospitali?
Mara nyingi watu hawa hupewa dawa za usingizi na za kulegeza misuli[muscle relaxant] na baada ya muda hurudi katika hali ya kawaida.
hakuna ushahidi wa hali hii kuhusika na mambo ya kishirikina, ila ni kitu ambacho kina maelezo ya kitaalamu kabisa ya kujieleza.

jinsi gani ya kuzuia hali hii?
kama nilivyosema hapo mwanzo, wahusika wanatakiwa wa relax baada ya hali hii kutokea na kusubiri kwa muda fulani.
na hali hii huweza kuisha yenyewe, japokua ndio hivyo kwa akili ya kawaida watu wanashindwa kurelax hali hii haiwezi kuisha yenyewe kwani watu wengi wanakua wameshachangayikiwa muda huo.


                                                               STAY ALIVE

                                          DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO   
                                                          0653095635/0769846183


0 maoni:

Chapisha Maoni