data:post.body TATIZO LA KUOTA MATITI KWA WANAUME NA MATIBABU YAKE.[GYNACOMASTIA] ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

TATIZO LA KUOTA MATITI KWA WANAUME NA MATIBABU YAKE.[GYNACOMASTIA]

GYNACOMASTIA ni nini?
huu ni ugonjwa wa kuvimba matiti kwa wanaume unaosababisha na mvurugiko wa homoni ndani ya mwili wa binadamu.
                                                                 
homoni za oetrogen zinapokua nyingi kwa wanaume kuliko zile homoni za progesterone, mgonjwa anaweza kuvimba matiti yote mawili au akavimba titi moja.
tatizo hili hutokea pia wakati wavulana wakiwa wanabalehe kutokana na mabadiliko ya homoni lakini baadae hali hii huisha yenyewe.
kimsingi tatizo hili sio hatari kwa maisha lakini hutia aibu na kuwafanya wahusika wakose raha kabisa.

dalili za ugonjwa huu.

  • kuvimba kwa matiti na kua makubwa kama ya kike.
  • maumivu kwenye matiti ukigusa sehemu hizo.
chanzo cha tatizo hili.........
kama nilivyosema hapo mwanzo kwamba tatizo hili ni mvurugiko wa homoni za uzazi, homoni hizi zinaweza kuvurugwa na vyanzo mbalimbali kama ifuatavyo.
mabadiliko ya kawaida ya mwili; watu wengi hudhani kwamba homoni za oestrogen ni za wanawake tu kitu ambacho sio kweli, homoni hizi pia wanaume wanazo lakini kwa kiasi kidogo sasa pale homoni hizi zinapokua nyingi kuliko za zile za progesterone hali hii hutokea na wavulana wengi hupitia hali hii wakati wa kubalehe.
matumizi ya dawa; dawa nyingi sana huweza kuleta tatizo hili kama ifuatavyo,
dawa za madonda ya tumbo i,e cimetidine, omeprazole
dawa za msongo wa mawazo i.e amitriptyline
dawa za kansai.e chemotherapy
dawa za moyo i.e nifedipine, amlodipine. digoxin
dawa za kuzuia kutapika i.e metoclopramide
dawa za ukimwi i.e efavirenz
dawa za kupunguza maji mwilini i.e spironalactone
antibayotic; metronidazole
matumizi ya vilevi; baadhi ya vilevi kama pombe,bangi, methadone,na heroin ni chanzo cha kuongezeka na kukua kwa matiti.
matatizo ya kiafya;  magonjwa kama utapiamlo, magonjwa ya maini, magonjwa ya figo,, umri mkubwa, unene na kadhalika.
dawa za miti shamba; baadhi ya dawa za mitishamba ambazo zina changia utengenezaji wa homoni hizi za oestrogen zimekua zikichangia kuongezeka kwa tatizo hili.

nini madhara ya tatizo hili?
tatizo hili halina madhara yeyote sema humfanya mushusika ajisikie vibaya sana na kupata aibu.

jinsi ya kugundua ugonjwa huu.
daktari atakuchukua maelezo na kukufanyia vipimo mbalimbali kuhakikisha tatizo hili, baadhi ya vipimo hufanyika ili kuhakikisha kwamba sio magonjwa mengine ambayo yanakuja na dalili za ugonjwa kama huo..magonjwa kama saratani ya matiti, jipu au unene huweza kuja na dalili kama hizi.
vipimo kama...
  • damu
  • mamogram
  • ct scan
  • mri
  • utrasound
  • biopsy 
matibabu ya tatizo hili..
mara nyingi tatizo hili huondoka lenyewe bila matibabu yeyote japokua huweza kuchukua muda mrefu, lakini ni vyema kuondoa chanzo au kutibu chanzo cha tatizo kama kikionekana kama nilivyotaja kwenye sababu ya tatizo hili.
baadhi ya dawa za kutibu kansa ya matiti kama tamoxifen,raloxefine,arimidex zimesaidia kutibu tatizo hili kwa baadhi ya wanaume japokua dawa hizi hazikutengenezwa kwa ajili ya kazi hiyo.
kama maziwa yakishindikana kutoka au kama mtu anataka kuyatoa haraka basi upasuaji huweza kufanyika kutibu matatizo haya kitaalamu kama mastectomy au liposuction.

                                                           STAY ALIVE

                                   DR,KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                            O653095635/0769846183

Maoni 4 :