Kwa miaka mingi ugonjwa wa sikoseli umekua tishio na mateso kwa wahanga na wanafamilia wa watu wanaoumwa ugonjwa huu.
ugonjwa huu wa kurithi kama tunavyofahamu hua hauna dawa ya kuutibu kabisa ila dawa za kupunguza makali.
wanasayansi wamekaa na kuumiza sana vichwa kwa miaka mingi kupata mwarobaini wa tatizo hili ambalo linawasumbua sana vichwa.
miaka ya hivi karibuni kumetokea ugunduzi ambao umelenga kupunguza magonjwa mengi duniani na kuwafanya binadamu kua imara zaidi kitaalamu kama gene therapy.
sisi wote tunatambua kwamba magonjwa yote hushambulia binadamu kulingana na uimara wa yeye alivyoumbwa yaani genes.
kuna watu ni wepesi sana kuugua na wengine ni wagumu sana kuugua na hii ni sababu ya gene ambazo tunarithi kutoka kwa wazazi wetu.
gene therapy ni teknolojia iliyojipanga kubadisha au kuzifuta gene ambazo sio imara na kuweka zile ambazo ni imara.
hivyo tunategemea vizazi vijavyo vitakua na gene imara kupambana na magonjwa ambayo yanatutesa sana sasa hivi kutokana na unyonge wetu wa kimaumbile.
teknolojia hii inatumika vipi kwa wagonjwa wa sickle cell?
sasa teknolojia hii itatumika kulingana na chanzo cha ugonjwa husika, hivyo kwa upande wa sikoseli ugonjwa ambao mifupa kitaalamu kama bone marrow inayotengeneza seli ambazo katika mazingira fulani ya kukosa hewa ya oxygen ya kutosha hubadilika shepu na kua kama mundu au mwezi..
basi mgonjwa huyu atabadilishiwa vitengeneza damu au bone marrow hizo na kuwekewa zile nzima ambazo zinatoa seli nzima.
kazi hii inafanyika vipi?
kwanza mgonjwa hupewa dawa za kuua bone marrow zake kitaalamu kama chemotherapy, baada ya hapo bone marrow zake zote ambazo zinatoa seli za sikoseli zinakua zimekufa kisha huwekewa bone marrow mpya kutoka kwa mtu ambaye anakua amejitolea kumchangia, [mara nyingi mtu huyu anatakiwa awe ndugu yake wa tumbo moja na baba mmoja ambaye ni mzima na damu yake inafanana na ndugu yake mgonjwa].
bone marrow hizi huingizwa kupitia mishipa ya damu kama jinsi mtu anavyoongezewa damu ya kawaida na baada ya hapo hizo bone marrow mpya zinaanza kutengeneza seli mpya na mgonjwa anakua amepona kabisa.
kazi hii inachukua muda gani?
kazi hii huweza kuchukua wiki kadhaa mpaka miezi, mgonjwa anatakiwa aendelee kuwepo karibu na wataalamu ambao wamefanya hiyo kazi yaani transplant team ili wamfuatilie kwa muda mrefu na kuangalia kama kuna madhara anapata ili yaweze kutibika.
timu hii ikishajiridhisha kama mgonjwa amepona unaweza kurushusiwa kwenda nyumbani.
kuna ushahidi wa hichi kitu?
march 3 mwaka 2017 jarida la new england journal of medicine liliandika kwamba mgonjwa wa kwanza wa duniani hatimaye amepona kabisa sikoseli, kazi hiyo ilifanyika nchini ufaransa ambapo matibabu yalianza mvulana huyo akiwa na miaka 13 na alipofikisha miaka 15 alikua hana dalili zozote za ugonjwa huu kwa vipimo na dalili hivyo aliachishwa dawa zote za sikoseli.
"tangu amefanyiwa matibabu hajaonyesha dalili yeyote ya kuugua, hajaongezewa damu, maumivu yameisha na anacheza michezo shuleni na hii inatupa uhakika kwamba mtoto huyu amepona kabisa" alizungumza Dr.Philipe Leboulch ambaye ni profesa wa medicine katika chuo kikuu cha paris.
baada ya hapo nchi mbalimbali zilianza kuripoti kufanikiwa kwa kitu hicho na kuleta matumaini kwa wagonjwa hawa.
nini madhara ya matibabu haya?
kutokana na madhara ya matibabu haya mara nyingi wanashauri yatumike kwa mgonjwa ambaye ugonjwa unamsumbua sana.
madhara kama kutokwa na damu nyingi, matibabu kufeli na ugonjwa kurudi, na kifo huwezi kutokea hivyo ukiamua matibabu haya lazima uwe tayari kwa lolote.
japokua wataalamu wanaamini miaka ijayo wataweza kupunguza madhara haya kutokana na tafiti zinazoendelea.
ni wapi unaweza kupata huduma hii?
huduma hii hupatikana nchi zilizoendelea kama south africa, marekani, india, ufaransa na kadhalika na gharama yake huanzia shilingi milioni mia saba mpaka bilioni moja na milioni mia mbili, inategemea na nchi au hospitali.
lakini hapa nchini kwetu hakuna huduma hii.
tunategemea mabadiliko ya teknolojia yataleta mapinduzi ya matibabu huko mbeleni na huenda huduma hizi zitaweza kuwafikia maskini wa nchi za kiafrika ambao ndio wahanga wakuu kwa gharama ndogo miaka ijayo.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
[0653095635/0769846183]
ugonjwa huu wa kurithi kama tunavyofahamu hua hauna dawa ya kuutibu kabisa ila dawa za kupunguza makali.
miaka ya hivi karibuni kumetokea ugunduzi ambao umelenga kupunguza magonjwa mengi duniani na kuwafanya binadamu kua imara zaidi kitaalamu kama gene therapy.
sisi wote tunatambua kwamba magonjwa yote hushambulia binadamu kulingana na uimara wa yeye alivyoumbwa yaani genes.
kuna watu ni wepesi sana kuugua na wengine ni wagumu sana kuugua na hii ni sababu ya gene ambazo tunarithi kutoka kwa wazazi wetu.
gene therapy ni teknolojia iliyojipanga kubadisha au kuzifuta gene ambazo sio imara na kuweka zile ambazo ni imara.
hivyo tunategemea vizazi vijavyo vitakua na gene imara kupambana na magonjwa ambayo yanatutesa sana sasa hivi kutokana na unyonge wetu wa kimaumbile.
teknolojia hii inatumika vipi kwa wagonjwa wa sickle cell?
sasa teknolojia hii itatumika kulingana na chanzo cha ugonjwa husika, hivyo kwa upande wa sikoseli ugonjwa ambao mifupa kitaalamu kama bone marrow inayotengeneza seli ambazo katika mazingira fulani ya kukosa hewa ya oxygen ya kutosha hubadilika shepu na kua kama mundu au mwezi..
basi mgonjwa huyu atabadilishiwa vitengeneza damu au bone marrow hizo na kuwekewa zile nzima ambazo zinatoa seli nzima.
kazi hii inafanyika vipi?
kwanza mgonjwa hupewa dawa za kuua bone marrow zake kitaalamu kama chemotherapy, baada ya hapo bone marrow zake zote ambazo zinatoa seli za sikoseli zinakua zimekufa kisha huwekewa bone marrow mpya kutoka kwa mtu ambaye anakua amejitolea kumchangia, [mara nyingi mtu huyu anatakiwa awe ndugu yake wa tumbo moja na baba mmoja ambaye ni mzima na damu yake inafanana na ndugu yake mgonjwa].
bone marrow hizi huingizwa kupitia mishipa ya damu kama jinsi mtu anavyoongezewa damu ya kawaida na baada ya hapo hizo bone marrow mpya zinaanza kutengeneza seli mpya na mgonjwa anakua amepona kabisa.
kazi hii inachukua muda gani?
kazi hii huweza kuchukua wiki kadhaa mpaka miezi, mgonjwa anatakiwa aendelee kuwepo karibu na wataalamu ambao wamefanya hiyo kazi yaani transplant team ili wamfuatilie kwa muda mrefu na kuangalia kama kuna madhara anapata ili yaweze kutibika.
timu hii ikishajiridhisha kama mgonjwa amepona unaweza kurushusiwa kwenda nyumbani.
kuna ushahidi wa hichi kitu?
march 3 mwaka 2017 jarida la new england journal of medicine liliandika kwamba mgonjwa wa kwanza wa duniani hatimaye amepona kabisa sikoseli, kazi hiyo ilifanyika nchini ufaransa ambapo matibabu yalianza mvulana huyo akiwa na miaka 13 na alipofikisha miaka 15 alikua hana dalili zozote za ugonjwa huu kwa vipimo na dalili hivyo aliachishwa dawa zote za sikoseli.
"tangu amefanyiwa matibabu hajaonyesha dalili yeyote ya kuugua, hajaongezewa damu, maumivu yameisha na anacheza michezo shuleni na hii inatupa uhakika kwamba mtoto huyu amepona kabisa" alizungumza Dr.Philipe Leboulch ambaye ni profesa wa medicine katika chuo kikuu cha paris.
baada ya hapo nchi mbalimbali zilianza kuripoti kufanikiwa kwa kitu hicho na kuleta matumaini kwa wagonjwa hawa.
nini madhara ya matibabu haya?
kutokana na madhara ya matibabu haya mara nyingi wanashauri yatumike kwa mgonjwa ambaye ugonjwa unamsumbua sana.
madhara kama kutokwa na damu nyingi, matibabu kufeli na ugonjwa kurudi, na kifo huwezi kutokea hivyo ukiamua matibabu haya lazima uwe tayari kwa lolote.
japokua wataalamu wanaamini miaka ijayo wataweza kupunguza madhara haya kutokana na tafiti zinazoendelea.
ni wapi unaweza kupata huduma hii?
huduma hii hupatikana nchi zilizoendelea kama south africa, marekani, india, ufaransa na kadhalika na gharama yake huanzia shilingi milioni mia saba mpaka bilioni moja na milioni mia mbili, inategemea na nchi au hospitali.
lakini hapa nchini kwetu hakuna huduma hii.
tunategemea mabadiliko ya teknolojia yataleta mapinduzi ya matibabu huko mbeleni na huenda huduma hizi zitaweza kuwafikia maskini wa nchi za kiafrika ambao ndio wahanga wakuu kwa gharama ndogo miaka ijayo.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
[0653095635/0769846183]
0 maoni:
Chapisha Maoni