data:post.body ZIFAHAMU DAWA KUU 6 ZINAZONENEPESHA SANA. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

ZIFAHAMU DAWA KUU 6 ZINAZONENEPESHA SANA.

tunaishi kwenye ulimwengu wa magonjwa mengi sana yasiyotibika ambayo yanakuhitaji kutumia dawa kila siku ili uweze kuishi au kutumia dawa mara kwa mara kwa ajili ya kutibu tatizo fulani la kimwili.                         
                                                               
dawa hizi ni muhimu sana kwa afya yetu lakini bahati mbaya moja ya madhara yake ni kuongezeka unene kitu ambacho watu wengi hawakipendi na ni chanzo cha magonjwa mbalimbali ya kudumu kama moyo na kisukari.
sasa sijaandika makala hii kutishia watu lakini nimeandika makala hii ili watumiaji watumie huku wakijua kwamba dawa hizi zinaweza kuwanenepesha zaidi kama ifuatavyo.
dawa za uzazi wa mpango; karne ya 20 dawa ya kwanza ya kuzuia mimba iligundulika na kuleta mapinduzi makubwa kwenye vita ya kupambana na ongezeko la watu duniani..leo hii dawa hizi zinatumika na mamilioni ya watu duniani kwa matumizi ya kila siku au kwa matumizi ya kuzuia mimba pale wanaposhiriki tendo la ndoa siku za hatar.
bahati mbaya dawa hizi zina tabia ya kuongeza hamu ya kula na kukunenepesha watumiaji...na ukifanya utafiti utagundua wanawake wengi siku hizi ni wanene ukilinganisha na wanaume.
dawa za kutibu kisukari; mtu akigunduliwa na kisukari matibabu ya kwanza sio dawa, matibabu ya kwanza ni chakula na mazoezi..
lakini kwa bahati mbaya watu wengi hukimbilia dawa baada ya kugundulika.
kinachofanyika ni kwamba sukari ikiwa nyingi kwenye damu ukampa mtu dawa ya kuipunguza sukari ile, sukari hutolewa kwenye damu na kupelekwa kwenye seli na kua mafuta huko.
sasa unapoendelea kutumia dawa hizo mafuta mengi zaidi yanaendelea kutengenezwa na dozi yako ya kutumia dawa inazidi kuongezeka sababu ya kuongezeka uzito.
dawa za kutibu presha;  baadhi ya dawa za kutibu presha zimeonekana kuhusika sana na kuongeza uzito watumiaji, mfano wa dawa hizo ni kikundi cha beta blockers kama propanolol, atenolol, carviderol na kadhalika.
dawa hizi hufanya kazi kwa kupunguza kasi ya mapigo ya mwili hii hupunguza kasi ya mwili kuchoma mafuta kitaalamu kama metabolism.
steroids; hizi ni dawa zinazotumika sana kwa shida mbalimbali kama magonjwa ya mifupa, pumu na alleji mbalimbali.
dawa hizi zina tabia ya kuzuia maji mengi kutoka mwilini kwa njia ya mkojo na kuongeza hamu ya kula.
matumizi ya muda mrefu wa dawa hizi huongeza uzito na kupunguza kinga ya mwili kwa kuzuia mwili kupambana na magonjwa.
mfano wa dawa hizi ni dexamethasone, betamethasone, predinisole, triamnisolone na kadhalika.
dawa za msongo wa mawazo; dawa mbalimbali hutumika kwa watu ambao wanasumbuliwa sana na msongo wa mawazo, dawa hizi huongeza kiasi cha homoni ya serotonin ambayo humfanya mtu awe mchangamfu muda mwingi na kupunguza hali yake ya kua kwenye mawazo mengi.
tafiti zinaonyesha kwamba dawa hzi zitakupunguza uzito kwa muda mfupi lakini uzito wako utaongezeka mara dufu baada ya muda mrefu.
mfano wa dawa hizi ni amitriptyline, prozac.fluoxetine na paroxetine.
dawa za wagonjwa wa akili; baadhi ya dawa za magonjwa ya akili zilionekana ni tishio kwa kuongeza uzito kwa mara ya kwanza tu zilipoingia sokoni, dawa hizi zina madhara ya kufanya kazi kwenye ubongo na kukuongeza sana hamu ya kula na hii ndio chanzo kikuu cha unene kwani huwezi kuvumilia kula chakula kidogo.mfano chlropromazine.
mwisho; kama unatumia baadhi ya dawa hapo juu na unahisi ni chanzo cha wewe kunenepa basi ni vema ukaongea na daktari wako ili akutafutie mbadala wa dawa hizo, japokua baadhi ya dawa zinaweza zisiwe na mbadala sahihi sana.

                                                                 STAY ALIVE

                                         DR,KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

Maoni 1 :

  1. Nikweli Dr as a Priscriber I have notice to 2 of my mental client and 1of Hyperglycaemic client...and it has been a big challenge to reverse the conditions.. Would come with the solution please.

    JibuFuta